bushman
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,411
- 743
kwako marehemu baba wa taifa,natumaini umepunzika kwa amani hakika nataka kukujuza maajabu mengi yaliyotokea tz toka uaage dunia;
- Kepten john komba amekuwa mbunge lakini kazi yake ni kusinzia tu bungeni
- Lowasa alipata uwaziri mkuu
- CCM imekuwa kichaka cha mafisadi
- Chama Chako kimejaa magamba tu
- Raisi wa nchi hajui kwa nini watu wake ni maskini
- Madini ambayo uligoma yasichimbwe mpaka watu wako watakapokuwa na uwezo,leo yanachimbwa na wananchi wanauwawa kwa risasi wakipinga unyonyaji lakini serikali inawaita wavamizi.
- Magari ya ikulu yanachakachuliwa mafuta
- Mafisadi wanaitwa mashujaa
- Uongozi unapatikana kwa kuwa na pesa badala ya uwezo wa mtu
- Kilimo kimekuwa ni siasa tu watu wanakufa na njaa
- Kiongozi mkuu wa nchi (mkuu wa kaya) anahubiri udini
- Semina elekezi kwa mawaziri zakutosha pamoja ya kuwa wanakutana kwenye vikao vya baraza la mawaziri
- Yusuph makamba alishika nafasi ya katibu mkuu CCM
- UVCCM sio kisima cha fikra tena imegeuka kijiwe cha kahawa