Kwanini ikulu walitumia yahoo - mawazo yangu

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
KWA NINI IKULU WALIAMUA KUTUMIA YAHOO

Pamoja na kwamba nilikosoa uamuzi wa ikulu ya tanzania kutumia barua pepe ya yahoo kwa ajili ya kuwasiliana na wananchi , nimekaa tena na kufikia mara nyingi zaidi kuona ni kwanini wao waliamua kufanya hivyo , ikulu ni sehemu nyeti sana lazima iwe na wataalamu waliobobea kwenye mawasiliano yao hawawezi kukurupuka tu na maamuzi ,lazima watakuwa wamejadiliana na kuona kile wanachotaka kufanya kwa muda mfupi .

Kama mnakumbuka wiki moja kabla ya tangazo la ikulu kulikuwa kuna mambo yanaendelea kwenye ulingo wa siasa nchini haswa uchaguzi wa chadema , chadema walifanikiwa sana kuteka mitandao mbali mbali na majukwaa mbali mbali hata kwenye magazeti kutokana na uchaguzi huo , mambo ya zitto kutaka kupambana na mbowe na mengine mengi sana siwezi kutaja .

Mwishowe chadema waliamua sasa kuanzisha utaratibu wa kukusanya michango yao kupitia simu za mikono hii ni njia nzuri nawapongeza lakini wajue kwamba nchi yetu kwa sasa hakuna sheria za kudhibiti mambo mengi yanayohusu mitandao pia simu zinasajiliwa kwahiyo huko mbeleni inaweza kuwa mbaya sana kwa wanaharakati wao haswa kipindi cha uchaguzi .

Inawezekana kabisa kwamba chadema walifanikiwa kuteka anga ya tanzania kwa kiasi kikubwa kila mtu macho yalikuwa huko , ndio ikulu ikaja na mbinu hii , kama wao wanatumia mitandao na majukwaa mengine nasi tunakuja na hii kuwasiliana na wananchi moja kwa moja kuanzia live kwenye tv mpaka kwenye mitandao ya internet .

Pia kuna kitu kingine walipotumia yahoo labda walimaanisha kokote mtu alipo kama anaweza kutumia ( IM ) instant Messenger kama yahoo , trillian na msn wanaweza kuingiza anuani ile ya yahoo kwenye contact list yao wawe wanaweza kuchat moja kwa moja na raisi kwa wakati huo pamoja na siku nyingine kwa kutumia hiyo hiyo na ni kitu cha kweli ni watu wengi sana wanaweza kutumia hizi messenger kwa ajili ya mawasiliano ya hapo kwa hapo .

Lingine inawezekana walitumia yahoo kama tanganya toto kumbe barua zote zilizoingia yahoo zilikuwa zinapelekwa katika email nyingine yaani email forwading , hii inaweza kusaidia sana kuhifadhi maswali kwa ajili ya utafiti huko mbeleni na kujua wale wote waliouliza maswali hayo , kwahiyo inawezekana waliona jambo hilo mapema .

Kuna kitu kinaitwa spam , hizi anuani za yahoo , hotmail na gmail zinaweza kufilter spam vizuri na kwa umakini zaidi kuliko hizi zingine za kawaida kwa kuwa yalikuwa ni maswali ya moja kwa moja inawezekana mpinzani akaamua kutuma spams kwa wingi ili kuvuruga mambo ukiwa na hizi barua pepe za kawaida maofisini kwetu ni hatari sana .

Mwisho napenda kutoa wito kwa Ikulu kuweka namba ambazo kupiga ni bure ili kila mwananchi aweze kupiga anavyotaka , kuna wengine huko walipo hawana uwezo hata wa kununua vocha za simu kutokana na hali zao kukiwa na huduma za bure basi wengi zaidi watawasiliana na raisi pamoja na kuchangia mawazo yao .

Bila kusahau kuanzisha sehemu yao katika mtandao wa www.youtube.com kwa ajili ya kuweka video zote zinazomhusu raisi kwa ajili ya ummah wale wanaotaka kudownload na kutumia kwenye shuguli zingine , hata juzi ile wale waliombali wangeweza kumwona raisi kutumia youtube na kuuliza maswali .

