Kwanini Dar-es Salaam tu,tena Ubungo Bus terminal tu?

mchovu wa fikra

JF-Expert Member
Jul 16, 2016
335
393
Nimekuwa nikijiuliza sana swali hili kuhusu dar-ubungo bus terminal,ni kwanini watu wanalipishwa pesa kuingia ndani ya stendi pindi wawasindikizapo ndugu ama jamaa zao na wakati mwingine hata wao wenyewe ikiwa hawakukata tiketi?

Mbona mtu anaweza msindikiza nduguye airport na asichajiwe pesa,au airport na ubungo, au ubungo ndio yenye thamani zaidi?
Mbona stendi zingine za mikoani hawatulipishi pesa kama hizo? Arusha,Mbeya,Mwanza na Tanga hakuna gharama kama hizo kwanini dar tu?

Ni nani hasa mnufaikaji wa mradi huu ambao gharama zake hupanda kila siku? Kuvuka kigamboni ni sh.200 lakini kuingia ubungo tu ndani mule ambapo hakuna gharama yeyote ambayo halmashauri inaingia kwa wewe kumpeleka ndugu yako pale unalipia Sh.300 kwa sasa,

Serikali nayo imekuwa kinara wa kutuibia raia wake? Magufuli hulioni hili nalo kuwa kero kwa raia? Mradi huu hauna tija bali ni wizi ambao tumekuwa tukiibiwa kwa muda mrefu sana.
Tanzania ni nchi yetu sote jamani msitushike kila mahali.Kwanini ubungo,na pesa za hapo zinapelekwa wapi?

Ubungo mnatuibia sana aisee,maana katika stendi nyingi huwa vyombo vya usafiri ulipishwa na raia kutumia bure miundo mbinu iliyopo hapo,Kulikoni Ubungo bus terminal?

Kwa daraja la kigamboni mlisema kuwa sehemu nyingi duniani hilo ufanyika,naomba kujua kama kuna sehemu duniani wanalipisha raia wake kwa kuingia na kutoka katika stendi ya mabasi.

Kwa wenye majibu na maswali mengine zaidi huenda tukapata ukweli wa gharama hizi naomba tufahamishane wakuu.
Asante.
 
Umenena vyema Mkuu.

Binafsi nakereka na hili sioni tija wala manufaa ya tozo zile. Huwa wanasema lengo ni kugharamia usafi kituoni. Cha kushangaza bado kuna uchafu uliokithili ndani ya kituo.

Hili nalo ni jibu, Tena limeshaiva sana linakaribia kutumbuka lenyewe.

Sipati picha siku Mkulu akishtukiza pale wangapi watang' olewa maana kumejaa uozo.
 
Wanajaribu kupunguza wasio na kazi na vibaka wasifanye pale ndio sehemu ya kwenda kufanya mipango yao ya uovu,japo hawajaweza kutimiza azma yao hiyo kwani vibaka ni wengi na wauza bangi na wasio na sehemu za kulala ni wengi sana mle ndani.
 
Nimekuwa nikijiuliza sana swali hili kuhusu dar-ubungo bus terminal,ni kwanini watu wanalipishwa pesa kuingia ndani ya stendi pindi wawasindikizapo ndugu ama jamaa zao na wakati mwingine hata wao wenyewe ikiwa hawakukata tiketi?
Mbona mtu anaweza msindikiza nduguye airport na asichajiwe pesa,au airport na ubungo, au ubungo ndio yenye thamani zaidi?
Mbona stendi zingine za mikoani hawatulipishi pesa kama hizo? Arusha,Mbeya,Mwanza na Tanga hakuna gharama kama hizo kwanini dar tu? Ni nani hasa mnufaikaji wa mradi huu ambao gharama zake hupanda kila siku? Kuvuka kigamboni ni sh.200 lakini kuingia ubungo tu ndani mule ambapo hakuna gharama yeyote ambayo halmashauri inaingia kwa wewe kumpeleka ndugu yako pale unalipia sh.300 kwa sasa,Serikali nayo imekuwa kinara wa kutuibia raia wake? Magufuli hulioni hili nalo kuwa kero kwa raia? Mradi huu hauna tija bali ni wizi ambao tumekuwa tukiibiwa kwa muda mrefu sana.
Tanzania ni nchi yetu sote jamani msitushike kila mahali.Kwanini ubungo,na pesa za hapo zinapelekwa wapi?
Ubungo mnatuibia sana aisee,maana katika stendi nyingi huwa vyombo vya usafiri ulipishwa na raia kutumia bure miundo mbinu iliyopo hapo,Kulikoni Ubungo bus terminal?
Kwa daraja la kigamboni mlisema kuwa sehemu nyingi duniani hilo ufanyika,naomba kujua kama kuna sehemu duniani wanalipisha raia wake kwa kuingia na kutoka katika stendi ya mabasi.
Kwa wenye majibu na maswali mengine zaidi huenda tukapata ukweli wa gharama hizi naomba tufahamishane wakuu.
Asante.
Hata daraja la kigamboni a.k.a daraja la nyerere gari tu ndio hulipishwa na vyombo vya moto ila watu n bure, sasa iweje ubungo iwe hela?
 
Nasikia mwenye mrad ni muha wa kigoma, na amewachimba mkwara et wakimtumbua pale ataigeuza dar iwe bush kama ujij ndo maan mheshimiwa anapaogopa
 
Wanajaribu kupunguza wasio na kazi na vibaka wasifanye pale ndio sehemu ya kwenda kufanya mipango yao ya uovu,japo hawajaweza kutimiza azma yao hiyo kwani vibaka ni wengi na wauza bangi na wasio na sehemu za kulala ni wengi sana mle ndani.
Sababu kwamba utozaji wa Tshs. 200/= kwa wasindikizaji usaidia kupunguza idadi ya wasio na kazi na vibaka nadhani ni moja ya visingizio tu ili kuhalalisha tozo hiyo.

Kwa kibaka ambaye anajua kwamba akiwa na Tshs. 200 ya kulipia getini na kuingia ndani ya stand atafanikiwa kumwibia abiria hata 1,000/= hawezi kushindwa kuitafuta hiyo 200/=.
 
Sababu kwamba utozaji wa Tshs. 200/= kwa wasindikizaji usaidia kupunguza idadi ya wasio na kazi na vibaka nadhani ni moja ya visingizio tu ili kuhalalisha tozo hiyo.

Kwa kibaka ambaye anajua kwamba akiwa na Tshs. 200 ya kulipia getini na kuingia ndani ya stand atafanikiwa kumwibia abiria hata 1,000/= hawezi kushindwa kuitafuta hiyo 200/=.

Hiyo niliyoitaja sio sababu pekee katika kuamua kuweka kiingilio pale,inaweza kuwa ni sehemu ya chanzo cha mapato kwa jiji ili kugharamia mambo mbalimnali ikiwemo usafi na ulinzi au ni utaratibu wa sehemu kama zile kwani nakumbuka miaka ya nyuma hata kwenye stesheni ya reli Dsm tulikuwa tunakata tiketi za kusindikiza wageni na kama huna utaishia kumpungia mikono kwa mbali,lakini ukikata hiyo tiketi unaingia mpaka kwenye behewa mnapiga stori hadi muda treni kuondoka.
 
Nasikia mwenye mrad ni muha wa kigoma, na amewachimba mkwara et wakimtumbua pale ataigeuza dar iwe bush kama ujij ndo maan mheshimiwa anapaogopa
hata huko kigoma, kuingia ni bure kutoka ni aidha uoneshe tiketi au ulipe 200/-
 
Back
Top Bottom