Kwanini Hayati Magufuli hapoi?

Kwa ndani kabisa, haya mambo ya Ukatoliki na Uislam tunashindwa kuwa na common say towards viongozi wetu. Wametugawa nasi tukawezekana. #UdiniUkristoVsUislam. Viongozi wote have got both strengths and weaknesses
Waislam ni ombaomba sana
 
Ukiwatoa Nyerere, Mkapa na Magufuli waliobaki walikuwa wanafilisi nchi. Sasa wakumbukwe kwa lipi?
Mkapa pia muondoe hapo naye alikuwa mjasiriamali ! Na alibinafsisha mashirika mengi bila ya sababu yeyote ya maana. !!
 
Hata Uganda wanamsema sana Idd Amin

Makanisani kila siku wanamsema shetani....
 
makufuli alifanya mambo makubwa kuliko awamu zote , makufuli alitengeneza nchi kwa tabia na kuondoa ufisadi na wizi wa aina tofauti katika ngazi zote makufuli aliondoa kujifanya mimi mtoto wa fulani nitakuweka ndani, makufuli aliwatetea sana watu wa hali ya chini . makufuli alikuwa hafichi kitu mkweli na muazi hata kama weww ni rafiki yake ukizinguwa anakuzinguwa. makufuli alikuwa anaweza kufanya mradi wowote bila kujali mkopo,kwa hiyo katika hayo niliyoyaeleza kuna watu walibanwa kwa ufisadi vyeti biashara haramu dawa za kulevya biashara za magendo na hasa bandarini hao ndio wanaokuja kila siku kumsema vibaya. na kuna wale wanatafuta teuzi ni lazima amseme makufuli na kuna wale wataka sifa kwenye media anapoitwa kuzungumzia jambo lazima amtaje makufuli ili aonekane nae kaongea, lakini kumbuka marehemu anashindana na watu walio hai bado marehemu makufuli anakuwa mshindi,
 
Umesahau alivyokuwa na bahati ya kuokota vichwa vya treni bandarini. Havikuwa na mwenyewe japo vilikuwa na nembo ya TRL
 
Magufuli ameacha nini? Ameacha wizi wa Tsh 2.4 Trilion, chuki dhidi ya upinzani, ubaguzi wa maendeleo kwa kupendelea Chato, umalaya kwa akina Jokate na Kairuki, matusi kwenye majukwaa, kuropoka, ubishi wa Corona mpaka imemuua, uuaji wa akina Ben Saanane na Azory Gwanda, utekaji wa akina MoDewji, maonezi kwa akina Eric Kabendera na Tito Magoti na dharau kwa wanawake tu.

Atakumbukwa kwa UDIKTETA, kukandamiza Demokrasia, Wizi wa uchaguzi Serikali za Mitaa 2019, wizi wa kura uchaguzi Mkuu 2020, kuvunja Katiba, kudhibiti Bunge na kuitishia Mahakama. Vilevile kuminya uhuru wa kujieleza na kuitishia vyombo vya habari.

Nani atanikamata leo nikisema Magufuli alikuwa muuaji? Hakuna kwa vile Rais SSH anakubali kukosolewa kwa misingi ya Sheria. Ila wapumbavu kama wewe wanafiriaalikuwa mtu wa maana
 
Hapoi kwa sababu kuna Magufuli Bus Terminal, Magufuli Hostels, Magufuli Secondary School, Magufuli Bridge, Magufuli Town-Dodoma, Magufuli Legacy, na Magufuli policy
 

ukiona mtu anakuletea sijui azori aliuwawa ujue chaggadema hawana ajenda
 
Hawa ndiyo Watanzania wenyewe wanaofanya tuoekane wajinga. Wajinga wengi kwenye makundi makubwa wanaweza kumchagua mjinga mwenzao kuwa Rais
 
Kuna siku kanisani hawajamtaja shetani
 
Magufuli was controversial figure.
1.Alitangaza vita vya vyeti fake huku akilinda baadhi ya watumishi wakuu na idara nyingine wasiguswe.
2.Alihubiri kuangamiza rushwa lakini akiwaruhusu traffic police kupewa pesa za hongo alioiita pesa ya kupiga brush viatu.
3.Alianzisha elimu bure matokeo yake darasa la kwanza wanafunzi kwenye chumba kimmoja walijaa zaidi ya 200.
Hata pale vilipopatikana au kujenga vyumba vya madarasa hakuajiri walimu wapya kuendana na wingi wa madarasa.
4.Aliomba mkopo/msaada wa Elimu wenye thamani ya 400 million dollars uliokuwa na sharti ya kuruhusu waliozaa kurudi shuleni kuendelea na masomo,lakini ulipokuwa tiyari akauruka kimanga.

5.Akiwa waziri wa miundo mbinu wakati wa Jk,aliufagilia mradi wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo,lakini alipoukwaa uraisi akaukana kabisa.
6.Alitumia pesa nyingi kujenga uzio wa kuzunguka eneo zima la madini ya Tanzanite huko Merelani ili kudhibiti utoroshaji wa madini hayo,kumbe wajanja wakachimba mahandaki kama ya wa Palestine ukanda wa Gaza,wakaendelea kutorosha madini hayo kwa njia za chini kwa chini.

7.Alihamia Dodoma kwa kuhamisha serikali yake na Taasisi mbali mbali tokea Dar kwa kile alichodai makao makuu ya nchi,lakini kwa nyakati mbali mbali akaifanya Chato kufanya shughuli mbali mbali za kitaifa hata kuliko Dodoma.
8.Hakupenda kukosolewa lakini yeye akiwakosoa waliomtangulia na viongozi wengine kwenye serikali yake.
9.Alikataa safari za kwenda nchi za nje za mbali akidai anapunguza matumizi kumbe alikuwa na kitufe Pacemaker chenye kurekebisha mapigo ya moyo ambacho kinaweza kuadhirika sana kwasababu ya mitambo ya electronic ya ndege.
10.Tuliambiwa tunadai ushuru wa makanikia sh 360 trillion tukaambuli sh 700 billion hata trillioni mmoja haijafika.
Kibaya zaidi Barrick waliitoa pesa hiyo kwa awamu wakisema ni msaada wa maendeleo wala si kodi ya makanikia hawadaiwi.
11.Alituhamasisha ataleta maendeleo kwa wananchi wote, kuwa hajali mwananchi anatokea chama gani lakini wakati mwingine akidai kuwabomolea nyumba ambao hawakumchagua.
12.Takwimu za viwanda alivyodai 8000 vimejengwa wakati wa utawala wake haikuwa sahihi.
 
Hata mmpambe vipi hapambiki.
 
Uko sawa mtu wa Mungu.
 
Kama wizi uliondoka awamu yake mbona alikufa rais tajiri kuliko wote? Makonda aliyekuwa jicho lake utajiri mwingi kaupata kipindi cha jiwe.Bahati mbaya akaiba mpaka uchaguzi mkuu pamoja na ule wa Serikali za mitaa matokeo yake sasa hivi nchi imejaa wala rushwa,wezi wa wazi,matapeli na mazuzu.
 
Asiwe, apambwe, atukuzwe na aabudiwe hakuna madhara hasi wala chanya. Waliobaki hai wanafanya maamuzi ya nchi. Hao ndo wana madhara hasi au chanya.
 
Ukiwatoa Nyerere, Mkapa na Magufuli waliobaki walikuwa wanafilisi nchi. Sasa wakumbukwe kwa lipi?
Mkapa huyu huyu aliyeuza viwanda na mashirika ya umma kwa bei ya kutupa katika sera yake ya ubinafsishaji au Ken Mkapa aliyekuwa mchezaji wa Yanga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…