Kwani pale Magogoni pana nini

Kwani pale Magogoni pana nini

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,880
Reaction score
828,445
Simulizi zinasema kuwa kuna watu waliwahi kupachezea na kuzindika mambo yao mahali hapo. Ndiyo maana kuna mambo ambayo ukifanya kinyume, yanakurudia mwenyewe kwa namna mbaya sana.

Usiku giza linapoingia na watu wanapoenda kulala, mizimu huamka na yale maroho huanza kazi zake. Kuna simulizi pia za watu kupelekewa moto vibaya sana. Haya yalitokea zaidi kipindi kile kabla ya yule wa mwisho kuondoka. Wanasema kipindi hicho hakukuwa na kulala kabisa.

Hata hivyo, location yenyewe inaweza kuwa tatizo kubwa. Pale ni kama madhabahu takatifu; ukikipapasa vibaya kidogo tu au kukinajisi, basi vile viumbe vikichoka kukaa kwenye maji makuu huja pale ufukweni kwao kubarizi.

Hiyo midude, wanasema haina mzaha, hasa kuanzia saa saba mpaka saa tisa. Ni kama eneo lote linachukuliwa kwa muda fulani hakuna kutoka, ila kuingia ni ruksa.

Niliwahi kuishi nyumba ya aina hiyo huko Tanga. Wenyeji waliniambia, “Hapo pazito, usipaone kama kawaida. Hakikisha hupachafui kiroho. Na siku ukienda kuchafuka nje, hakikisha unajitakasa kabla ya kuingia ndani.”

Siku moja ya weekend nikapita chocho moja lenye mitungi na mikasi. Nikajifurahisha nafsi mpaka karibu siku inapinduka ndipo nikarudi nyumbani. Bahati mbaya nikajisahau kujitakasa.

Nikaingia ndani, nikatia komeo, nikajilaza fofofooo foool!

Saa nane usiku nikastuka ghafla. Nikakuta chumba chote kimejaa mwanga. Nikacheki taa—haikuwa imewashwa. Nikadhani labda ni wenge la mitungi tu. Kabla sijakaa sawa, ule mwanga ukapotea, nami nikahisi wazi kabisa kuwa pale chumbani (sio kitandani) sikuwa peke yangu.

Vituko vilivyoendelea kuanzia hapo mpaka alfajiri, kabla ya adhana ya kwanza, sitakaa nisahau kamwe.

Hapa palipo sasa pamechafuliwa na kunajisiwa vibaya sana. Si mahali pasafi tena, wala hapana utukufu. Yale madude tayari yamefanya hapo kuwa kiwanja chao cha kudumu, na mizimu imeruhusu. Hivyo ni mahali hapakaliki, hapalaliki!

Falme mbili haziwezi kukaa pamoja—ufalme wa nuru na ufalme wa giza lazima zipigane. Ukivaa joho jeupe nje lakini ndani umejaa uvundo, lazima usande.

Wapangaji waliotangulia walitumia damu kubwa kwa uchache na kwa uangalifu mkubwa, ndiyo maana walivumiliwa kwa kiasi fulani. Lakini washauri wabaya na vipotoshi waliodai itumike damu kubwa kwa wingi wameharibu kila kitu kabisa.

Sasa miungurumo, miito, vilio na taswira za wenye damu zao zinawaandama kila wanapokanyaga pale. Panatisha sana, na kuogopesha kupita kiasi.

Ukimuona baba ameondoka kwenye nyumba yake, hata kama ni ya kupanga, akaenda kuishi uswazi kwenye nyumba ndogo—wakati mwingine usimkejeli. Muonee huruma. Ana mambo mazito na magumu moyoni.

Good morning, Tanganyika!
1767724311321.jpg
 
Simulizi zinasema kuna watu waliwahi kupachezea na kuzindika mambo yao, hivyo kuna mambo ukiyafanya kinyume.. Yaani ndivyo sivyo inakula kwako mbaya

Usiku kiza kikiingia na watu wakienda kulala, mizimu vinyamkera na yale maroho huingia kazini
Kuna simulizi pia za kupelekewa moto vibaya Sana, na hii ilitokea sana kipindi kile kabla ya yule aliendoka wa mwisho! Wanasema ilikuwa hakuna kulala
Hata hivyo location pia inaweza kuwa ni tatizo kubwa.. Pale ni sawa na madhabahu takatifu pakichezewa kidogo tu pakanajisika, basi midude ikichoka kukaa kwenye maji makuu huenda pale kaka ufukweni pao kubarizi

Hiyo midude wanasema haina show za kitoto hasa kuanzia saasaba mpakasaatisa.. Ni kama vile yanaliteka eneo lote kwa muda hakuna kutoka mtu Ila kuingia ruksa
Nilishawahi kuishi nyumba ya namna hiyo Tanga. Wenyeji wakaniambia hapo pazito usipaone hivyo, hakikisha hupachafui kiroho.. Na siku ukienda kuchafuka nje hakikisha unakuwa msafi kabla hujaingia ndani
Weekend moja nikapita chocho moja lenye mitungi na mikasi.. Nikaifurahisha nafsi mpaka karibia siku kupinduka ndio nikarudi kwangu..Si nikajisahau kujitakasa!
Nikaingia ndani nikatia komeo nikalala fofofoo fool!
Nane usiku nikastuka na kuona chumba chote kina mwanga.. Kucheki taa haiwaki. Nikadhani ni wenge la mitungi tuu. Kabla sijakaa sawa mwanga ule ukapotea na nikahisi kabisa pale chumbani (sio kitandani) siko pekeyangu
Vituko vilivyoendelea baada ya pale mpaka alfajiri kabla ya adhana ya kwanza sitakaa nivisahau
Hapa pa sasa pamechafuliwa na kunajisiwa vibaya Sana! Sio pasafi na hapana utukufu tena
Yale madude yameshapageuza kiwanja chao cha kudumu.. Na mizimu imeruhusu. Hivyo hapakaliki hapalaliki!

Falme mbili hazikai pamoja hasa ufalme wa nuru na ufalme wa giza ni lazima zitasigana! Ukivaa joho jeupe nje lakini ndani umefutika uvundo lazima usande
Wapangaji waliotangulia walitumia damu kubwa kwa uchache na kwa uangalifu mkubwa ndio maana walau walivumiliwa kiasi chake

Washauri wabaya na vipotoshi waliosema itumike damu kubwa halafu nyingi ndio wameharibu kabisa
Mwangi, miito, vilio na taswira za wenye damu zao zinawaandama kila wakitia miguu yao! Panatisha Sana na kuogopesha Sana!

Ukimuona baba kahama kwenye mjumba wake wat maana hata kama ni wa kupanga na kwenda kuishi uswazi kwenye nyumba ndogo sometimes usimkejeli bali muonee huruma! Ana mazito na magumu moyoni

Good morning Tanganyika!View attachment 3526449
Kaka Na mie Nawaza niende kuunga juhudi kabla ba mwenye nyumba hajaja kunitupia makopo yangu nje
 
Kaka Na mie Nawaza niende kuunga juhudi kabla ba mwenye nyumba hajaja kunitupia makopo yangu nje
Hapana my dear sister.. Ukikwama tutakwamuana! Sasa hivi kuunga juhudi hakulipi tena!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom