Samcezar
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 13,096
- 22,818
Habari wanajamvi.
Leo napenda tupeane ushauri sisi wenye nchi. Kwa kipindi kirefu kumekuwa na uwekezaji wa miundombinu ya barabara kuu na za vitongoji ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami.
Ila kwa bahati mbaya rami hii huwa haidumu hata kidogo na huwa tunakumbwa na adha ya mashimo (potholes) karibuni kila kona ambayo hukua na kugeuka kuwa mashimo makubwa sana hatarishi kwa usalama wa raia na vyombo vyao.
Nimejiuliza kwann mataifa makubwa kama Marekani, barabara zao kubwa tena unakuta za line ya nne kwa nne au sita kwa sita zimejengwa kwa kiwango cha ZEGE.
Na unaambiwa hizi barabara zina life span ya minimum miaka 20 hadi 40 kinyume na za lami ambazo huwa ni 15 years maximum kabla hazijaanza kuwekwa viraka.
Kwanini serikali katika hizi barabara za vitongoji kusiwekwe tu kiwango cha zege tusahau hii changamoto ya mashimo ambayo sasa imekuwa ni kero maana kushughulikiwa ni hadi miaka ya kukaribia uchaguzi ndipo utaona vifusi vinawekwa.
Kwanini hatuwekezi katika barabara za zege?
Kwa wale ambao hamjawahi jua kuna barabara za zege nendeni mkatazame barabara za basi za mwendokasi mtajionea barabara ya zege ina muonekano gani pamoja na uimara wake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo napenda tupeane ushauri sisi wenye nchi. Kwa kipindi kirefu kumekuwa na uwekezaji wa miundombinu ya barabara kuu na za vitongoji ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami.
Ila kwa bahati mbaya rami hii huwa haidumu hata kidogo na huwa tunakumbwa na adha ya mashimo (potholes) karibuni kila kona ambayo hukua na kugeuka kuwa mashimo makubwa sana hatarishi kwa usalama wa raia na vyombo vyao.
Nimejiuliza kwann mataifa makubwa kama Marekani, barabara zao kubwa tena unakuta za line ya nne kwa nne au sita kwa sita zimejengwa kwa kiwango cha ZEGE.
Na unaambiwa hizi barabara zina life span ya minimum miaka 20 hadi 40 kinyume na za lami ambazo huwa ni 15 years maximum kabla hazijaanza kuwekwa viraka.
Kwanini serikali katika hizi barabara za vitongoji kusiwekwe tu kiwango cha zege tusahau hii changamoto ya mashimo ambayo sasa imekuwa ni kero maana kushughulikiwa ni hadi miaka ya kukaribia uchaguzi ndipo utaona vifusi vinawekwa.
Kwanini hatuwekezi katika barabara za zege?
Kwa wale ambao hamjawahi jua kuna barabara za zege nendeni mkatazame barabara za basi za mwendokasi mtajionea barabara ya zege ina muonekano gani pamoja na uimara wake.
Sent using Jamii Forums mobile app