ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,681
Siasa za Tanzania lately zimekuwa TOO light.
Ninayo masikitiko makubwa kwa namna nchi inavyokwenda hasa CCM kuwalinda kwa NGUVU zote wauza unga na mafisadi.
Waliapa kuwashughulikia Mafisadi hasa walifocha fedha nje lakini majuzi nimesikia mkuu mmoja akisema hawana fedha za kwenda Uswiswi kufuatilia fedha zilizofichwa huko! Alipotakiwa kueleza kama wamewasiliana na Ubalozi wao hapa nchini alikuwa 'mbogo' kweli kweli.
Hivyo hivyo kwa madawa ya kulevya nayo pia hawataki kuchukua hatua hasa ikizingatiwa kuwa yanamaliza vijana wetu.😕
Mkuu Chama, wako watu kibao kama mimi tusio na vyama, bali wenye "watu!".mkuu Pasco
Naona umekaa kimitego zaidi; haiwezekani hata siku udai eti huna chama hiyo sio kweli naona hiyo triangle uliiyoitengeneza umeweka maslahi yako binafsi hebu tuhabarishe zaidi kwasababu watu wanavutiwa na sera siyo mtu mmoja; El atatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sera za chama chake hali kadhalika ZZK na Jussa watumikia sera za vyama vyao!
Mkuu Chama, unachotakiwa sio lazima kuusema tuu ukweli unaojua ukijulikana utakuchafua, bali kuukubali ukweli kwa kujinyamazia tuu kimya!.Tatizo lako humuelewi Pasco; yeye tayari ameshajigeuza kuwa mpiga debe wa EL kwa hiyo atasema lolote anafahamu fika nafasi ya mgombea wake ina utata hebu jiulize ikiwa "CCM inachofanya ni kulinda wanachma wake" huyu anayempigia debe ni mwanachama wa chama gani? Huoni kama Pasco ni mtu anayejitega mwenyewe?
Nchi hii haitaongozwa na wahuni Chadema never hilo msahau. Njooni na kila aina ya uzushi na hampati kitu.
Lete ushahidi unao unyesha kama ccm wanawalinda hao mafisadi na wauza unga unajua nyinyi vijana mnapoteza muda wenu mwingi kulipa elfu moja kukaa kwenye internet kuhatarisha maendeleo yenu muda wakwenda shule nyinyi kazi yenu kupost utumbo tu kwenye JF
Mkuu Chama, wako watu kibao kama mimi tusio na vyama, bali wenye "watu!".
Hakuna ubishi kuwa CCM ni chama cha mafisadi na kimeoza na kunuka rushwa inside out!. Hii ni kufuatia mafisadi kukamata uongozi wa CCM, na kuwaweka mfukoni viongozi wenu karibu wote!. Jinsi ya kupata uongozi wa CCM siku hizi ni kwa rushwa nje nje!. Uendeshaji wa siasa za CCM ni kwa uongo, fitna na majungu, huku kikihubiri "siasa za majitaka" dhidi ya upinzani wowotw wa ndani au nje!.
Lakini pamoja na madudu yote haya, bado kuna wana CCM wachache ambao ni safi, sio mafisadi, sio walarushwa, wana siasa safi na weledi wa hali ya juu mmoja wao ni Mwalimu. Kuna watu hata leo na toka vyama vyote ambao wanamkubali Mwalimu!.
Vivyo hivyo kwa EL, japo ni kafisadi, na chama cha mafisadi na mifisadi, ila ni yeye ndiye "mwenye uwezo" hivyo wako watu wanamkubali ambao hawana vyama na wengine hata Chadema wanajua akisimama, yule wa kwao hatathubutu hata kupenyeza pua!, kwa sababu kama safari hii ni zamu ya "Kaskazini!", haiwezekani ikawa "Kaskazini Kaskazini!".
CCM ni li zimwi, ila katika uchaguzi wa 2015, its a choice between zimwi likujualo, na lile usiulolijua!.
