Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Mambo bado mazito Kamati ya Mwinyi
Na Mwandishi wetu
21st February 2010
Ilimwita Spika Sitta amwombe radhi Edward Lowassa
Kwa kuchelewesha kufunga mjadala wa Richmond
Kuruhusu makombora kuelekezwa kwa Lowassa na mawaziri
Spika akataa kuomba radhi ili kutunza hadhi ya wabunge
Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi
Kamati iliyoundwa na Halmashauri Kuu (NEC), ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka jana kwa ajili ya kutafuta chanzo cha uhasama na chuki baina ya wabunge wa chama hicho huenda isifanikiwe kupatanisha makambi mawili yanayotuhumiana.
Habari za ndani zinasema kuwa awali kamati hiyo ambayo inaongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, ilimwita aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, na kumtaka Spika Sitta kumwomba radhi Lowassa juu ya sakata la Richmond.
Nia ya Sitta kutakiwa kuomba radhi ni kutokana na kuchelewa kufunga mjadala wa Richmond na kuruhusu makombora kuelekezwa waziwazi kwa Lowassa na mawaziri wengine waliohusishwa na kashfa ya zabuni tata ya kufua umeme wa dharura ambayo kampuni ya Richmond ilipewa.
Taarifa zaidi zinasema kuwa Spika Sitta alikataa kuomba radhi kutokana na kashfa hiyo na kuhoji sababu za kufanya hivyo badala ya Serikali yenyewe kuwachukulia hatua watumishi wake waliolisababishia taifa hasara kutokana na kampuni `tata' ya Richmond.
Chanzo chetu kimedai kuwa, Sitta aliigomea kamati ya Mwinyi na kuhoji wananchi watalielewaje Bunge kuhusiana na sakata zima iwapo Lowassa na wenzake wangesafishwa bila kuwataja na kuwakemea wahusika wa Richmond.
"Tumejiuliza Bunge litawaeleza nini Watanzania ambao waliumizwa na Richmond, ziko wapi milioni 152 zilizokuwa zikilipwa kwa Richmond kila siku kama ‘capacity charge' au nani alihusika…Sitta ameitaka kamati hiyo kujibu maswali hayo na mengine mengi ambayo wananchi wanahoji kuhusiana na Richmond kabla hajaomba radhi," kilisema chanzo chetu.
Aidha, imedaiwa kuwa kitendo cha Spika Sitta kukataa kuomba radhi kimeendelea kuiumiza kamati ya Mwinyi pamoja na chama kwa kuwa sakata la Richmond ndio chanzo cha mpasuko ndani ya chama hicho.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema wiki hii baada ya kumalizika kwa mkutano wa NEC mjini Dodoma, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema kazi iliyobakia ni kuwakutanisha vinara wa makundi mawili yanayosuguana yaani Lowassa na Sitta. Hata hivyo, alisema mazungumzo ya usuluhisho baina ya makundi hayo mawili yanaendelea vizuri na kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kupata muafaka.
Msekwa ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Mwinyi, alisema mvutano ya makundi hayo ulianza baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya Richmond na kueleza kuwa walichobaini ni wabunge hao kulinda nafasi zao majimboni kwa kuwa wabunge wamekuwa wakituhumiana kwa kila mmoja kudai kuwa kundi moja linataka kuliong'oa lingine jimboni.
Msekwa alisema hawana nia ya kukemea wala kumvua mwanachama wake yeyote uanachama na badala yake kazi waliyonayo ni kujenga umoja na mshikamano ndani ya chama.
Huku akinukuu kifungu cha Biblia na Quran, alionya kuwa kundi ambalo halitakubali kupatanishwa na lingine, 'litaandamwa'.
Tayari Kamati ya Mwinyi imeongezewa mwezi mmoja ili iweze kuyakutanisha makundi hayo mawili na Msekwa aliahidi kuwasilisha ripoti ya kazi hiyo kwenye kikao cha Kamati Kuu kitakachofanyika mwishoni mwa Machi, mwaka huu.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Na Mwandishi wetu
21st February 2010
Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi
Kamati iliyoundwa na Halmashauri Kuu (NEC), ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka jana kwa ajili ya kutafuta chanzo cha uhasama na chuki baina ya wabunge wa chama hicho huenda isifanikiwe kupatanisha makambi mawili yanayotuhumiana.
Habari za ndani zinasema kuwa awali kamati hiyo ambayo inaongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, ilimwita aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, na kumtaka Spika Sitta kumwomba radhi Lowassa juu ya sakata la Richmond.
Nia ya Sitta kutakiwa kuomba radhi ni kutokana na kuchelewa kufunga mjadala wa Richmond na kuruhusu makombora kuelekezwa waziwazi kwa Lowassa na mawaziri wengine waliohusishwa na kashfa ya zabuni tata ya kufua umeme wa dharura ambayo kampuni ya Richmond ilipewa.
Taarifa zaidi zinasema kuwa Spika Sitta alikataa kuomba radhi kutokana na kashfa hiyo na kuhoji sababu za kufanya hivyo badala ya Serikali yenyewe kuwachukulia hatua watumishi wake waliolisababishia taifa hasara kutokana na kampuni `tata' ya Richmond.
Chanzo chetu kimedai kuwa, Sitta aliigomea kamati ya Mwinyi na kuhoji wananchi watalielewaje Bunge kuhusiana na sakata zima iwapo Lowassa na wenzake wangesafishwa bila kuwataja na kuwakemea wahusika wa Richmond.
"Tumejiuliza Bunge litawaeleza nini Watanzania ambao waliumizwa na Richmond, ziko wapi milioni 152 zilizokuwa zikilipwa kwa Richmond kila siku kama ‘capacity charge' au nani alihusika…Sitta ameitaka kamati hiyo kujibu maswali hayo na mengine mengi ambayo wananchi wanahoji kuhusiana na Richmond kabla hajaomba radhi," kilisema chanzo chetu.
Aidha, imedaiwa kuwa kitendo cha Spika Sitta kukataa kuomba radhi kimeendelea kuiumiza kamati ya Mwinyi pamoja na chama kwa kuwa sakata la Richmond ndio chanzo cha mpasuko ndani ya chama hicho.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema wiki hii baada ya kumalizika kwa mkutano wa NEC mjini Dodoma, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema kazi iliyobakia ni kuwakutanisha vinara wa makundi mawili yanayosuguana yaani Lowassa na Sitta. Hata hivyo, alisema mazungumzo ya usuluhisho baina ya makundi hayo mawili yanaendelea vizuri na kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kupata muafaka.
Msekwa ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Mwinyi, alisema mvutano ya makundi hayo ulianza baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya Richmond na kueleza kuwa walichobaini ni wabunge hao kulinda nafasi zao majimboni kwa kuwa wabunge wamekuwa wakituhumiana kwa kila mmoja kudai kuwa kundi moja linataka kuliong'oa lingine jimboni.
Msekwa alisema hawana nia ya kukemea wala kumvua mwanachama wake yeyote uanachama na badala yake kazi waliyonayo ni kujenga umoja na mshikamano ndani ya chama.
Huku akinukuu kifungu cha Biblia na Quran, alionya kuwa kundi ambalo halitakubali kupatanishwa na lingine, 'litaandamwa'.
Tayari Kamati ya Mwinyi imeongezewa mwezi mmoja ili iweze kuyakutanisha makundi hayo mawili na Msekwa aliahidi kuwasilisha ripoti ya kazi hiyo kwenye kikao cha Kamati Kuu kitakachofanyika mwishoni mwa Machi, mwaka huu.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI