Kwanini Balali hakuzikwa Tanzania?

Kwanini Balali hakuzikwa Tanzania?

Status
Not open for further replies.

MAGEUZI KWELI

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2011
Posts
1,947
Reaction score
254
Jamani si kuwa naota..Ninajaribu kukumbukia Serikali yetu ya Tanzania na upana wa maamuzi yake..Tulikuwa na Gavana wa BOT na alikumbwa na Kashfa Lukuki mpaka Macho yoote ya Watanzania yakaganda kwenye Sakata Hilo.

Sasa Huyu jamaa alikufa, Nini kilisababisha Maiti isije Tanzania kwa mazishi na uhakika wa kifo Cha mtu huyu???

Serikali kutokuwa na Maamuzi mapana kuhusu sakata la BOT ilikuwa inakusudia nini??

Nimewaza nikatoka na Hili hebu tuuchambue kidogo huu uongozi tulio nao na upana wa maamuzi yake...

Haya njooni tusemezane Asema Bwana.
 
embu fikiri unyeti wa cheo chake halafu afariki watu wasihudhurie msiba wake, kiongozi gani wa nchi alienda kwenye mazishi yake? Kikwete pamoja na kupenda kuhudhulia misiba huu wa balali mbona hajaenda? Kwa kifupi balali yupo anakula bata tu
 
Inawezekana Kama kweli amekufa alikuwa ameukana uraia wa Tanzania. Pili labda aliacha wosia kwamba akifa asizikwe Tanzania ni mambo binafsi. Alikaa huko USA kwa miaka mingi na alikuwa na nyumba yake huko. Tumwache apumzike. Tupambane na Ndullu afanye kazi kwa tija yaliyopita SI ndwele tugange yajayo!:A S 465:
 
Tuliambiwa kuwa kifo cha Balali kilikuwa ni private death, na mazishi yake pia yakawa ni private (nadhani hata mkewe hajui kama mumewe alikufa) na inawezekana alijizika mwenyewe. RIP Balali watanzania walikuhitaji ujibu tuhuma lakini Mungu alikupenda zaidi.
 
Hajazikwa kwakuwa
bado hajafa ile
ilikuwa funika kombe
mwanaharam apite
 
...D. BALAAHILI, hahahaaa! Hao wahalifu waliopo tunawaangalia tu na kuanza kusaka "wafu"....!!!
 
inshu ya balali is so disguisting, yaani mtumishi wa umma ngazi ya Gavana anakufa then hasafirishwi kurejeshwa nyumbani/nchini kwake?
 
embu fikiri unyeti wa cheo chake halafu afariki watu wasihudhurie msiba wake, kiongozi gani wa nchi alienda kwenye mazishi yake? Kikwete pamoja na kupenda kuhudhulia misiba huu wa balali mbona hajaenda? Kwa kifupi balali yupo anakula bata tu

!!!!!kaaazi kweli kweli!!!kumbe hiyo ni sehemu ya hobie!
 
Nataka afe ili tupate ukweli!akifa kweli ndo ukweli wa mambo ndo utajulikana!Mungu asaidie na aweke mkono ili afe na tupate ukwel wa mambo!
 
Balali yupo hai anadunda kama kawaida.
 
Wakuu niwarejeshe kwenye waraka wa I wa mkuu "Hutaki Unaacha" alipoeleza mambo mengi kumtahadhalisha mkulu. Katika waraka ule ambao umo humu jamvini imeelezwa kuwa Balali aliuawa na kikosi maalum kwa kazi hiyo na kwa maelekezo ya mkulu mwenyewe ili kufunika mambo ambayo yalielekea kumlipukia mkulu mwenyewe. Imeelezwa kuwa baada ya kuuawa alichomwa moto na majivu yake kutupwa baharini. Kwa maelezo zaidi rejea waraka huo Part I, uusome hadi mwisho sio kuishia njiani (kama kawaida ya watz wengi) kwakuwa ni mrefu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom