Kwanini Halima Mdee na wenzake licha ya kutokuwa wanachama wa Chama cha Siasa bado ni Wabunge?

MKWEAMINAZI

JF-Expert Member
May 28, 2023
930
1,299
Nimepitia katiba ya nchi yetu Katiba ambayo hata Rais anapochaguliwa lazima aiape kwanza ndio awe Rais na pia aseme atailinda ataihifadhi na kuiheshimu.

Pia Katiba hiyo hiyo imeeleza Spika anavyopatikana na kuala kuwa atailinda kuitetea na kuihifadhi. Katiba hiyo hiyo imeeleza jinsi Wabunge watakavyopatikana na sifa zao na pia imeeleza jinsi ubunge wao utakavyokoma ikiwa ni pamoja na kufukuzwa uanachama na chama kilichomdhamini.

Katiba hiyo hiyo nimeisoma mwanzo mpaka mwisho sijaona kifungu chochote kinachomlinda mbunge aliyefukuzwa uanachama kuendelea kuwa mbunge kama ilivyo kwa Halima Mdee na wenzake 18.

Suala la kupinga kufukuzwa uanachama ni suala binafsi la aliyefukuzwa na hulifanya mara baada ya kuvuliwa ubunge kama katiba inavyoelekeza lakini imekuwa kinyume kwa suala la wabunge 19 waliofukuzwa uanachama wao serikali na bunge vimeamua kwa makusudi kukiuka katiba kwa kutowavua ubunge kama ilivyowahi kufanya kwa wabunge wa CUF na CCM mara tu baada ya kupata barua ya kufukuzwa uanachama wao kutoka kwenye vyama vyao na bunge halikusubiri mahakama itoe maelekezo, lakini kwa hawa 19 bunge na serikali wamewaruhusu kuendelea kuwa wabunge bila kuwa wanachama wa chama cha siasa kinyume na katiba na kuwataka wapinge kufukuzwa kwao wakiwa Wabunge.

Swali gumu: Je, kwanini Halima Mdee na wenzake 18 bado ni wabunge ili hali sio wanachama wa chama cha siasa kwa mujibu wa katiba ya nchi?

1652327090551.jpg
1652427482224.jpg
 
Hao Ni Wana Ccm Ni Mpango Uliopangwa
Ikumbukwe Ccm Ilipora Uchaguzi Ikasahau Kuwa Bila Upinzani Bunge Litakosa Uhalari Ikabidi Watumie Kuwaingiza Halima Na Wenzake
 
Nimepitia KATIBA ya NCHI yetu KATIBA ambayo hata RAIS wa Anapochaguliwa LAZIMA aiape kwanza ndio awe RAIS na pia Aseme ATAILINDA ATAIHIFADHI na KUIHESHIMU.
Pia KATIBA hiyo hiyo imeeleza SPIKA anavyopatikana na Kuala kuwa ATAILINDA KUITETEA NA KUIHIFADHI .KATIBA hiyo hiyo imeeleza Jinsi WABUNGE watakavyopatikana na SIFA ZAO na pia imeeleza jinsi UBUNGE wao UTAKAVYOKOMA ikiwa ni pamoja na KUFUKUZWA UANACHAMA na CHAMA kilichomdhamini.KATIBA hiyo hiyo nimeisoma mwanzo mpaka Mwisho SIJAONA KIFUNGU chochote kinachomlinda MBUNGE aliyeFUKUZWA UANACHAMA kuendelea kuwa MBUNGE kama ilivyo kwa HALIMA MDEE na WENZAKE 18.
Suala la Kupinga KUFUKUZWA UANACHAMA ni suala BINAFSI la ALIYEFUKUZWA na hulifanya mara baada ya KUVULIWA UBUNGE kama KATIBA INAVYOELEKEZA lakini imekuwa Kinyume kwa SUALA la WABUNGE 19 waliofukuzwa Uanachama wao SERIKALI na BUNGE vimeamua kwa MAKUSUDI KUKIUKA KATIBA kwa KUTOWAVUA UBUNGE kama ilivyowahi kufanya kwa WABUNGE wa CUF na CCM Mara tu baada ya KUPATA BARUA ya KUFUKUZWA UANACHAMA wao kutoka kwenye Vyama vyao na BUNGE halikusubiri MAHAKAMA itoe MAELEKEZO lakini kwa hawa 19 BUNGE na SERIKALI wamewaruhusu kuendelea kuwa WABUNGE Bila kuwa WANACHAMA wa Chama cha SIASA Kinyume na KATIBA na kuwataka Wapinge KUFUKUZWA kwao WAKIWA WABUNGE.
SWALI GUMU:
JE KWANINI Halima Mdee na Wenzake 18 Bado ni WABUNGE ili hali SIO WANACHAMA wa CHAMA cha SIASA kwa Mujibu wa KATIBA ya NCHI?
View attachment 2644213View attachment 2644218
muulize mbiwe nani alipeleka barua ya kuwatambulisha kwa spika
 
Wajinga ni wengi Nchi hii haina maelezo yaani mtu anakula Kodi yako unasema Mungu anawapa RIZIKI daah
Mlaji namba moja yupo na inawezekana hukumchagua,SASA aliekataliwa na wananchi atateuaje waliobora!!?

