Kuna mambo mengi yanayomfanya Mh. Tundu Lisu ang'are kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka huu. Miongoni mwa mambo hayo ni haya yafuatayo:-
1) Tukio la kunusurika kuuwawa baada ya kupigwa risasi kule Dodoma. Watu wanajiuliza "NI YEYE KWELI" aliyepigwa risasi akanusurika na kifo? Kitendo hiki pekee kinashawishi watu waende kumuona ili kujiridhisha kama kweli ni yeye.
2) Vyama vya Upinzani havikuwa vinafanya kampeni kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2015 - 2020. Sababu hii inawafanya wananchi wawe na uchu wa kutaka kusikia ni kitu gani vyama vya upinzani wataongea kwenye kampeni zao?
3) Katika kipindi cha miaka mitano kuna mambo mengi yalijitokeza ambayo hayakuwafurahisha wananchi hasa kwa yale yaliyogusa maslahi yao. Hapa wananchi huenda kwenye mikutano ya Lissu kwa lengo la kutaka kusikia ana utetezi gani juu ya maslahi yao yaliyopotea?
4) Mtu maarufu anapokuwa haonekani machoni mwa watu kwa muda mrefu, hutengeza shauku kwa wananchi ya kutaka kumuona! Mbinu hii hutumiwa mara nyingi na wasanii ambapo muda mwingi, hasa mchana, huutumia wakiwa ndani wanakariri mashairi na mistari ya nyimbo au script za tamsilia, maigizo, au muvi zao wanazotaka kurekodi. Hivyo basi, Tundu Lissu alipokuwa Ubelgiji alikuwa mafichoni, ametengeneza shauku kwa wananchi ya kutaka kumuona na kumsikiliza akitoa ushuhuda juu ya tukio lake.
5) Umahiri wa kuongea wa Mh. Tundu Lissu kwa kutumia "logic", ni sababu nyingine pia inayomfanya ang'are kwenye kampeni za mwaka huu. Ujasiri wa kuongea mambo ambayo wengine wanaogopa pia kunamfanya ang'are kwenye kampeni hizi.
NB: Mimi siyo mwanachama wa chama chochote kile na sifungamani na upande wowote. Nimeamua tu kuandika ili kuwasilisha mawazo yangu kwenye mada hii kwa jinsi ninavyoona.