Kwanini gazeti la Mwananchi hilisomwi TBC?

Kwanini gazeti la Mwananchi hilisomwi TBC?

Congo

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2008
Posts
2,079
Reaction score
2,334
Naomba kuuliza kwa anayejua. Kwa nini gazeti la Mwananchi halisomwi kwenye kipindi cha jambo leo asubuhi?
 
Labda linachelewa kutoka.....kwih kwih!
 
Inategemea kama gazeti limepelekwa tbc so kama haijawafikia hakuna jinsi, pia inategemea mwenye gazeti anaweza akawa hataki lisomwe au ameshindwa kulifikisha kwa wakati unaopaswa.
 
Hata mimi silisomi sasa hivi. Ila kipindi cha nyuma nilikuwa nalisoma kila siku bila kukosa.
 
Halisomwi sababu halipo au uliliona limerukwa?
 
Tido Mhando alitoka TBC kwenda kuliongoza Mwananchi. ndio bifu ilipoanzia hapo. Mkurugenzi wa sasa wa TBC hawezi kufikia kiwango au upeo wa Tido.
 
hilo swali ni sawa na kuuliza mbona kanisani hawasomi quran
Umemjibu vyema sana, kwa kuwa gazeti la Mwananchi linaigonga sana 'nyundo' serikali ya CCM, na kwa kuwa TBC1, ni 'watiifu' wakubwa wa magamba, ni kitu obvious kuwa chombo hicho kitakuwa tu kinasoma magazeti ya Uhuru, Jambo leo, Mtanzania na Majira, na hata siku moja hutasikia TBC1, isome gazeti la Mwananchi na gazeti la Tanzania Daima, na siku zote watakuwa wanapiga 'fix' kuwa hadi wanaingia mitamboni studio, gazeti hilo, lilikuwa halijawafikia!!
 
Hongera kwa kuwa mfatiliaji wa TBC,nadhan world cup final day ndo tuliagana
 
Me nilidhani pia ungeuliza kwanini gazeti hilo hilo halisomwi ITV/Radio One... Jibu lingekuwa gazeti hili linawapa homa Nipashe... Teh teh.
 
Huyu mleta mada mjinga sana. Kakurupuka bila kufanya utafiti, mbona hata itv hawalisomi na hujauliza?

Na sio hilo tu hata Raia mwema na raia mtanzania hazisomwi mbona hujahoji?

Uharo mtupu.
 
Back
Top Bottom