Tanganyika na Zanzibar zilungana nusu, na kutengeneza Tanzania. Ni muungano nusu kwa sababu Zanzibar iligoma kuingia kwenye muungano kamili, iliendelea kuwa na Serikali yake, na inajitambulisha kama ni nchi, na tena yenye mipaka yake.
Hoja muhimu hapa, ni kwa nini kila dhuluma kubwa dhidi ya Tanganyika, wakati wote imefanyika kwa kusimamiwa na viongozi wazanzibari? Je, Tanganyia, ni kubwa jinga? Kwa nini hata wanaCCM watanganyika hawaumizwi na dhuluma dhidi ya Tanganyika?
Baadhi ya Dhuluma kubwa kabisa dhidi ya Tanganyika:
1. Uporwaji wa bandari za Tanganyika ulifanyika wakati Rais ni mzanzibari, waziri prof. Mbarawa ni mzanzibari, mwanasheria wa wizara Johari ni mzanzibari, katibu mkuu na mkurugenzi wa bandari, wote walikuwa wazanzibari. Na ikumbukwe kuwa wizara hiyo siyo ya muungano! Na uporwaji huo ulihusisha bandari za Tanganyika pekee. Kama lilikuwa ni jambo la heri, kwa kuwa wahusika wote walikuwa ni wazanzibari, kwa nini bandari za Zanzibar hazikuwa za mwanzo kupewa DPW? Uunaamini kuwa Wazanzibari walikuwa wanaipenda sana Tanganyika kuliko Zanzibar yao?
2. Uporwaji wa mbuga za wanyama na hifadhi za misitu, na kisha kugawiwa waarabu, ulifanyika wakati wa utawala wa Mwinyi (mzanzibari) na wakati wa Rais Samia (mzanzibari), Mchengerwa akiwa waziri wa utalii. Wakati wa utawala wa Nyerere, Mkapa na Kikwete, hakuna mbuga ya wanyawa wala hifadhi ya msitu aliwahi kupewa mgeni.
3. Uporwaji wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Arusha, na kisha kugawiwa waarabu umefanyika wakati wa utawala wa Samia. Sijasikia kama uwanja wa ndege Zanzibar wamepewa waarabu.
4. Mradi wa mwendokasi umeporwa na kupewa wageni wakati wa utawala wa Samia.
5. Wakati wa utawala wa Samia, ndipo tumeshuhudia wazanzibari wengi zaidi kuliko wakati wowote, wakipewa nafasi za uongozi ndani ya Tanganyika, tena kwenye zile nafasi zisizo za muungano. Wazanzibari wameteuliwa kuwa wakuu wa wilaya Tanganyika, wakati mtanganyika hawezi kuwa hata sheha huko Zanzibar.
6. Ni wakati wa utawala wa Samia, wazanzibari na waarabu wengi wamechukua maeneo makubwa ya ardhi Tanganyika, wakati watanganyika wananyimwa haki ya kumiliki hata robo eka ya ardhi Zanzibar.
NB: Tunasema huu ni uporaji wa rasilimali za Tanganyika kwa sababu hao wanaoitwa wawekezaji hawawekezi chochote cha maana. Bandari tumejenga wenyewe. DPW hawajajenga bandari yoyote. Uwanja wa ndege tumejenga wenyewe, hakuna mwarabu aliyejenga uwanja wa ndege Tanganyika. Mbuga za wanyama na misitu ametuumbia Mungu, hao wawekezaji toka Uarabuni hawajaleta hata fisi au mbweha. Barabara ya mwendokasi tumejenga wenyewe. Sasa tunawaita wawekezaji, wamewekeza nini? Hawa ni wavunaji, siyo wawekezaji.
7. Imefikia kiwango sasa, jaji mzanzibari anawaondolea watanganyika haki za kidemokrasia kwa kuzuia chama cha upinzani kufanya shughuli za siasa, lengo kwa vyovyote ni kutaka Wazanzibari waendelee kufaidika kwa kuitumia Tanganyika. Hili siyo sahihi, na siyo haki hata kidogo.
Je, kwa mazingira haya, kuna mtu yeyote anaweza kueleza kwa uwazi Zanzibar inainufaisha vipi Tanganyika katika huu muungano?
Tunahitaji sana mabadiliko kwenye muundo wa Muungano huu wa hasara. Maadamu Zanzibar imegoma kuingia kwenye Muungano kiukamilifu, basi tubakie na mahusiano kwenye maeneo fulani tu, na wazanzibari wasiwe na haki yoyote kwenye mambo yale ya Tanganyika yasiyo ya muungani. Mzanzibari anayetaka kumiliki ardhi ya Tanganyika, kwanza aukane uraia wa Zanzibar. Mzanzibari anayetaka kufanya kazi kwenye mamlaka za Serikali Tanganyika zisizo za Muungano, kwanza aukane uraia wa Zanzibar.
Fikiria, Serikali ya Zanzibar ina mwanasheria wake mkuu. Hivyo anayeitwa mwanasheria mkuu wa serikali, kiuhalisia ni mwanasheria mkuu wa Tanganyika, halafu mwanasheria huyo ni mzanzibari! Hivi Tanganyika imekosa watu kiasi cha kumtumia expatriate kuwa mwanasheria mkuu wake?