Ingawa kumekuwa na makosa ya hapa na pale naamini sasa ikulu pamoja na wadau wengine watakaa vizuri wajipange kwa ajili ya kuamua kuja na aina nzuri zaidi ya mawasiliano isiyokuwa na usumbufu na iliyobeba uasilia wetu kabisa .

Haya ni mawazo yangu tu , Karibuni tuendee kujenga nchi www.wanabidii.net , www.naombakazi.com
 
KWA NINI IKULU WALIAMUA KUTUMIA YAHOO

Pamoja na kwamba nilikosoa uamuzi wa ikulu ya tanzania kutumia barua pepe ya yahoo kwa ajili ya kuwasiliana na wananchi , nimekaa tena na kufikia mara nyingi zaidi kuona ni kwanini wao waliamua kufanya hivyo , ikulu ni sehemu nyeti sana lazima iwe na wataalamu waliobobea kwenye mawasiliano yao hawawezi kukurupuka tu na maamuzi ,lazima watakuwa wamejadiliana na kuona kile wanachotaka kufanya kwa muda mfupi .

Kama mnakumbuka wiki moja kabla ya tangazo la ikulu kulikuwa kuna mambo yanaendelea kwenye ulingo wa siasa nchini haswa uchaguzi wa chadema , chadema walifanikiwa sana kuteka mitandao mbali mbali na majukwaa mbali mbali hata kwenye magazeti kutokana na uchaguzi huo , mambo ya zitto kutaka kupambana na mbowe na mengine mengi sana siwezi kutaja .

Mwishowe chadema waliamua sasa kuanzisha utaratibu wa kukusanya michango yao kupitia simu za mikono hii ni njia nzuri nawapongeza lakini wajue kwamba nchi yetu kwa sasa hakuna sheria za kudhibiti mambo mengi yanayohusu mitandao pia simu zinasajiliwa kwahiyo huko mbeleni inaweza kuwa mbaya sana kwa wanaharakati wao haswa kipindi cha uchaguzi .

Inawezekana kabisa kwamba chadema walifanikiwa kuteka anga ya tanzania kwa kiasi kikubwa kila mtu macho yalikuwa huko , ndio ikulu ikaja na mbinu hii , kama wao wanatumia mitandao na majukwaa mengine nasi tunakuja na hii kuwasiliana na wananchi moja kwa moja kuanzia live kwenye tv mpaka kwenye mitandao ya internet .

Pia kuna kitu kingine walipotumia yahoo labda walimaanisha kokote mtu alipo kama anaweza kutumia ( IM ) instant Messenger kama yahoo , trillian na msn wanaweza kuingiza anuani ile ya yahoo kwenye contact list yao wawe wanaweza kuchat moja kwa moja na raisi kwa wakati huo pamoja na siku nyingine kwa kutumia hiyo hiyo na ni kitu cha kweli ni watu wengi sana wanaweza kutumia hizi messenger kwa ajili ya mawasiliano ya hapo kwa hapo .

Lingine inawezekana walitumia yahoo kama tanganya toto kumbe barua zote zilizoingia yahoo zilikuwa zinapelekwa katika email nyingine yaani email forwading , hii inaweza kusaidia sana kuhifadhi maswali kwa ajili ya utafiti huko mbeleni na kujua wale wote waliouliza maswali hayo , kwahiyo inawezekana waliona jambo hilo mapema .

Kuna kitu kinaitwa spam , hizi anuani za yahoo , hotmail na gmail zinaweza kufilter spam vizuri na kwa umakini zaidi kuliko hizi zingine za kawaida kwa kuwa yalikuwa ni maswali ya moja kwa moja inawezekana mpinzani akaamua kutuma spams kwa wingi ili kuvuruga mambo ukiwa na hizi barua pepe za kawaida maofisini kwetu ni hatari sana .

Mwisho napenda kutoa wito kwa Ikulu kuweka namba ambazo kupiga ni bure ili kila mwananchi aweze kupiga anavyotaka , kuna wengine huko walipo hawana uwezo hata wa kununua vocha za simu kutokana na hali zao kukiwa na huduma za bure basi wengi zaidi watawasiliana na raisi pamoja na kuchangia mawazo yao .