Mungu yupo hata zama za uovu mkuu,ukatae ukubali nakuambia!!
 
Katiba hiyo hiyo nimeisoma mwanzo mpaka mwisho sijaona kifungu chochote kinachomlinda mbunge aliyefukuzwa uanachama kuendelea kuwa mbunge kama ilivyo kwa Halima Mdee na wenzake 18.
Katiba haisomwi tuu yenyewe kama katiba, bali inasomwa na sheria, taratibu na kanuni,
jee umesoma na sheria, taratibu na kanuni?.
Suala la kupinga kufukuzwa uanachama ni suala binafsi la aliyefukuzwa na hulifanya mara baada ya kuvuliwa ubunge kama katiba inavyoelekeza
Kwa mujibu wa katiba hiyo hiyo inaeleza uamuzi wowote ambao ni kinyume cha katiba, sheria, taratibu na kanuni, ni void ab initio, maana yake hawakufukuzwa kikatiba, kisheria, kitaratibu na kikanuni!. Kwa mujibu wa Bunge, wale bado hawajafukuzwa, ni wabunge halali wa Bunge la JMT. Kule kufukuzana kwa a kangaroo court, hakutambuliki na mamlaka zozote!.
Kwa vile wabunge hawa ambao ni wanawake wa shoka, wameupinga ukangaroo wa Chadema, mahakamani, Bunge linausubiri uamuzi wa Mahakama, lilifanya hivyo kwa Mhe. Hamad Rashidi Mohamed alivyofukuzwa kikangaroo na CUF, na limefanya hivyo kwa Zitto Kabwe alipofukuzwa kikangaroo na Chadema.
lakini imekuwa kinyume kwa suala la wabunge 19 waliofukuzwa uanachama wao serikali na bunge vimeamua kwa makusudi kukiuka katiba kwa kutowavua ubunge kama ilivyowahi kufanya kwa wabunge wa CUF na CCM mara tu baada ya kupata barua ya kufukuzwa uanachama wao kutoka kwenye vyama vyao.
Taarifa ya kufukuzwa kwao, ilitangulia kufika Bungeni kabla ya taarifa ya kupinga kufukuzwa.
na bunge halikusubiri mahakama itoe maelekezo, lakini kwa hawa 19 bunge na serikali wamewaruhusu kuendelea kuwa wabunge bila kuwa wanachama wa chama cha siasa kinyume na katiba na kuwataka wapinge kufukuzwa kwao wakiwa Wabunge.
Taarifa ya kupinga kufukuzwa kinyume cha katiba ilitangulia kufika Bungeni kabla ya taarifa ya kufukuzwa, hivyo Bunge limewakingia kifua.
Swali gumu: Je, kwanini Halima Mdee na wenzake 18 bado ni wabunge ili hali sio wanachama wa chama cha siasa kwa mujibu wa katiba ya nchi?
Kwa mujibu wa katiba, hap wote bado ni wanachama halali wa Chadema mpaka itakapo toa uamuzi wa shauri lao.
P
 
Nimepitia katiba ya nchi yetu Katiba ambayo hata Rais anapochaguliwa lazima aiape kwanza ndio awe Rais na pia aseme atailinda ataihifadhi na kuiheshimu.

Pia Katiba hiyo hiyo imeeleza Spika anavyopatikana na kuala kuwa atailinda kuitetea na kuihifadhi. Katiba hiyo hiyo imeeleza jinsi Wabunge watakavyopatikana na sifa zao na pia imeeleza jinsi ubunge wao utakavyokoma ikiwa ni pamoja na kufukuzwa uanachama na chama kilichomdhamini.

Katiba hiyo hiyo nimeisoma mwanzo mpaka mwisho sijaona kifungu chochote kinachomlinda mbunge aliyefukuzwa uanachama kuendelea kuwa mbunge kama ilivyo kwa Halima Mdee na wenzake 18.

Suala la kupinga kufukuzwa uanachama ni suala binafsi la aliyefukuzwa na hulifanya mara baada ya kuvuliwa ubunge kama katiba inavyoelekeza lakini imekuwa kinyume kwa suala la wabunge 19 waliofukuzwa uanachama wao serikali na bunge vimeamua kwa makusudi kukiuka katiba kwa kutowavua ubunge kama ilivyowahi kufanya kwa wabunge wa CUF na CCM mara tu baada ya kupata barua ya kufukuzwa uanachama wao kutoka kwenye vyama vyao na bunge halikusubiri mahakama itoe maelekezo, lakini kwa hawa 19 bunge na serikali wamewaruhusu kuendelea kuwa wabunge bila kuwa wanachama wa chama cha siasa kinyume na katiba na kuwataka wapinge kufukuzwa kwao wakiwa Wabunge.

Swali gumu: Je, kwanini Halima Mdee na wenzake 18 bado ni wabunge ili hali sio wanachama wa chama cha siasa kwa mujibu wa katiba ya nchi?

View attachment 2644213View attachment 2644218
hao wamefukuzwa mdomoni tu sio unavyodhania, Mkuu wa chama anajua kucheza na akili za watu.. acha watu watumie kodi kama waengine wanavyotumia.. ukiyafuatilia utakauka mate na kumaliza wino bure..
 
Back
Top Bottom