Yes EL is the devil, and "yule jamaa", pia is the devil!, but between the two devils chose the lesser!, EL is the lesser devil kuliko "yule jamaa!".
Naomba usiniulize "yule jamaa ni nani?!, vitu vingine is only ment kwa ma gt only, if not sorry!.
Pasco.
Mkuu Chama, unachotakiwa sio lazima kuusema tuu ukweli unaojua ukijulikana utakuchafua, bali kuukubali ukweli kwa kujinyamazia tuu kimya!.
Unajua fika kuwa CCM ni chama cha mafisadi!, huu ni ikweli halisi!. Ujajua kuwa "Jamaa" alipata upangaji wa ile nyumba nyeupe kupitia bilioni 40 za ufisadi wa Kagoda!. Unajua mafisadi wakitaka kufisidi, kwanza hukata kadi za CCM!. Ujajua ile mijizi ya EPA ilisamehewa kwa sababu yote ni mianachama ya CCM!. Unajua ni kwanini ilisemehewa?!.
"CCM inalinda Mafisadi na wauza "sembe" kwa sababu ni wanachama wake!" this is a fact, mkuu Chama kubali, katalaa ila ukweli ndio huo!.
Pasco.
Mkuu Chama, kubali kataa, ugombea urais kwa CCM, hupatikana kwa "mbinu! na sio uwezo kama unavyotaka kudai!.Mkuu Pasco
Naona unaendelea kujikanganja; unaposema EL ni lesser devil huoni kwamba unajipaka mavi ya uso mwenyewe? Pamoja na kuwepo wimbi la mafisadi ndani ya chama bado wapo wanaCCM wenye uwezo na wasafi; naona bado unajichanganya sana uraisi wa Tanzania hauotolewi kwa mantiki ya mgombea ni mtu wapi ni uwezo wa mgombea aliyesimamishwa; hili la ukanda unalolishabikia inaonekana wazi unataka kuigawanya Tanzania kwa mafungu kama hoja ni Kaskazini sio lazima iwe Arusha au Kilimanjaro; Tanga nayo ni sehemu ya kaskazini je upo tayari kumpigia debe mgomea kutoka Kaskazini mkoa wa Tanga?
Mkuu Chama, kubali kataa, ugombea urais kwa CCM, hupatikana kwa "mbinu! na sio uwezo kama unavyotaka kudai!.
Kama kweli ni kwa uwezo, hebu wakumbuke wagombea wenu finalists wa 2005, aliyepita, alipita kwa uwezo gani dhidi ya aliyowashinda?!. Au "sura" pia ni uwezo?!.
Kama kweli sasa kwa sasa CCM itateua kutokana na uwezo, then mgombea wenu ndiye "yule" kwa sababu kuiwezo, hana wa kumlinganisha!, kikubalika, hana wa kumsogelea!, kiushindani, hana wa kushindana naye!.
"Rais wa Tanzania mwaka 2015 atatoka Kaskazini! na "TA nayo pia ni "kaskazi!" na "yule" ni "kijana wetu!".
Pasco.
Mkuu Chama, amini usiamini, sijawahi kuvuta hata senti tano kipande toka kwa EL!, nimesikia kuna timu EL, BM, SS na sasa HM, mimi sio member wa timu yoyote kwenye makundi hayo, ila nasimama kwenye ukweli, ndio maana kila siku tunalumbana humu na marafiki zangu kibao.mkuu Pasco
Kuna haja ya kumpigia debe mtu ambaye ni mtata wakati wapo watu safi ambao hawana utata? Kama hoja ni uwezo sina haja ya kutaja majina lakini wengi tu wameonyesha wanaouwezo mkubwa; bado najiuliza na hicho kitendawili chako umepewa ahadi gani? sio bure debe hili unalopiga; mimi nataka tupate mtu safi mwenye maadili simpigii debe mtu yoyote muda huo sina ila naweka mbele maslahi ya taifa na chama changu makini CCM.