Kwanini Kagera isijiondoe kwenye koti la Tanzania?

ichumu lya

JF-Expert Member
Aug 11, 2016
2,605
2,729
Leo naandika kwa masikitiko makubwa sana baada ya Wakulima wa Vanilla Mkoani Kagera kulia kilio cha samaki na machozi yao kuondoshwa na maji.

Nimepitia maeneo tofauti tofauti mkoani Kagera nimekutana na wakulima wengi waliong'oa mikahawa baada ya anguko la bei na kupanda Vanilla leo vanilla iliyokuwa inanunuliwa kilo moja mbichi Tsh. 100, m000/ kipindi hicho kushuka kufikia Tsh.3, 000/ kwa kilo ni masikitiko na majonzi makubwa kuona bado kuna watu wanajiita viongozi sijui wanaongoza vitu gani wakati wakulima wanalia na kujikataa wenyewe.

Iko hivi Kagera ikiwa mwishoni mwa mikoa ambayo wananchi wana umasikini wa kutupwa nchini kwa mujibu wa tafiti mbalimbali lakini ni mkoa wenye wasomi wengi nchini wasio na faida nyumbani kwao.

Niliwahi kuhoji umuhimu wa kuwa na wasomi wenye kiwango cha mwisho uku ukuongiza kwa umasikini na watu wake kuwa kwenye top ya utapiamlo leo sitaji sifa za mkoa huu unaoongoza kwa vivutio vya uwekezaji Tanzania kwa kuwa katikati ya nchi nne ambazo ingetosha kuwa mkoa unaochangamka kiuchumi kuliko mikoa yote Tanzania.

Niliwahi kuhoji pia kwamba kwanini Kagera isijitenge kutoka Tanzania ili kuruhusu nchi yoyote kuja kuwekeza Kagera kuliko kukaa kwenye nchi isiyotambua/kuona umuhimu wa Kagera iliyozungukwa na Ziwa Victoria mito na mbuga ambazo kama zingetumika vizuri zingetosha kubadili uchumi wa Kagera na kuwa center ya kuichumi kwa nchi hizi nne ikiwamo na Tanzania?

Leo sitaki kabisa kuandika uduni wa miundombinu kama stendi na soko kuu vilivyochoka kama ajuza nasema sitaki kuandika namna Kagera ilivyotengwa kiuwekezaji kwamba ukifika Kyerwa utakutana na madini ya Kutengeneza bao (TIN) wananchi wamekalia utajiri kama wale watani zangu walivyokuwa wanachezea almasi bao.

Ukija mwambao wa Kemondo utakutana na mchanga wa vioo nyumba) bado mchanga huu hutumika kujengea nyumba lakini ukiona mashine za kutengeneza bati ni mashine ndogo isiyohitaji ata mita 100 na ardhi kujenga kiwanda alkadhalka na mashine za vioo.

Njoo kwa upande wa elimu Kagera ni mkoa usiokuwa na chuo kikuu hata kimoja, mkoa wa wasomi hapo simahanishi wasomi wajenge vyuo ila kwa nafasi zao uko walipo wana ushawishi mkubwa ata serikalini nako tumeangukia pua.

Tulikua tumebaki na kilimo lakini miaka zaidi ya 20 tulivamiwa na ugonjwa wa mnyauko ndizi (jeuri ya wanaKagera) zikanyauka lakini serikali haikuona sababu ya kuokoa zao hili badala yake walituacha tupambane na hali zetu apo napo Maprofessor wetu walitwambi mnyauko unatikana na uvivu unaopelekea mashamba kukanda utafiti niliupinga kwa hoja mpaka leo wako kimya.

Niliwauliza kama utafiti wenu umekomea hapo kwanini hamkujishighlisha kwenda Uganda ugonjwa ulikoanzia na leo walishausahau?

Majibu walioyafungia kwenye tafiti zao mliokuwa pale Bukoba coop hotel (Yaasira), nakumbuka nilivyowabana wasomi wetu leo tunalia na umaskini Kagera wakati umetengenezwa na serikali hii tangia vita ya Uganda.

Hapo nitapita kidogo serikali njoo mtuambie baada ya vita ya Uganda mlichukua hatua gani kuinua uchumi wa Kagera ulioathiliwa pakubwa na vita ile ya kitaifa? Nani alipewa fidia ya vita ile?

Nasema leo nina hasira na serikali hii yenye chuki na Kagera na mimi natangaza chuki na serikali hii maana ilinichukia mimi na wanaKagera tangia mwanzo ndiyo maana kila fursa ya uwekezaji ilielekezwa Mwanza sio Kagera.

Rejea miaka ya 1940 Kagera ilivyokuwa linganisha na Mwanza miaka ile Mwanza haikuona ndani kutokana na mchanganyo wa kibiashara kulikua na mwingiliano mkubwa kati ya Uganda na Kagera, Rwanda na Burundi leo tunachekwa na kutukanwa kwa makosa ya serikali.

Kwangu mimi naona mkwamo wa Kagera unatokana na muundo wa Katiba ya nchi yetu kama tungekuwa na serikali za majimbo tukaachana na wakuu wa Wilaya wa kuteuliwa na mtu asiye na historia na maeneo yetu mkuu wa jimbo tungemwajibisha lakini pia asingekuwa anasikiliza majungu kwakuwa angekuwa anatokana na sisi na akivurunda hawezi kuishi kwenye maeneo yetu haya ni maoni yangu nisipigwe pingu.

Sitaki kuzungumzia sheria ya ULANGUZI. ilivyovuruga juhudi za kiuchumi Kagera kuliko mkoa wowote nchini, nikiuliza NHC waliwahi kujenga nyumba ipi katikati ya mji nje ya walizonyang'anya wazee wetu? Msiniulize mengi lengo nikutaka vijana wanaojinasbu kulinda seriki hii wajue wanamkingia kifua adui.

Mimi Katikabakama nalazimika kukaa na kuililia Kagera na kizazi chetu sisi ni yatima kweli kweli mkoa unaoongoza kwa wasomi huku unaongoza kwa umaskini na utapia mlo ardhi ya Kagera imesubiri kupokea miili ya wasomi Madoktor, Maproffesor na wasomi wa viwango tofauti tofauti walioshindwa kutumia elimu kama fursa ya kiuchumi Kagera.

Mtu mmoja miaka ya Karibuni aliwahi kuimba namimi nakubaliana naye kwamba "omukyemba ky'omugaiga embaga yoona eryoomw' omwomworo nalila n'aboruganda bonka" Acha tulie na wanaukoo Kagera ibaki sehemu ya kuzika wasomi wetu wanaoletwa kwenye majeneza ya mamilioni yanayoliwa na wadudu pindi wakioza.

Leo sitoi ushauri kwa serikali maana miaka yote nashauri lakini sikio la kufa haliwezi kusikia dawa. Kwa upande wa Wakulima wote kuanzia Kahawa, Vanilla, na mazao yote ya kibiashara kila mtu ajitafakali siraha ya kuiadhibu serikali hii kila mmoja anayo kichwa

.@Katikabakama-2023
 
Hiyo sio Zanzibar, huo ni mkoa ndani ya Tanganyika/ Tanzania, huwezi kumega kipande cha nchi utapigika uchakae kama si kufa kabisa. Tumewachoka wachochezi, mara kusini ijitenge, mara kilimanjaro ijitenge, mara kagera ijitenga, enhe wakishajitenga tanzania ibakiwe na nini? Mna mawazo ya kiuasi hamtakubaliwa
 
Andiko lako ni zuri sana! Ila najiuliza kwa nini unalialia na kuona kila fursa inapelekwa Mwanza! Kwa maonj yangu serkali ndo adui yenu!

Wakija watu wa Mwanza hapa hawatakuelewa Mwanza umefika hapo kwa kuchapa kazi na kukaribisha wageni bila kuwabagua na mchanganyiko huo wa wenyeji na wageni ndo unaifanya Mwanza kuwa hapo lakini ninyi hamko hivo wageni mnawabaugua sana!
 
Andiko lako ni zuri sana! Ila najiuliza kwa nini unalialia na kuona kila fursa inapelekwa Mwanza! Kwa maonj yangu serkali ndo adui yenu...
Muda wangu unabana lakini ukipitia mwaka 1945 nyuma Kagera ilikuwa mbali ya Mwanza sisi tumehujumiwa alichofanya Nyerere ni kuhakikisha Kagera haipati viwanda na vyuo vikuu mpaka leo wembe ni ule kuhakikisha Kagera inakuwa ya mwisho. Swala la ukalimu nakuachia wewe maana aliyeanzisha majungu ayo ni uyo uyo Nyerere ili kutudhohofisha kifkra.
 
Jamani mbona nasikia vanila bei yake milioni moja
Uongo mtupu uongozi wa mkoa wamlikubaliana na wanunuzi bei ya Tsh.15, 000/kwa kilo mbichi lakini wanunuzi walewale wakadili na uongozi wa mkoa baada ya wakulima kuondoka walipe Tsh.3, 000/ kwa kilo mbichi. Kwaiyo kuna pesa wanachukua mkoa na nyingine zinabaki kwa mnunuzi mkulia anaambuli elfu tatu tu.
 
VALILLA kavu iyo usiseme bei ni Tsh.300, 000/ kwa kilo lakini bado hakuna wanunuzi kabisa.
IMG_20230718_194649_397.jpg
 
Uongo mtupu uongozi wa mkoa wamlikubaliana na wanunuzi bei ya Tsh.15, 000/kwa kilo mbichi lakini wanunuzi walewale wakadili na uongozi wa mkoa baada ya wakulima kuondoka walipe Tsh.3, 000/ kwa kilo mbichi. Kwaiyo kuna pesa wanachukua mkoa na nyingine zinabaki kwa mnunuzi mkulia anaambuli elfu tatu tu.
Dawa nyie acheni kulima hiyo vanilla

Ova
 
Muda wangu unabana lakini ukipitia mwaka 1945 nyuma Kagera ilikuwa mbali ya Mwanza sisi tumehujumiwa alichofanya Nyerere ni kuhakikisha Kagera haipati viwanda na vyuo vikuu mpaka leo wembe ni ule kuhakikisha Kagera inakuwa ya mwisho. Swala la ukalimu nakuachia wewe maana aliyeanzisha majungu ayo ni uyo uyo Nyerere ili kutudhohofisha kifkra.
Mwanza pia inabebwa na geographical position na migodi kwa hiyo haiwezi kulingana na Kagera kwa ukuaji wake wa kiuchumi pia tamaduni ya wenyeji kutokuwa na fitina nyingi kwa wageni!
Kingine jamii ya kanda ya Ziwa upande wa Mwanza,Mara,Shinyanga na Geita ni wachapakai sana! Ndio maana hata kwenye industry ya mining vijana wa mikoa hiyo wamejaa ila vijana wa Kagera wachache sana!
 
Leo naandika kwa masikitiko makubwa sana baada ya Wakulima wa Vanilla Mkoani Kagera kulia kilio cha samaki na machozi yao kuondoshwa na maji.

Ni

.@Katikabakama-2023
Sasa huko si ndiyo kwenye PhD nyingi zaidi duniani?

Si wangelima vanilla kwengine na kahawa ibaki hapohapo?

Majanga mengine yakujitafutia.

Mimi siyo mkulima lakini nafahamu wakulima wenye maana, wanalima mazao ya haraka haraka ya kuwaingiza pesa kila siku, huku mazao ya kudumu yakibaki na kuya maintain hapo hapo yalivyo. Dah, kwanini wasilime mahindi kwa wingi, ni pesa za haraka haraka na haziufungi mtaji kwa muda mrefu.

Nshomile mbona wanatuangusha? Huyu anna tibaijuka kakaa analipigia debe kanisa kwenye dpw badala ya kuwaelekeza wakulima huko wafanye nini.

Hiyo shule alienda kusomea ujinga?

cc Mama Amon
 
Sasa huko si ndiyo kwenye PhD nyingi zaidi duniani?

Si wangelima vanilla kwengine na kahawa ibaki hapohapo?

Majanga mengine yakujitafutia.

Mimi siyo mkulima lakini nafahamu wakulima wenye maana, wanalima mazao ya haraka haraka ya kuwaingiza pesa kila siku, huku mazao ya kudumu yakibaki na kuya maintain hapo hapo yalivyo. Dah, kwanini wasilime mahindi kwa wingi, ni pesa za haraka haraka na haziufungi mtaji kwa muda mrefu.

Nshomile mbona wanatuangusha? Huyu anna tibaijuka kakaa analipigia debe kanisa kwenye dpw badala ya kuwaelekeza wakulima huko wafanye nini.

Hiyo shule alienda kusomea ujinga?

cc Mama Amon
Sijui niseme nini ila tatizo la Kagera ni serikali tangia ilivyotaifisha mali za wafanyabiashara na kubeba fedha za KCU walitukata miguu tusisonge mbele wanakagera waliogopa kuwekeza nyumbani kwa kuogopa hujuma nyingine kama nilivyoeleza juu
 
Mimi nakazia hapo kwenye nyumba za NHC zilizojaa mjini kati hapo Bukoba...kimsingi zinauchakaza mji wa Bukoba...

Kwa nini wasiziuze kama hawataki kuzivunja na kuzijenga upya? Kwan Bukoba ni mji mkongwe wa urithi wa Dunia...
Zile nyumba za NHC zilizonyanganywa wahindi warudishiwe au wauze kwa watu wemye uwezo...Bukoba inao kibao tu...inafanya mji wa Bukoba uonekane umechakaa..na sio Bukoba tu miji mingo tu kuanzia Dar kule posta...nyumba nyingi za NHC zinauchakaza mji wa Dar..same us to tabora, moshi, morogoro nk...

Huoni hii sehemu ambayo haina hizo nyumba chakavu inavyopendeza kwa majumba mapya mjini Bukoba!!...sasa imagine lile eneo kubwa lenye NHC lingekuwa na nyumba fupi fupi hiv nzr Bukoba si ingekuwa paris ndogo kabisa huku Bukoba cathedral ikiwa mnara wa Eiffel..
dfg.JPG
 
Hii nchi upumbavu mwingi...na vilaza...


Yaan mtu unamazao yako umelima mwenyew lakin ukivuna inakubidi uiuzie serikali kwa bei wanayoitaka wao...

Ukijitafutia masoko yako mwenyew nje ya nchi UNAHUJUMU UCHUMI

Baadae wanakuja na takwimu uchwara kagera hawana kipato sijui maskini nini kifanyike..
 
Sijui niseme nini ila tatizo la Kagera ni serikali tangia ilivyotaifisha mali za wafanyabiashara na kubeba fedha za KCU walitukata miguu tusisonge mbele wanakagera waliogopa kuwekeza nyumbani kwa kuogopa hujuma nyingine kama nilivyoeleza juu
Sitisheni kulima hizo vanilla

Huko,bora mkose wote

Ova
 
Mwanza pia inabebwa na geographical position na migodi kwa hiyo haiwezi kulingana na Kagera kwa ukuaji wake wa kiuchumi pia tamaduni ya wenyeji kutokuwa na fitina nyingi kwa wageni!
Kingine jamii ya kanda ya Ziwa upande wa Mwanza,Mara,Shinyanga na Geita ni wachapakai sana! Ndio maana hata kwenye industry ya mining vijana wa mikoa hiyo wamejaa ila vijana wa Kagera wachache sana!
Mkuu hizo mwanza na shinyanga nk...yaan usukumani kiujumla ni miji tu ndo kuna uafadhali wa maisha ( ingawa miji mingi ukiondoa mwanza ni slums tu maana zinajengwa ovyo ovyo bila standard maalumu ndo maana Kwa kanda ya ziwa baada ya mwanza mji wenye muonekano wa kimji ni Bukoba pamoja na kwamba Bukoba inakosa miundombinu kama stendi nzr na soko)

Huko vijijini kuna umaskini wa kutupwa...uchirikina na kuchoka na maisha kabisa...hii ni tofauti ni Vijiji vya wahaya huko Bukoba vijijini, misenyi nk...pamoja na kwamba sio extremely rich lakin wanavijiji wengi wana maisha standard...na wana huduma zote za kijamii...

Ndo maana mji wa Bukoba wala hauwezi kukua sana kwa sababu bado watu hawajapata sababu kubwa ya kuwakimbiza vijijini ndo maana hadi saa tatu usiku unapata daladala za kwenda vijijini huko....

Bukoba kuna waganda, wanyankole, watu wa mara hadi wachaga kibao tu wanafanya biashara vzr tu hio myth ya kubaguliwa na wwnyeji unakuja nayo kichwani...mtu hawezi kukuchukia bila sababu...yaan uje Bukoba na tabia zako za kuwaita wahaya wakoje sijui wahaya wako hiv...bro wahaya hawapendi dharau...
 
Hii nchi upumbavu mwingi...na vilaza...


Yaan mtu unamazao yako umelima mwenyew lakin ukivuna inakubidi uiuzie serikali kwa bei wanayoitaka wao...

Ukijitafutia masoko yako mwenyew nje ya nchi UNAHUJUMU UCHUMI

Baadae wanakuja na takwimu ucharwa kagera hawana kipato nini kifanyike..
Dawa ni kuacha kulima

Ova
 
Halooooo mimi wacha nikae kimya wasije wakasema nina chuki na wanakagera lakini miongoni mwa vitu vinavyowaangusha ni SIFA ZA KIJINGA.
 
Back
Top Bottom