Kwako kipi ni kipimo cha kiongozi bora?

Kwako kipi ni kipimo cha kiongozi bora?

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
35,768
Reaction score
86,453
Naona kama watu wanakuwa na mikanganyiko haswa katika siasa zetu hapa Tanzania, imekuwa sio vuta nikuvute bali ni vurumai yakufuata mtu yoyote kwasababu mbalimbali aidha, nyadhifa fedha ama kujuana!.

Hivyo binafsi nikawaza kipi ni kipimo cha kiongozi bora..?

Binafsi naweza kusema kiongozi bora ni yule anaeongoza watu kufikia malengo yao, huku akilinda nakuendeleza mazuri yaliyopo na yajayo, awe muwajibikaji,mstahimilivu na weledi wakuona mbele, maana kuwa kiongozi ni kuwa dira yakuona mbele!.

Sasa sijui kama hapa kwetu tunaangalia haya au tunachagua tu kama tunavyochambua maharage!. nafikiri kila mtu aelewe dhana ya uongozi na umuhimu wa kura yake kabla hajaamua tu kutia tiki baadae ikawa kizaizai!.

Naona kama vile watu wamepotoka hivi sasa!, wanapenda kusikiliza viongozi wakitoa umbea na vijembe wala si hoja za wapi tulipo, tunaenda wapi kivipi na kwanini...?

Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.
 
Naona kama watu wanakuwa na mikanganyiko haswa katika siasa zetu hapa Tanzania, imekuwa sio vuta nikuvute bali ni vurumai yakufuata mtu yoyote kwasababu mbalimbali aidha, nyadhifa fedha ama kujuana!.

Hivyo binafsi nikawaza kipi ni kipimo cha kiongozi bora..?
Binafsi naweza kusema kiongozi bora ni yule anaeongoza watu kufikia malengo yao, huku akilinda nakuendeleza mazuri yaliyopo na yajayo, awe muwajibikaji,mstahimilivu na weledi wakuona mbele, maana kuwa kiongozi ni kuwa dira yakuona mbele!.

Sasa sijui kama hapa kwetu tunaangalia haya au tunachagua tu kama tunavyochambua maharage!. nafikiri kila mtu aelewe dhana ya uongozi na umuhimu wa kura yake kabla hajaamua tu kutia tiki baadae ikawa kizaizai!..
Naona kama vile watu wamepotoka hivi sasa!, wanapenda kusikiliza viongozi wakitoa umbea na vijembe wala si hoja za wapi tulipo, tunaenda wapi kivipi na kwanini...?

Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.
Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.👌🏿
 
Kiongozi bora ni yule anayeamini katika haki, anayesimama kwenye ukweli, mzalendo wa kweli, mtu mwenye akili nyingi na maono ya mbali, mtu mwenye busara na hekima, mnyenyekevu, ni mkali kwa wala rushwa, wazembe, wapiga dili, wahuni, nk.
 
Kiongozi bora ni yule anayeamini katika haki, anayesimama kwenye ukweli, mzalendo wa kweli, mtu mwenye akili nyingi na maono ya mbali, mtu mwenye busara na hekima, mnyenyekevu, ni mkali kwa wala rushwa, wazembe, wapiga dili, wahuni, nk.
Kabisa una akili kubwa sana
 
Naona kama watu wanakuwa na mikanganyiko haswa katika siasa zetu hapa Tanzania, imekuwa sio vuta nikuvute bali ni vurumai yakufuata mtu yoyote kwasababu mbalimbali aidha, nyadhifa fedha ama kujuana!.

Hivyo binafsi nikawaza kipi ni kipimo cha kiongozi bora..?

Binafsi naweza kusema kiongozi bora ni yule anaeongoza watu kufikia malengo yao, huku akilinda nakuendeleza mazuri yaliyopo na yajayo, awe muwajibikaji,mstahimilivu na weledi wakuona mbele, maana kuwa kiongozi ni kuwa dira yakuona mbele!.

Sasa sijui kama hapa kwetu tunaangalia haya au tunachagua tu kama tunavyochambua maharage!. nafikiri kila mtu aelewe dhana ya uongozi na umuhimu wa kura yake kabla hajaamua tu kutia tiki baadae ikawa kizaizai!.

Naona kama vile watu wamepotoka hivi sasa!, wanapenda kusikiliza viongozi wakitoa umbea na vijembe wala si hoja za wapi tulipo, tunaenda wapi kivipi na kwanini...?

Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.

Katika Tawala nyingi sana za Afrika na Tanzania ikiwamo, hakuna Viongozi bali kuna WATAWALA.

NB: Elewa tofaufi iliyopo Kati ya Viongozi na Watawala.
 
