Kwanini hatuwezi kupata Channel zingine DStv kama Startimes..... kwanini niwe na Decoder mbili?

Kwanini hatuwezi kupata Channel zingine DStv kama Startimes..... kwanini niwe na Decoder mbili?

dawa ni kuwabana hawa dstv,wenze2 kenya mpaka jana wana local chanels tano kweny package za dstv,kwa nin isiwe sisi? Viongozi wetu ni majanga sana

Mkuu dstv walisema wataweka 5 local channels ila utatakiwa kulipia kitu kama elfu 6 per month on top of your package. Sijawafuatilia tangu mwaka uanze but walikuwa kwny process. Ulizia ofisini kwao. So usinunue decoder nyingine.

Ajabu hawajaitangaza hii, nafikiri kwa makusudi tu!
 
Mkuu naipenda jf ninayo moja napata za dstv,bongo,kanal,mytv,nk jf ni mambo yote

Usishangae pale utakapoambiwa ukitaka kuingia JF lazima uwe na king'amuzi!! ......chazeiya magamba weye.
 
hawajamaa waliwaambia watanzania wajiandae kumbe wao ndio hawaja jiandaa muda wote waliokuwa wanatanza nivizuri wangetujuza watanzania tujiandae kununnua vingamuzi zaidi ya vitatu ilituweze kupata local channel leo namsikia naibu waziri makamba baada ya kuzima mitambo anazungumzia negotioation zinaendelea kuongeza channel kwenye baadhi ya vingamuzi kwa nini hilo lisingefanyika kabla.
Mkuu mipango hapa kwetu ni kama azabu,watu wengi hatuko teyari kupanga mipango ya baadaye!
 
Jamani kuingiza channel kwenye king'amuzi tofauti kisicho cha zuku, star times na ting ni makubaliano ya mwenye channel na mmiliki wa king'amuzi. kwa hiyo kama mwenye channel yake anataka ionekane dstv waingie mkataba hata wakiweza waingize zooote za tanzania ni wenye channel zao tu kuamua kuingia mkataba. Serikali inahamishia matangazo kwenye digital kupitia ving'amuzi vitatu vya kwenye mkataba na tcra (star times, zuku, ting). Mnaweza kunitajia nchi moja duniani ambayo ina decodar yenye channel zote za nchi hiyo. na hiyo decoder inaitwaje? acheni ubwege!!!!!!!!!!!!
 
Hapa lazima harmonisation ifanyike haraka iwezekanavyo!

Mkuu Tukutuku, suala hili TCRA walipaswa kuli-address toka mwanzo lakini hawana muda wa kufanya mambo muhimu - a lion's share ya muda wao ni kuitisha mikutano/kongamano kukusanya wabunge kwenda kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa mfumo wa digitali as if magazeti na TV hazitoshi kuelimisha watu. Kuhusu DSTv naona wanaonyesha zaidi local channel za Kenya na Uganda labda kampuni za hapa Tanzania wamewakatalia kurusha channels zao - si unajua tena!

Na hili la kuruhusu Multiplex Providers watatu kufanya kazi zile zile, zitawachanganya watu sana maana kila Provider atavutia kwake na hatuna uhakika kama watakubaliana kuharmonise local channels ili raia wasilazimike kununua vingamzi vitatu. Wasipo jirekebisha wakaishia kupigana vita vya kibiashara, naona Raia wenye uwezo kidogo watahamia kwenye madishi.
 
Jamani kuingiza channel kwenye king'amuzi tofauti kisicho cha zuku, star times na ting ni makubaliano ya mwenye channel na mmiliki wa king'amuzi. kwa hiyo kama mwenye channel yake anataka ionekane dstv waingie mkataba hata wakiweza waingize zooote za tanzania ni wenye channel zao tu kuamua kuingia mkataba. Serikali inahamishia matangazo kwenye digital kupitia ving'amuzi vitatu vya kwenye mkataba na tcra (star times, zuku, ting). Mnaweza kunitajia nchi moja duniani ambayo ina decodar yenye channel zote za nchi hiyo. na hiyo decoder inaitwaje? acheni ubwege!!!!!!!!!!!!
Mkuu Muya, ubwege hauko kwa wananchi bali TCRA wanaoshindwa kusimamia mambo yenye maslahi kwa wananchi. TCRA inakaribisha hatari ya kila kituo kuja na decoder yake, maana wameshindwa kusimamia ubora na uhimara wa signal kupitia kwa kampuni walizozipa leseni. Matokeo yake ni kuwa both wananchi na wenye vituo vya TV wanalalamika.

Jambo lingine linalokera ni kwa TCRA kuridhika na cheap propaganda ya DSTV kuwa wanatoa huduma yao kwa misingi ya burudani na hivyo wasiingiliwe. Swali ni kuwa kwani TBC1, na channels za Kenya na Uganda zinazoonekana zote ni 'entertainment' channels? Kwanini wakubali kuumiza Watanzania kibao ambao tayari wana huduma ya DSTV?

Nadhani ubwege uko kwa TCRA na sio vinginevyo!
 
Back
Top Bottom