Tusikubali wageni waibeze Tanganyika. Watanganyika tuwe na uzalendo kwa Tanganyika yetu kama wazanzibari walivyo na uzalendo kwa Zanzibar yao.
Hoja muhimu hapa, ni kwa nini kila dhuluma kubwa dhidi ya Tanganyika, wakati wote imefanyika kwa kusimamiwa na viongozi wazanzibari? Je, Tanganyia, ni kubwa jinga? Kwa nini hata wanaCCM watanganyika hawaumizwi na dhuluma dhidi ya Tanganyika?
Baadhi ya Dhuluma kubwa kabisa dhidi ya Tanganyika:
1. Uporwaji wa bandari za Tanganyika ulifanyika wakati Rais ni mzanzibari, waziri prof. Mbarawa ni mzanzibari, mwanasheria wa wizara Johari ni mzanzibari, katibu mkuu na mkurugenzi wa bandari, wote walikuwa wazanzibari. Na ikumbukwe kuwa wizara hiyo siyo ya muungano! Na uporwaji huo ulihusisha bandari za Tanganyika pekee. Kama lilikuwa ni jambo la heri, kwa kuwa wahusika wote walikuwa ni wazanzibari, kwa nini bandari za Zanzibar hazikuwa za mwanzo kupewa DPW? Uunaamini kuwa Wazanzibari walikuwa wanaipenda sana Tanganyika kuliko Zanzibar yao?
2. Uporwaji wa mbuga za wanyama na hifadhi za misitu, na kisha kugawiwa waarabu, ulifanyika wakati wa utawala wa Mwinyi (mzanzibari) na wakati wa Rais Samia (mzanzibari), Mchengerwa akiwa waziri wa utalii. Wakati wa utawala wa Nyerere, Mkapa na Kikwete, hakuna mbuga ya wanyawa wala hifadhi ya msitu aliwahi kupewa mgeni.
3. Uporwaji wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Arusha, na kisha kugawiwa waarabu umefanyika wakati wa utawala wa Samia. Sijasikia kama uwanja wa ndege Zanzibar wamepewa waarabu.
4. Mradi wa mwendokasi umeporwa na kupewa wageni wakati wa utawala wa Samia.
5. Wakati wa utawala wa Samia, ndipo tumeshuhudia wazanzibari wengi zaidi kuliko wakati wowote, wakipewa nafasi za uongozi ndani ya Tanganyika, tena kwenye zile nafasi zisizo za muungano. Wazanzibari wameteuliwa kuwa wakuu wa wilaya Tanganyika, wakati mtanganyika hawezi kuwa hata sheha huko Zanzibar.
6. Ni wakati wa utawala wa Samia, wazanzibari na waarabu wengi wamechukua maeneo makubwa ya ardhi Tanganyika, wakati watanganyika wananyimwa haki ya kumiliki hata robo eka ya ardhi Zanzibar.
NB: Tunasema huu ni uporaji wa rasilimali za Tanganyika kwa sababu hao wanaoitwa wawekezaji hawawekezi chochote cha maana. Bandari tumejenga wenyewe. DPW hawajajenga bandari yoyote. Uwanja wa ndege tumejenga wenyewe, hakuna mwarabu aliyejenga uwanja wa ndege Tanganyika. Mbuga za wanyama na misitu ametuumbia Mungu, hao wawekezaji toka Uarabuni hawajaleta hata fisi au mbweha. Barabara ya mwendokasi tumejenga wenyewe. Sasa tunawaita wawekezaji, wamewekeza nini? Hawa ni wavunaji, siyo wawekezaji.
7. Imefikia kiwango sasa, jaji mzanzibari anawaondolea watanganyika haki za kidemokrasia kwa kuzuia chama cha upinzani kufanya shughuli za siasa, lengo kwa vyovyote ni kutaka Wazanzibari waendelee kufaidika kwa kuitumia Tanganyika. Hili siyo sahihi, na siyo haki hata kidogo.
Je, kwa mazingira haya, kuna mtu yeyote anaweza kueleza kwa uwazi Zanzibar inainufaisha vipi Tanganyika katika huu muungano?
Tunahitaji sana mabadiliko kwenye muundo wa Muungano huu wa hasara. Maadamu Zanzibar imegoma kuingia kwenye Muungano kiukamilifu, basi tubakie na mahusiano kwenye maeneo fulani tu, na wazanzibari wasiwe na haki yoyote kwenye mambo yale ya Tanganyika yasiyo ya muungani. Mzanzibari anayetaka kumiliki ardhi ya Tanganyika, kwanza aukane uraia wa Zanzibar. Mzanzibari anayetaka kufanya kazi kwenye mamlaka za Serikali Tanganyika zisizo za Muungano, kwanza aukane uraia wa Zanzibar.
Fikiria, Serikali ya Zanzibar ina mwanasheria wake mkuu. Hivyo anayeitwa mwanasheria mkuu wa serikali, kiuhalisia ni mwanasheria mkuu wa Tanganyika, halafu mwanasheria huyo ni mzanzibari! Hivi Tanganyika imekosa watu kiasi cha kumtumia expatriate kuwa mwanasheria mkuu wake?
Tusikubali wageni waibeze Tanganyika. Watanganyika tuwe na uzalendo kwa Tanganyika yetu kama wazanzibari walivyo na uzalendo kwa Zanzibar yao.