Balozi wa tanzania nchini kenya.Hivi yule mama Batilda Yuko wapi,nakumbuka swaga zake za vilemba na eloquence yake kwenye kujibu maswali na kutoa maelezo.
Hakupewa hata UDC?
leo arusha katika kata ya daraja 2 ambako kutafanyika uchaguzi wa nafasi ya udiwani Oktoba 28 kikundi cha Green Guard wa CCM waliwapiga wananchi waliokuwa wanaoonyesha ishara ya vidole inayotumiwa na chama cha CDM.Green Guard hao walioongozwa na Jambazi Sugu Jumanne Mjusi.
Mtu huyo anafahamika sana arusha kama jambazi sugu ambaye amehusika na matukio mbalimbali ya kihalifu na mauaji na rekodi zake ziko polisi na alinza kujiingiza katika siasa za CCM katika uchaguzi wa mwaka 2005 akiwa katika kambi ya mgombea ubunge wa CCM Dr.Batilda Burian.
Alitumika kuwatisha wapinzani wa Batilda na kukusanya taarifa mbalimbali hasa za waliokuwa wanampinga mgombea huyo na tangu wakati huo amejikita katika shughuli za kisiasa za CCM, na baadhi ya viongozi wa chama hicho wamekuwa hawapendezwi na hatua ya kumtumia mhalifu huyo wakidai kuwa ni kuchafua chama.
Je ni kwanini vyombo vya dola vimeshindwa kumchukulia hatua mtu huyo ambaye nahatarisha usalama wa watu wengine wanaopinga CCM?Je ni kwanini CCM inamtumia mtu ambaye hana rekodi nzuri katika maisha ya kijamii?
Nimemsikia rpc Arusha akisema huyo jamaa juzi kaiba kwa mtu na amekutwa na bastola ya wizi. Halafu ndie hutumiwa na Ccm kwenye chaguziNani msafi CCM.