Kwanini baadhi ya wadada ukiwatongoza, wanajibu kikatili bila sababu?

Balqior

JF-Expert Member
Jun 8, 2021
1,709
5,697
Utakuta unamu-approach mdada kistaarabu uanzishe naye mahusiano ya kimapenzi, ambayo pengine yataishia kwenye ndoa, sometimes unachukua namba yake unachat nae kistaarabu, aloo majibu anayojibu unajiuliza sababu ya kukujibu hivyo huoni, useme labda alikukataa halafu unaendelea kumsumbua hakuna, useme umemwambia kitu cha kumtusi au kumdhalilisha, hamna. Useme huyo mdada ni slay queen mdangaji, ukimuangalia sio tabia zake hata hafananii, kimahusiano useme kuna wanaume waliwahi kumuumiza, unakuta hata ex hana,

Ukimwambia mwanaume usiemtaka kuwa "Nashukuru kwa kunipenda, ila kiukweli sihitaji mahusiano ya kimapenzi na wewe, samahani kama nimekukwaza" halafu, akiendelea kukusumbua ndiyo sasa uchukue hatua Ya kumtukana na kumpa majibu ya dharau utapungukiwa nini?

Ile mtu unamtext sms za kwanza tu, Unapewa majibu ya dharau na ya kunya kama yote nakaaga nashangaa, najiuliza huyu mtu akipata mume, huko kwenye ndoa atakua ni mke wa aina gani.
 
Tafuta hela wanawake watakutongoza wenyewe na wewe ndio utachagua yupi anaekufaa. As a man, focus on building your frame and ignore chasing women.
Ukiwa na hela watakuja wengi...kwasababu ya hiyo hela yako hawatakuwa wanakupenda...

labda umwambie atafute hela akizipata aachane na mambo ya wanawake...ila kama ata deal na wanawak...trust me yaan akiwa na hela ndo atajuta zaidi kuliko mwanzo....kwasababu atafikiria nina kila kitu halafu mbona wanazingua tena
 
Tafuta hela za kutosha,
Ukisha zipata hao wanawake watakua wanapanga foleni wenyewe.
Manara na ela zake mwanamke alimkimbia ukiamin hela ndo kila kitu utakuja kuwa dissapoint sana

Hakuna kitu kinaudhi ujue mwanamke yupo kwa ajili ya hela zako, yaan ukitoa fedha out of equation sio wako ndo maana mtu kama diamond anaishi maisha ya kihuni japokua na utajiri wote ule
 
Ukiwa na hela watakuja wengi...kwasababu ya hiyo hela yako hawatakuwa wanakupenda...

labda umwambie atafute hela akizipata aachane na mambo ya wanawake...ila kama ata deal na wanawak...trust me yaan akiwa na hela ndo atajuta zaidi kuliko mwanzo....kwasababu atafikiria nina kila kitu halafu mbona wanazingua tena
Umeongea point kubwa sana ukiwa na hela halafu ndo utafute wanawake utakuwa dissapointed sana
 
Kama nakuona vile ukisoma reply ya mtongozo🐒

images - 2023-04-03T070310.666.jpeg
 
Unaijua sababu ya kukimbiwa huyo Manara?
Unaijua sababu ya kukimbiwa huyo Manara?
We siumesema atafute hela ndo maana nimekuambia fedha sio kila kitu, kuna watu wana hela za kawaida ila wanaishi na familia zao vizuri,

Kuna watu wana hela wanaishi maisha ya kihuni tusipende kuwaaminisha vijana wetu kwamba hela ndo kila kitu watakua tayari kufanya mambo ya kijinga ili wazipate

Mfano huyo mtoa uzi humjui lakin unamwambia atafute hela
 
We siumesema atafute hela ndo maana nimekuambia fedha sio kila kitu, kuna watu wana hela za kawaida ila wanaishi na familia zao vizuri,

Kuna watu wana hela wanaishi maisha ya kihuni tusipende kuwaaminisha vijana wetu kwamba hela ndo kila kitu watakua tayari kufanya mambo ya kijinga ili wazipate

Mfano huyo mtoa uzi humjui lakin unamwambia atafute hela
Huyo Mwanamke aliyeachana na huyo Manara aliulizwa kua,watu wanasema ulifuata hela,ni kweli? akajibu kwa kuuliza "Kwani Haji ana hela? ana hela za kawaida tu"Kijana tafuta hela acha kujifariji na misamiati,hii Dunia ya leo inahitaji fedha.
 
Back
Top Bottom