Ni kweli kabisa,nilikuwa na binti mmoja kutoka kondoa,nilikaa naye kwenye mahusiano mwaka mmoja na nusu,kumbe anafanya maushirikina yake huko ya kufa mtu,then mimi aijui lolote!
Mungu mkubwa alisafiri kwenda Mwanza kwa ndugu zake,aliniachia ufunguo wa nyumba yake,na ilikuwa haipiti siku bila kwenda kwake,(japo yeye hayupo,ila moyo ulikuwa hauwezi kustahimili bila kutia mguu pale kwake)
Siku moja nimeenda kwake,moyo wangu ukawa mzito sana,na sikujua tatizo nini,nikapiga goti pale ndani,nikasali sana kimoyo moyo,nilipomaliza nikajitupa kitandani nikiwa nimefumba macho,nilipofungua macho nikatazama sehemu anaweka mikoba yake,(palikuwa na mikoba kama 20 hivi imetundikwa kwenye vistand vyao vile)
Nikiwa nimetazama ile stand,niinuka nikachukua mkoba mmoja tu,nilipofungu mle ndani nilichoka sana,sana sanaa!
Nilikuta kuna madawa kibao,na vihirizi vidogo vidogo 3,magome ya miti,na kikaratasi kimeandikwa kama kiarabu kwa wino mwekundu!
Nilichoka sana,sikuwahi kujua kama binti mrembo kiasi kile angeweza kuwa na mambo ya kishirikina!
Kibaya zaidi,nikiwa chumbani kwake namalizia upekuzi wangu,aimu yake ikaita,akanambia najua unachofanya,nakuomba sana usinielewe vibaya!(hii iliniogopesha sana,lakini nikavaa ujasiri wa ajabu,mifawa dawa,kucha, na nywele vilivyokuwa vimefungwa fungwa pamoja na zile hirizi NIKAZICHOMA MOTO)
Kesho yake alipanda gari kurudi,nilimwambia tangu sasa kaa mbali na mimi,japo kwa bahati mbaya sana kumbe alikuwa ame-conceive,nilimuacha kwa hakika japo kwa maumivu na huruma nyingi kutokana na ujauzito!
Kwa sasa nasubiri mtoto wangu akue kue kidogo nimchukue maisha yaendelee,Kondoa sijui kwanini wanapenda sana mambo ya ushirikina!