Bila kusahau kuanzisha sehemu yao katika mtandao wa www.youtube.com kwa ajili ya kuweka video zote zinazomhusu raisi kwa ajili ya ummah wale wanaotaka kudownload na kutumia kwenye shuguli zingine , hata juzi ile wale waliombali wangeweza kumwona raisi kutumia youtube na kuuliza maswali .

Ingawa kumekuwa na makosa ya hapa na pale naamini sasa ikulu pamoja na wadau wengine watakaa vizuri wajipange kwa ajili ya kuamua kuja na aina nzuri zaidi ya mawasiliano isiyokuwa na usumbufu na iliyobeba uasilia wetu kabisa .


Haya ni mawazo yangu tu , Karibuni tuendee kujenga nchi www.wanabidii.net , www.naombakazi.com

Nayaunga mkono hayo niliyowekea wekundu. Hata hivyo email redirect siyo njia madhubuti ya kujikinga na spam au madudu mengine mtandaoni. Wala siyo njia mbadala ya kuwasiliana na wananchi. Wanafungu la kushughulikia mambo haya, hela hizo sijui zinatumika vipi... (kukwepakwepa maswali, au?)...
Naona watakuwa wamewasiliana nawe kwa karibu kuwapatia ushauri baada ya kuwa umeyasema yafuatayo:

RAISI WAJIBISHA WATENDAJI WAKO

Mheshimiwa Raisi Toka uingie madarakani kumekuwa na jitihada nyingi sana zinazofanywa na watendaji wako katika kuhakikisha unakuwa karibu zaidi na wananchi wako kwa njia rahisi zaidi za mawasiliano .

Toka umeingia madarakani watendaji wako wamekuwa wakitumia zaidi mitandao ya kimataifa yaani INTERNET kwa ajili ya kukuweka wewe karibu zaidi na wananchi wako , pamoja na jitihada hizi za kupongezwa kuna mengine yamefanyika inabidi sasa uwe macho na hawa watu .

Miaka miwili iliyopita mlianzisha tovuti maalumu kwa ajili ya wananchi kutoa maoni yao , kipindi hicho watu mbali mbali walilalamika kuhusu gharama za tovuti hiyo hakuna aliyejali kujali kwa maana ya kutoa ufafanuzi kwa wananchi hata hivyo tovuti hii mpaka leo iko kimya .

Baadaye mlianzisha tovuti zingine ambazo zilikuwa zinafanana na hizo za kutoa maoni , naona kuna moja bado iko lakini imeshindwa kupambana katika soko ili kuweza kutambulika itumike kiurahisi na watu wengi zaidi maana yake iko kimya .

Halafu likaja hili la ikulu kuanzisha blogu yake ya mawasiliano ambayo ilikuwa imesajiliwa katika Google , si unakumbuka raisi ulienda kutembelea makao makuu ya google mwaka huu na wasaidizi wako ? wale ndio mlisajili blogu kwao , pamoja na kusajili imeandikwa mara chache sana mtu akitaka habari zozote inabidi atembelee blogu na mitandao mengine na sio blogu hiyo .

Mheshimiwa hakukuwa na sababu za msururu wa tovuti zote hizi pamoja na blogu hizi zote kwa sababu raisi aliyekutangulia alikuwa na tovuti maalumu ya ikulu na nyingine iliyokuwa inaitwa statehouse ilibidi kuendeleza tovuti hizi na kuweka hivyo vyote .
Kumbuka Ikulu sio mali yako wewe wala ya mwingine wowote yule , kiongozi aliyetoka alitambua hilo sio mali yake ndio maana akaacha tovuti hizo zenye majina ya ikulu , ili wewe ukiingia mtumie hizo na muziendeleze tofauti yake mmeziacha zote na kuanzisha zetu wenyewe hii sio tabia nzuri mheshimiwa .