Haki imesimama kama haki na imekamilika bila kutegemea asilimia kama kipimo , nipo nalewa kimtindo🤣
Wewe tulia nikuelimishe na nikufundishe ukisema haki kama haki tu itakuwa hujamaliza!, maana sio kila hitaji ni haki na sio kila haki ni hitaji!. mfano ukisema kila mtu apewe haki kwa asilimia mia utayaboronga haki lazima iwe na wastani!, maana watakuja mashoga watalilia kupewa haki!, watakuja wauwaji watakuja nao kulilia haki so haki kama haki lazima iwe na limit na ndio maana kuna kitu kinaitwa sheria!.
sheria ndio kipimo cha haki.
 
Anayeongoza kwa misingi ya haki , utu na huruma.
Anayejua ,anayejali maslahi ya anaowaongoza
Asiyependa rushwa na ubadhilifu wa mali za anaowaongoza.
Mwenye msimamo usioyumba.
Mcha Mungu.
Mwenye maono na uthubutu.
 
Kiongozi bora ni yule anayeamini katika haki, anayesimama kwenye ukweli, mzalendo wa kweli, mtu mwenye akili nyingi na maono ya mbali, mtu mwenye busara na hekima, mnyenyekevu, ni mkali kwa wala rushwa, wazembe, wapiga dili, wahuni, nk.
Hili neno "Haki" nafikiri linahitaji mjadala
 
Naona kama watu wanakuwa na mikanganyiko haswa katika siasa zetu hapa Tanzania, imekuwa sio vuta nikuvute bali ni vurumai yakufuata mtu yoyote kwasababu mbalimbali aidha, nyadhifa fedha ama kujuana!.

Hivyo binafsi nikawaza kipi ni kipimo cha kiongozi bora..?

Binafsi naweza kusema kiongozi bora ni yule anaeongoza watu kufikia malengo yao, huku akilinda nakuendeleza mazuri yaliyopo na yajayo, awe muwajibikaji,mstahimilivu na weledi wakuona mbele, maana kuwa kiongozi ni kuwa dira yakuona mbele!.

Sasa sijui kama hapa kwetu tunaangalia haya au tunachagua tu kama tunavyochambua maharage!. nafikiri kila mtu aelewe dhana ya uongozi na umuhimu wa kura yake kabla hajaamua tu kutia tiki baadae ikawa kizaizai!.

Naona kama vile watu wamepotoka hivi sasa!, wanapenda kusikiliza viongozi wakitoa umbea na vijembe wala si hoja za wapi tulipo, tunaenda wapi kivipi na kwanini...?

Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.
 
Wewe tulia nikuelimishe na nikufundishe ukisema haki kama haki tu itakuwa hujamaliza!, maana sio kila hitaji ni haki na sio kila haki ni hitaji!. mfano ukisema kila mtu apewe haki kwa asilimia mia utayaboronga haki lazima iwe na wastani!, maana watakuja mashoga watalilia kupewa haki!, watakuja wauwaji watakuja nao kulilia haki so haki kama haki lazima iwe na limit na ndio maana kuna kitu kinaitwa sheria!.
sheria ndio kipimo cha haki.
Nimekuelewa sana , kwani hizo sheria unazodai zimebana vipi makalio ya wangese bongo?
 
Hili neno "Haki" nafikiri linahitaji mjadala
Uko sahihi. Ni viongozi wachache sana wanaoamini kwenye hilo neno "HAKI". Maana ni neno pana! Binadamu anahitaji haki ya kuishi, haki ya kuoa na kuolewa, haki ya kuchagua na kuchaguliwa, haki ya......! Kuna haki nyingi sana.
 
Nimekuelewa sana , kwani hizo sheria unazodai zimebana vipi makalio ya wangese bongo?
Mh! hapa mimi sijadili ni sheria ipi imebana ama imeachia!, hapa nilikuwa nakuelewesha dhana ya haki ilivyopana!.. kuhusu sheria huo ni mjadala mwengine leo ningependa tuchambue kiongozi bora...😂
 
Hili neno "Haki" nafikiri linahitaji mjadala
Braza haki ,imesimama yenyewe baada ya kupimwa kwenye mlinganganyo miwili ambayo hiyo milinganyo inahitaji watu wa haki pia , hivyo haki ikisimama kwenye misingi hiii haihitaji propaganda, na hiyo ipo wazi kama ya mbuzi bwashee.
 
Kwa mfano, wanaweza kuwa na mapungufu lakini hawa ni mfano
FB_IMG_1710699424957.jpg
FB_IMG_1747677777001.jpg
 
Mh! hapa mimi sijadili ni sheria ipi imebana ama imeachia!, hapa nilikuwa nakuelewesha dhana ya haki ilivyopana!.. kuhusu sheria huo ni mjadala mwengine leo ningependa tuchambue kiongozi bora...😂
Kiongozi bora awe kwenye misingi ya haki tu basiii
 
Back
Top Bottom