Haya mambo ya Lowasa na Sitta hayana maana tena kwa watanzania,mwaka mzima Richmond lakini mwisho wake ni huo wa kufunga mjadala bila ya wahusika kuwajibishwa,mimi nina sema mtendaji mkuu wa serikali awe na msimamo na ache usanii na atimize wajibu wake.
Katika kuongoza nchi haitakiwi undungunaizesheni(Nepotism na favouratism) hii inaadhiri katka kutoa maamuzi ya msingi.Lowasa alivurunda yeye akae mbali na watanzania hawezi kujiosha.
Na tunamshauri Mzee Mwinyi atumie hekima kusuluhisha hili na sio kumladhimisha Sitta kumuomba msamaha Lowasa.
Kwa sisi ambao tumesomea kozi za utatuzi wa migogoro- Msuluhishi hatakiwa kuegemea upande wowot.ni lazima awe neural - hii kamati haitafikia maamuzi yenye mafanikio.
Na Sitta akizubaa hiki kitakuwa ni kitanzi kwake,maana Lowasa ni rafiki mtendaji mkuu - hapa kazi ipo.Lakini Mungu akiwepo upande wetu tutamhofia na ni?
Lazima haki itapatikana Tanzania - Tunaiombea nchi dhidi ya hawa wavurugaji na wafujaji wa mali za watanzania
Elisante Yona