Baada ya yote hayo leo tena nimesoma Barua toka ikulu kwa vyombo vya habari inayohusu mkutano wako kesho moja ya kitu kilichonichekesha na kunihuzunisha ni hili la kuweka email ya yahoo ambayo ni swalikwarais@yahoo.com , inahuzunisha sana kwa sababu watendaji wako wameshindwa kubuni njia nzuri zaidi na bora kwa ajili ya wananchi kutoa maoni yao kwenye karne hii .

Anuani ya barua pepe hiyo imesajiliwa leo na ninaamini wakati wanasajili hawakusoma maelezo ya ziada kabla ya kuendelea na usajili hivi ikatokea sasa mtu akafanikiwa kuingilia anuani hiyo akachukua maswali hayo pamoja na mawasiliano mengine mtafanya nini ? halafu akaamua kuifuta mtafanya nini ? na suala la usalama wako hapo umeliwekaje ? .

Mheshimiwa kila unapotaka kusoma Ujumbe kwenye Anuani hiyo kama kweli utakuwa unaisoma , kumbukumbu zinabaki yahoo kwenyewe , kila unapojaribu kujibu maswali kutumia anuani hiyo inapoenda itajulisha ilijibiwa akiwa wapi kwahiyo uhalifu unaweza kuanza hapo na kuendelea sipendi kuona hili likiendelea

Kwa maslahi ya usalama Wako wewe mwenyewe raisi , wasaidizi wako na wengine ambao watakuwa kwa njia moja au nyingine wanatumia anuani hiyo nawaomba kabisa muache kutumia anuani hiyo andaeni njia nzuri za mawasiliano kati ya raisi na wananchi wake na hivi vyote vinaweza kufanyika kwenye tovuti ya ikulu ikitengenezwa vizuri tu .

Kingine mnatakiwa mfungue channel zetu kwenye tovuti zingine kama youtube hii ni kwa ajili ya video muwe mnaweka video zenu na vingine humo , Raisi wa sasa wa Marekani alisaidiwa sana na youtube katika kufanikisha mambo yake mengi .

Mheshimiwa raisi ulizindua Mkonga wa mawasiliano siku chache tu zilizopita kwa sasa mtandao uko haraka sana hakuna matatizo kama zamani naamini wasaidizi wako wakitumia advantage hii utafika mbali hata kwenye kampeni zako za mwaka 2010 utatesa sana .

Mwisho ni kukuomba wewe na wasaidizi wako muwe karibu sana na wataalamu wenu wa ICT katika utendaji wa kazi inawezekana hata hii ANUANI iliyotengenezwa leo pamoja na hizo BLOGU zimetengenezwa bila ridhaa ya wataalamu wenu wa ICT nah ii ni mbaya sana , hawa watu wanasomeshwa kwa pesa nyingi sana lazima tuone tofauti yao katika jamii .

Na...hapa ambapo uliwashushua kikwelikweli:

Lakini Hao TBC pamoja na Ikulu wawe kama wameenda shule jamani umeona hiyo email hapo chini swalikwar...@yahoo.com hii ni freeemail toka yahoo na tena imesajiliwa leo leo dakika chache zilizopita tu wanataka wananchi watume email zao huko , waliposajili hii email walisoma terms zote za yahoo?

Kwamba kila unapofungua au kuwasiliana na mtu kuna log huwa wanazihifadhi? Kwa kazi zao wao wenyewe yahoo? hapa kwetu tunatakiwa kumuuliza maswali raisi kwa kutumia email hiyo hiyo kwa kweli hili halikubaliki

RAISI WAJIBISHA WOTE WALIOTENGENEZA EMAIL HII , WEWE NI RAISI UNATAKIWA ZAIDI YA
HII UNATAKIWA KITU KINACHOKUTAMBULISHA SIO HII AIBU SANA , HIZO BAJETI KUBWA
MNAZOPITISHA HUWA MNATUMIA KWENYE NINI ? HIZO SEMINA NA WATU WANAENDA
KUFUNDISHWA NGAMBO MASUALA YA ICT NDIO LEO WANAKUJA NA HIKI KITU ?

HATUTAKI RAISI WETU AZARAULIWE KIASI HICHI
 
The Great SHY nadhani with "both the contradicting posts" haukutuma email kuuliza swali kwa Rais?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom