Kwanini baadhi ya wazazi hufurahishwa na tabia mbaya zinazoonyeshwa na watoto wao wa kiume?

asiyetabirika

Member
Oct 14, 2019
46
55
Nakumbuka ilikuwa ni mara ya kwanza kwenda kuandikishwa shule, nilipelekwa na mshua ila kwenye process za kuniandikisha kuna sehemu aliniacha nje ya ofisi ya mkuu wa shule kwenye bench, wakati nimekaa kwenye lile benchi nje kwenye ofisi ya mkuu wa shule baba akiwa ameingia ndani kumilisha baadhi ya taratibu ili nianze masomo yangu ya darasa la kwanza kuna mwanafunzi wa hiyo shule alikuja kukaa pembeni yangu akaanza kujitapa kuwa yeye yupo darasa la pili na kuna masomo magumu huku akinitisha na ugumu wa hesabu uliopo huko nilitishika kidogo kwa sababu mimi ilikuwa nikihesabu mwisho wangu ulikuwa ni mpaka kumi kwa ufasaha ila mwisho wangu kabisa ilikuwa ni mpaka 20 kwa mbinde.

Baada ya majigambo kadhaa ya yule mwanafunzi wakati anainuka kwenye lile bench tulilokaa wote akalisukuma makusudi kwa nyuma ili nidondokee nyuma kiukweli isingekuwa umahiri wangu ningeshuka chini, nilipatwa na hasira nika mfuata dogo nilimpa vichwa yaani nilipiga vichwa yule dogo alifurukuta kwa kurusha vingumi vyake lakini havikifua dafu nilitandika vichwa yaan hata sikujua ule ujasiri ulitoka wapi na ugumu wa bichwa langu ndio niliupima pale yaani nilitia ndosi, tia vichwa hadi mshua na mwalimu aliyekuwa nae ndani akatoka kuja kutuachanisha nikatia bichwa la mwisho kwa yule mwanafunzi akapiga magoti chini huku kamasi na jasho likimtoka mwilini na kwikwi za kulia.

Baada ya kuachanishwa yule mwalimu alinifokea sana huku akilitolea macho bichwa langu nadhani alishangazwa na ugumu wake akanitishia kunichapa mzee nae alionyesha kukasirika juu ya tukio lile, baada ya muda tukaruhusiwa turudi nyumbani huku yule mwanafunzi tukimuacha kapigishwa magoti akisubiri adhabu yake, mimi niliambiwa nikaanze shule juma tatu kwa sababu siku ile ilikuwa ijumaa.

Sasa cha kushangaza tukiwa njian mzee alionyesha kufurahishwa na uhodari wangu hasa kwa ule ujasiri wa kumtia vichwa mwanafunzi kwa siku ya kwanza tu na ukizingatia nilikuwa bado mgeni kabisa. Mshua aliniambia "safi sana mwanangu yaani usikubali kuonewa,hata mimi baba yako sikuwahi onewa kizembe shule, yaani yule ungetia ngumi na mateke kabisa" mzee alinipa kichwa yaan hata nilipoanza shule sikuwahi kuonewa hadi namaliza shule.

Sasa kwanini imekuwa wazazi wakifurahia badhi ya hizi tabia mbaya kwa watoto wao wa kiume? Taja pia tabia mbaya iliyowahi ifanya halafu ukapongezwa na mzazi kinyume na matarajio yako kuwa ungegombezwa.
 
Hata mimi huwa naonyesha kuchukia mbele ya macho ya watu pindi anapopigana mbele za watu ila tukiwa wenyewe huwa nampongeza nakuzidi kumpa mbinu nilidhani ni tabia yangu kumbe tupo wengi
 
Uswahili kijana wa kiume akionekana yuko mbio na vibinti na kuvitia mimba madingi baadhi hufurahia na kuona vijana wao ni vidume wa shoka..
 
Baba aje kuskia nimempiga mtoto wawatu, kitakachofuata ilikua mtaa mzima utajikusanya karibu na geti la home wakiskilizia baba anavyonipa kisago kikali, Allah amfanyie wepesi apo kitandani alipo, muda wa miaka 15 yuko kitandani strock imemlaza
Pole sana akhy

Allah atamuafu insha Allah
 
Nakumbuka ilikuwa ni mara ya kwanza kwenda kuandikishwa shule, nilipelekwa na mshua ila kwenye process za kuniandikisha kuna sehemu aliniacha nje ya ofisi ya mkuu wa shule kwenye bench, wakati nimekaa kwenye lile benchi nje kwenye ofisi ya mkuu wa shule baba akiwa ameingia ndani kumilisha baadhi ya taratibu ili nianze masomo yangu ya darasa la kwanza kuna mwanafunzi wa hiyo shule alikuja kukaa pembeni yangu akaanza kujitapa kuwa yeye yupo darasa la pili na kuna masomo magumu huku akinitisha na ugumu wa hesabu uliopo huko nilitishika kidogo kwa sababu mimi ilikuwa nikihesabu mwisho wangu ulikuwa ni mpaka kumi kwa ufasaha ila mwisho wangu kabisa ilikuwa ni mpaka 20 kwa mbinde.

Baada ya majigambo kadhaa ya yule mwanafunzi wakati anainuka kwenye lile bench tulilokaa wote akalisukuma makusudi kwa nyuma ili nidondokee nyuma kiukweli isingekuwa umahiri wangu ningeshuka chini, nilipatwa na hasira nika mfuata dogo nilimpa vichwa yaani nilipiga vichwa yule dogo alifurukuta kwa kurusha vingumi vyake lakini havikifua dafu nilitandika vichwa yaan hata sikujua ule ujasiri ulitoka wapi na ugumu wa bichwa langu ndio niliupima pale yaani nilitia ndosi, tia vichwa hadi mshua na mwalimu aliyekuwa nae ndani akatoka kuja kutuachanisha nikatia bichwa la mwisho kwa yule mwanafunzi akapiga magoti chini huku kamasi na jasho likimtoka mwilini na kwikwi za kulia.

Baada ya kuachanishwa yule mwalimu alinifokea sana huku akilitolea macho bichwa langu nadhani alishangazwa na ugumu wake akanitishia kunichapa mzee nae alionyesha kukasirika juu ya tukio lile, baada ya muda tukaruhusiwa turudi nyumbani huku yule mwanafunzi tukimuacha kapigishwa magoti akisubiri adhabu yake, mimi niliambiwa nikaanze shule juma tatu kwa sababu siku ile ilikuwa ijumaa.

Sasa cha kushangaza tukiwa njian mzee alionyesha kufurahishwa na uhodari wangu hasa kwa ule ujasiri wa kumtia vichwa mwanafunzi kwa siku ya kwanza tu na ukizingatia nilikuwa bado mgeni kabisa. Mshua aliniambia "safi sana mwanangu yaani usikubali kuonewa,hata mimi baba yako sikuwahi onewa kizembe shule, yaani yule ungetia ngumi na mateke kabisa" mzee alinipa kichwa yaan hata nilipoanza shule sikuwahi kuonewa hadi namaliza shule.

Sasa kwanini imekuwa wazazi wakifurahia badhi ya hizi tabia mbaya kwa watoto wao wa kiume? Taja pia tabia mbaya iliyowahi ifanya halafu ukapongezwa na mzazi kinyume na matarajio yako kuwa ungegombezwa.
Darasa la kwanza umeshajua mpaka kupiga vichwa? Na mtoto wa darasa la pili ameshajua kuja kutambia wageni kuwa kuna masomo magumu? Mbona watoto wadogo wanapokutana kwa mara ya kwanza tena shuleni hawafanya kama mlivyofanya?
 
Hata mimi huwa naonyesha kuchukia mbele ya macho ya watu pindi anapopigana mbele za watu ila tukiwa wenyewe huwa nampongeza nakuzidi kumpa mbinu nilidhani ni tabia yangu kumbe tupo wengi
Hahaha, una muwekea punching bag ndan, na mafunzo ya siri siri.

Ni uboya mtoto wa kiume akiwa sio mbabe, anapigwa ovyo.
 
Darasa la kwanza umeshajua mpaka kupiga vichwa? Na mtoto wa darasa la pili ameshajua kuja kutambia wageni kuwa kuna masomo magumu? Mbona watoto wadogo wanapokutana kwa mara ya kwanza tena shuleni hawafanya kama mlivyofanya?
hizo shule zenu za saint millen ndio zina wanafunzi kuku wa kisasa.

wewe darasa la kwanza siku ya kwanza tu naripoti nikachokozwa na demu,alikuwa mbabe balaa.bahati kuna mwenzangu alimuonya kwa kusema we fulani muache huyo ni shemeji yake na mwalimu mkuu,nikaachwa kusumbuliwa.vinginevyo ningeianza vibaya siku yangu ya kwanza maana sinaga dogo.
 
Mkuu hizi ni shule za msingi sio English medium, kwenye hizo Shule ukiwa mnyonge itakula kwako yaan utaibiwa penseli wewe utapigwa konzi na yeyote lakin utachomwa na punje ya ubuyu iliyosuguliwa chini lakin utaporwa ufagio au kidumu yaan kila Siku utarudi ukilia nyumban na michozi is I you she had uwe kero kwa wazazi
 
hizo shule zenu za saint millen ndio zina wanafunzi kuku wa kisasa.

wewe darasa la kwanza siku ya kwanza tu naripoti nikachokozwa na demu,alikuwa mbabe balaa.bahati kuna mwenzangu alimuonya kwa kusema we fulani muache huyo ni shemeji yake na mwalimu mkuu,nikaachwa kusumbuliwa.vinginevyo ningeianza vibaya siku yangu ya kwanza maana sinaga dogo.
Nimekuelewa fundi
 
Mwanangu huwa ni mpole sana.... Kila siku namwambia akipigwa arudishie halaf akimbie ila hanielewi. Huwa ananiudhii kila akirudi lazima awe na manung'uniko ya wenzake kumchokoza. Sijui nitumie mbinu gani anielewe.
 
Darasa la kwanza umeshajua mpaka kupiga vichwa? Na mtoto wa darasa la pili ameshajua kuja kutambia wageni kuwa kuna masomo magumu? Mbona watoto wadogo wanapokutana kwa mara ya kwanza tena shuleni hawafanya kama mlivyofanya?
Mlioanza shule enzi za Jakaya mnajulikana tu hata kwa maandishi yenu.
 
Mwanangu huwa ni mpole sana.... Kila siku namwambia akipigwa arudishie halaf akimbie ila hanielewi. Huwa ananiudhii kila akirudi lazima awe na manung'uniko ya wenzake kumchokoza. Sijui nitumie mbinu gani anielewe.
Kama niwakiume mkabidhi bishanga hilo jukumu. Mbona mambo yatakaa sawa kabisa
 
nilipasua vitoto vikatia adabu ila stori haikufika hom but babake akanifuma wacha anitie biti
 
Back
Top Bottom