Kwanini Afrika imeepukana na utabiri mbaya sana juu ya COVID-19?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,015
1,040
TIM图片20200624161237.jpg


Miezi miwili iliyopita wakati ugonjwa wa Covid-19 uliposhika kasi nchini China na baadaye Ulaya na Marekani, wataalamu wa magonjwa walijaribu kutabiri mahali gani kwengine COVID-19 itaangamiza zaidi

Wengi walifikiri Afrika itakuwa eneo linalofuata kuwa na hatari kubwa, lakini baada ya kufika COVID-19 barani Afrika utabiri wote mbaya haukuwa kweli

Sababu kuu za kwanini Afrika imeepukana na utabiri huo

Watu wengi wamekuwa na nadharia tofauti. Baadhi wanasema uwepo wa vijana wengi. Wakati vifo vingi vya COVID-19 katika Ulaya vimewagusa watu wenye umri wa zaidi ya miaka 60, umri wa kati wa watu wa Afrika ni miaka 19, na asilimia 60 ya bara la Afrika ni watu wenye umri wa chini ya miaka 25.

Wengine wanasema kwasababu hakuna takwimu sahihi kwa vile wengi hawakupimwa.

Lakini kwa ujumla ni kwamba wakati nchi za Ulaya zikisita kuchukua hatua, nchi za Afrika zilichukua hatua mapema za zuio, kuweka karantini na kupima watu joto. Pia Afrika imepambana na magonjwa mengi ya mlipuko hivyo ina uzoefu wa kupamabana na magonjwa.
 
Wakati tahadhari za Ulaya zinatolewa, Afrika ugonjwa ulikuwa haujasambaa sana. Ugonjwa ulipokuja ukakutana na mandalizi ya Kunawa mikono, kutumia barakoa na social distancing. Hatua hizi za tahadhari zikafuatiliwa vilivyo, ndio sababu wagonjwa hawajaa wengi sana hapa Afrika. Sijaongelewa "kikombe" cha Madagascar
 
Wakati tahadhari za Ulaya zinatolewa, Afrika ugonjwa ulikuwa haujasambaa sana. Ugonjwa ulipokuja ukakutana na mandalizi ya Kunawa mikono, kutumia barakoa na social distancing. Hatua hizi za tahadhari zikafuatiliwa vilivyo, ndio sababu wagonjwa hawajaa wengi sana hapa Afrika. Sijaongelewa "kikombe" cha Madagascar

Wakushukuriwa kwanza ni Wachina ambao walifanya tafiti za kina ili kubaini jinsi virus vya corona vinavyo sambazwa , vile vile na mbinu za kujikinga dhidi ya corona - hivyo bara la Africa lilipata bahati ya kujitayalisha jinsi ya kukabiliana na Corona miezi mitatu kabla hauja ingia Barani Africa.

The buzz word which saved continental African is:we were fore warned consequently fore ARMED, thanks to Tsi Xing Ping Govt effort for alarting the World to take precaution.
 
Tatizo maana ya utabiri waliisahau, kadhalika watu wanapanga na mwenye vyake anapanga, na mwenye vyake ni mbora wa kupanga. Ni hilo tu.
 
Back
Top Bottom