Kwanini Abeid Karume si Baba wa Taifa?

Kwanini Abeid Karume si Baba wa Taifa?

ChizzoDrama

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2019
Posts
1,317
Reaction score
1,235
Heshima kwenu Sana JF
.
Leo katika kumbukizi ya kifo cha MWL.JULIUS KAMBARAGE NYERERE , kuna mambo mengi Sana natamani ni yajue
Mosi ; ikiwa tuna fahamu ya kuwa Tanzania ni nchi ambayo imetokana na muunganiko Wa mataifa haya mawili yaani Tanganyika na Zanzibar
.
Pia tunajua fika kuwa kabla ya muunganiko huu mataifa haya yalikuwa na waasisi wake ambao ni MZEE KARUME & MZEE JULIUS
.
Hapo awali nilifikiri hii sentensi ya "BABA WA TAIFA " Ipo katika nafsi ya uwingi kwa maana ya kuwa tuna baba zetu Wa TAIFA wawili
.
Lakini ajabu ni kuwa Tanzania tuna mtambua mzee nyerere pekee Kama baba Wa TAIFA hili kwanini?

Natamani wajuzi Wa mambo mnifahamishe kuhusu hili
 
Ujinga wetu sisi ndio matokeo yetu sisi ,hakika Karume pia ni baba wa Taifa.
kwa kweli mkuu tunasahau kuwa hii nchi ni muungano ingekuwa baba Wa TAIFA la Tanganyika it's okey, lakini why kwa Tanzania
 
Zaidi ya 90% ya Watanzania wanamkubari Nyerere.....
May be ni 40% ya Watu wanaomkubari Karume Zanzibar...
 
Nyerere ni Icon, karume anaweza kuwa baba mdogo wa taifa. Achievements za nyerere haziwezi kulinganishwa na za karume kisiasa.

Movie inaweza kuwa na actors wengi lakini main akawa mmoja.
 
Heshima kwenu Sana JF
.
Leo katika kumbukizi ya kifo cha MWL.JULIUS KAMBARAGE NYERERE , kuna mambo mengi Sana natamani ni yajue
Mosi ; ikiwa tuna fahamu ya kuwa Tanzania ni nchi ambayo imetokana na muunganiko Wa mataifa haya mawili yaani Tanganyika na Zanzibar
.
Pia tunajua fika kuwa kabla ya muunganiko huu mataifa haya yalikuwa na waasisi wake ambao ni MZEE KARUME & MZEE JULIUS
.
Hapo awali nilifikiri hii sentensi ya "BABA WA TAIFA " Ipo katika nafsi ya uwingi kwa maana ya kuwa tuna baba zetu Wa TAIFA wawili
.
Lakini ajabu ni kuwa Tanzania tuna mtambua mzee nyerere pekee Kama baba Wa TAIFA hili kwanini?

Natamani wajuzi Wa mambo mnifahamishe kuhusu hili
ZANZIBAR si TAIFA, unataka awe baba wa Taifs gani?

Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, ni mkoa flani tu.
 
Nyerere ni Icon, karume anaweza kuwa baba mdogo wa taifa. Achievements za nyerere haziwezi kulinganishwa na za karume kisiasa.
Movie inaweza kuwa na actors wengi lakini main akawa mmoja.
sikupingi ingekuwa muvi inaitwa Tanganyika NYERERE ni main character ,vivyo hivyo ingeitwa Zanzibar KARUME angekuwa ni main character , so linapo kuja suala la pamoja kwanini heshima ziwe tofauti??
Pia kuna muvi zina staring wawili (ref DOUBLE IMPACT) Ya jean claud van dame
 
sikupingi ingekuwa muvi inaitwa Tanganyika NYERERE ni main character ,vivyo hivyo ingeitwa Zanzibar KARUME angekuwa ni main character , so linapo kuja suala la pamoja kwanini heshima ziwe tofauti??
Pia kuna muvi zina staring wawili (ref DOUBLE IMPACT) Ya jean claud van dame
Linganisha achievements za hao watu wawili kwenye bara letu la Afrika.
 
Nyerere aliishi muda mrefu zaidi ya Karume, hiibimemfanya akumbukwe na vizazi vingi.
naweza nisikubaliane na wewe mkuu wangu hasa hapa kwenye umri ,maana dunia imeshuhudia wanasayansi nguli kweli kweli na wenye heshima zao Kama ISAACK NEWTON richa ya kuishi miaka michache ,nadhani kuhusu suala la kukumbukwa ni LEGACY aliyo iacha MTU
.
Na sikati kuwa NYERERE kwa kwetu bara anayo legacy kubwa lakini vipi kwa huko visiwani ? Ni kweli kwamba alimzidi KARUME katika mipaka take?
 
Back
Top Bottom