Naona kama watu wanakuwa na mikanganyiko haswa katika siasa zetu hapa Tanzania, imekuwa sio vuta nikuvute bali ni vurumai yakufuata mtu yoyote kwasababu mbalimbali aidha, nyadhifa fedha ama kujuana!.
Hivyo binafsi nikawaza kipi ni kipimo cha kiongozi bora..?
Binafsi naweza kusema kiongozi bora ni yule anaeongoza watu kufikia malengo yao, huku akilinda nakuendeleza mazuri yaliyopo na yajayo, awe muwajibikaji,mstahimilivu na weledi wakuona mbele, maana kuwa kiongozi ni kuwa dira yakuona mbele!.
Sasa sijui kama hapa kwetu tunaangalia haya au tunachagua tu kama tunavyochambua maharage!. nafikiri kila mtu aelewe dhana ya uongozi na umuhimu wa kura yake kabla hajaamua tu kutia tiki baadae ikawa kizaizai!.
Naona kama vile watu wamepotoka hivi sasa!, wanapenda kusikiliza viongozi wakitoa umbea na vijembe wala si hoja za wapi tulipo, tunaenda wapi kivipi na kwanini...?
Nyakati za uchaguzi zimekuwa za watu kusema "twende tukapige hela!" huku ni sawa na kujichimbia shimo ukiamini ni kisima kumbe ni kaburi!.
Hatari sana, ila kama kuna jambo nimejifunza hivi sasa ni kwamba Kila kwenye point ya maumivu huwa kuna fulsa.
So, kiafrika afrika hasa kwenye nchi yangu ni ngumu sana kumpata kiongozi Bora kwasababu swala hili ni very subjective baina ya mwananchi wa chini wa kati na yule wa juu kiuwezo.
Ndio maana haijawahi kutokea hata mara moja vijana au wapiga kura wakawa na mtazamo mmoja juu ya kiongozi fulani.
Watu wa chini wanaamini kiongozi Bora ni yule ambae anatenda kwa haki lakini pia aliye na uwezo wa kuzisimamia lasirimali za nchi kiweledi na kusukuma gurudumu la maendeleo kiwazi zaidi.
Lakini watu wengi ambao wako na maisha ya kati na juu hawajali chochote kuhusu maendeleo ya jumla kama taifa ila wao wanachojali ni maendeleo yao binafsi, kwahiyo walio wengi huwa kwao kiongozi Bora ni yule ambae atawahakikishia usalama wa biashara zao na vyanzo vya ukwasi wao pasipo kujali kama ni biashara halila au si halali.
Sasa ukiangalia hapo utaona jinsi ilivyongumu kwasababu kiafrika uongozi huwa ni ngumu kupatikana kwa maamuzi ya sandukuni isipokua kuna watu hukaa mstari wa mbele ili kusaidia kiongozi aweze kupatikana, na katika watu hao hajawahi kuwepo mtu wa chini ila ni wale wa kati na wajuu zaidi ndio huwa wanasukuma hizi kete.
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema "ukiona mtu yeyote linapoongelewa swala la mabadiliko fulani fulani yeye akawa ni mpingaji mkubwa wa swala hilo jua huyo ameshiba au anashiba na mfumo uliopo kwahiyo anahofia mabadiliko yajayo yasije yakaharibu ule mfumo wa ushibaji wake kwahiyo anakua mtu wa kwanza kupinga kwa nguvu zote, ila mtu mwenye njaa hawezi kupinga swala la mabadiliko hasa ukishamwambia tukifanya haya mabadiliko wote tunaweza kuanza kushiba, atakubali haraka kwasababu hana cha kupoteza hata hayo mabadiliko yasipoleta matokeo ambayo yalikusudiwa".
Inshort katika nchi nyingi za kiafrika ule mfumo ambao ulikua unatumiwa na watawala wa kikoloni kutunyonya ndio ambao unatumika na watawala waliopo kutunyonya na hii yote ni kwasababu wanajua point ya maumivu ambayo watu wako nayo, kwahiyo hii kwao ni kama fulsa.
That's why swala hilo ni subjective kwa maana big papa wanajua aina ya kiongozi ambao wao wanamtaka so Kila muda unapofikia wanarudi kwa wengine kuwaaminisha huyu ndiye kwa kutumia ile point ya maumivu ambayo wako nayo na kundi kubwa la watu watasema huyu ndiye na wataunga mkono juhudi over and over again.