Kwanini gesti?

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,812
59,392
Nimeona malalamiko na matukio kibao yanayotokea nyumba za wageni yakiletwa humu!Wengine utawagundua ni maInfii kwahiyo hawawezi kupelekana nyumbani ila wengine ni mabachela!Sasa kwa hawa walio single kwanini hua wanapelekana gesti na sio kwenye makazi yao?Jinsi mtu anavyo-value uhusiano inachangia...au ndo inaonyesha kwamba hamna uhusiano pale wala heshima kwa kiasi fulani?Binafsi hua nafikiria mwanaume mpaka akupeleke gesti anakua amekudharau sana!Embu kakaz mtuambie...ni kwanini?
 
sio kakudharau kwa sababu na yeye anaingia humo humo. Kuna mawili yawezekana kama anaishi na wazazi hawezi kukupeleka kwake si heshima kula tundi home kwake,gesti kuna usiri fulani baina yenu wawili,inategemea pia kipato chake labda hana uwezo wa hoteli kubwa. Mwingine yawezekana ana wanawake zaidi ya moja sasa akikupeleka kwake anapoishi itakuwa soo kwake na jirani zake au wazazi wake.wengi wanaowapeleka home kwako ni wale ambao wameshafikia hatua ya uchumba na umeshatambulishwa kwa ndugu.sasa kama ndo mmejuana na ukakubali kula tundi unadai ukalie home kwake kwanini???popote pale mradi pawena utulive na usiri
 
Lizzy ukweli ikiwa mwanaume ana mpenzi mmoja atampeleka nyumbani kwake vinginevyo labda awe anaishi chumba kimoja na haishi peke yake.
 
Na sisi tunaomalizana kwenye vichaka na majumba mabovu unatuweka kwenye kundi gani!
 
Nafikiri pia inategemea mmefahamiana muda gani,as in relationship iko level gani?huwezi tu mmekutana leo kesho unampeleka kitandani kwako hata hujamuelewa huyo mwanamke na kuamua unataka awe nani kwenye uhusiano wako.......honestly,mi sijui naonaje ishu ya kwenda guest...
 
Lizzy ukweli ikiwa mwanaume ana mpenzi mmoja atampeleka nyumbani kwake vinginevyo labda awe anaishi chumba kimoja na haishi peke yake.

Hapo sawa...ila yule anaeishi peke yake nini kinasababisha ukiacha kuwa na mpenzi wake?
 
Nafikiri pia inategemea mmefahamiana muda gani,as in relationship iko level gani?huwezi tu mmekutana leo kesho unampeleka kitandani kwako hata hujamuelewa huyo mwanamke na kuamua unataka awe nani kwenye uhusiano wako.......honestly,mi sijui naonaje ishu ya kwenda guest...
Sasa kwanini wasisubiri mpaka wawaelewe ili wapelekane nyumbani?Yani hapo inaonyesha kitanda chake kina thamani zaidi ya mwili wake!
 
Na sisi tunaomalizana kwenye vichaka na majumba mabovu unatuweka kwenye kundi gani!

Hehe nyie bado watoto!Pesa ya guest hamna..nyumba ya kuwapeleka hamna na hormone zinawazidi nguvu mpaka mnakimbilia vichakani!
 
Back
Top Bottom