Kwa yanayotokea Burundi, Kuna haja ya kuwa na EAC?

johnmashilatu

JF-Expert Member
Sep 16, 2010
718
703
Kwa muda sasa, nimekuwa nikijaribu kuitazama jumuiya ya afrika mashariki kwa lengo la kutafuta manufaa yake hususan kwa watu maskini kabisa wanaoishi kwenye vijiji vya nchi hizo, lakini lakini kwa bahati mbaya nimekosa kuyaona hayo manufaa.

Jumuiya hizi za kikanda na nyingine zinazofanana na hizo hususan katika bara la afrika ni sawa na klabu za kuwakutanisha viongozi wakuu wa nchi wanachma ili kupiga soga huku wakitumia mamilioni ya fedha za walalahoi w amataifa hayo kwa ajili ya kujiburudisha.

Kinachoendelea Burundi ni kielezo ya fikra hizo kuwa jumuiya hizi hususan EAC ni vitengo vya kikanda vyenye lengo la kuwakutanisha na kuwanufaisha watu wachache huku mamilioni wengine wakiachwa wasijue haswa kinachoendelea.
Ni aibu kusikia wiki moja baada ya baada ya kuanza kwa machafuko yanayopeleka vifo na maelfu wengine kuishi ukimbizini, ndio sasa Jumuiya ya EAC inaanza kuchukua hatua kwa kinachoendelea nchini Burundi.

Sasa EAC ndio imetuma Ujumbe Burundi kwenda "kufahamu" nini kinaendelea wakati nchi za mbali na hata jumuiya nyingine kama UN zikiwa zimeanza mapema kuchukua hatua dhidi ya mgogoro wa Burundi. Baada ya tume kurejea na kuandaa ripoti ndio viongozi ( akiwemo na mwanzilishi wa dhahama hii, Nkurunziza) wa chi wanachama watakutana ili kubaini hatua za kufanya.

Najiuliza tu, Jumuiya hii iliyoko katika ncjhi za ukanda wenye historiaya machafuko ya mara kwa mara, inacho chombo ambacho kinaheshimiwa kwamba kikitoa maamuzi ya haraka na yatatekelezwa?
 
Watu wa Afrika Mashariki tunafanana sana .........Hili la Burundi nalo limeundiwa tume.

Wanamlinda mwenzao, hawawezi kumtosa Pierre wakati Kagame naye ana mpango wa kuongeza kipindi kingine hali kadhalika Museveni .
 
Watu wa Afrika Mashariki tunafanana sana .........Hili la Burundi nalo limeundiwa tume.

Wanamlinda mwenzao, hawawezi kumtosa Pierre wakati Kagame naye ana mpango wa kuongeza kipindi kingine hali kadhalika Museveni .

Umeona eeh,
Unda tume ili kuahirisha tatizo na mwisho kuwasahaulisha wahusika, watawala wote ndivyo walivyo. Kwanini tusichukue hatua kama wengine ambazo zinaweza kuwa kuwazuia watu kadhaaa kuingia nchi nyingine na kushikilia/kuzuia mali zao n.k?
 
Watu wa Afrika Mashariki tunafanana sana .........Hili la Burundi nalo limeundiwa tume.

Wanamlinda mwenzao, hawawezi kumtosa Pierre wakati Kagame naye ana mpango wa kuongeza kipindi kingine hali kadhalika Museveni .

The same applied to Mbowe, amebadili katiba ya chama akaongeza muda wa kuwa mwenyekiti bila kikomo, wanachadema kimyaaa, akiwa rais, atabadili katiba ya nchi ili aendelee mtaona kitakachofuata!
 
Narudia, Kagame mtusi, Mseven mtusi, Kabila fake mtusi. hapa hakuna siasa kuna kundi la kigaidi linalotaka kutawala kwa nguvu kutengeneza Bahima empire, wanaingia kidemokrasia lakini hawatoki kamwe, sasa mnataka na Burundi aje mtusi kwa njia ya demokrasia ili kukamilisha Bahima empire.

Sio kirahisi hivyo, Afrika mashariki haiwezi kutawaliwa na magaidi kwa kisingizio cha demokrasia... kamwe abadan
 
Narudia, Kagame mtusi, Mseven mtusi, Kabila fake mtusi. hapa hakuna siasa kuna kundi la kigaidi linalotaka kutawala kwa nguvu kutengeneza Bahima empire, wanaingia kidemokrasia lakini hawatoki kamwe, sasa mnataka na Burundi aje mtusi kwa njia ya demokrasia ili kukamilisha Bahima empire.

Sio kirahisi hivyo, Afrika mashariki haiwezi kutawaliwa na magaidi kwa kisingizio cha demokrasia... kamwe abadan

umeongea kwa hisia kali sana.
 
Hata kabla ya hapo EAC imekuwa matatizo sana. Hatuna urafiki wa kusema tuunde jumuiya sema ni kwasababu tunashre mipaka tu.
 
Mpaka leo viongozi wakuu wa Afrika Mashariki kuwa kimya kwa yale yanayoendelea Afrika Mashariki kule Tanzania (Kigoma) na Ngara kupokea wakimbizi toka Burundi na Kutomuweka chini raisi wa Burundi kwa uvunjifu wa wazi wa katiba yao, ndo kusema Umoja huu umeona ni sawa pamoja mdororo wa amani unaoonekana wazi? Karibu utoe maono yako.
 
Mpaka leo viongozi wakuu wa Afrika Mashariki kuwa kimya kwa yale yanayoendelea Afrika Mashariki kule Tanzania (Kigoma) na Ngara kupokea wakimbizi toka Burundi na Kutomuweka chini raisi wa Burundi kwa uvunjifu wa wazi wa katiba yao, ndo kusema Umoja huu umeona ni sawa pamoja mdororo wa amani unaoonekana wazi? Karibu utoe maono yako.

Kwani katiba iliandikwa lini na inasemaje? Si inasema Rais achaguliwe kwa kupigiwa kura na Wanachi, je Nkurunzinza amepigiwa kura na Wananchi mara ngapi? Mara moja tu - kwa hiyo ana haki ya kuchaguliwa kidemokrasia kwa mara ya pili - ndivyo katiba inavyo sema, sasa wajanja wanaingiza mambo ya ukabila chini chini kutimiza malengo/ndoto zao za kuhunda Empire - na hiki ndicho kinaendelea Burundi.
 
Kwani katiba ilihundwa lini na inasemaje? Si inasema Rais achaguliwe kwa kupigiwa kura na Wanachi, je Nkurunzinza amepigiwa kura na Wananchi mara ngapi? Mara moja tu - kwa hiyo ana haki ya kuchaguliwa kidemokrasia kwa mara ya pili - ndivyo katiba inavyo sema, sasa wajanja wanaingiza mambo ya ukabila chini chini kutimiza malengo/ndoto zao za kuhunda Empire - na hiki ndicho kinaendelea Burundi.
Nashukuru kwa maoni yako ila hapo kwenye rangi nyekundu naona umeeleweka lakini.......................
 
Kwa muda sasa, nimekuwa nikijaribu kuitazama jumuiya ya afrika mashariki kwa lengo la kutafuta manufaa yake hususan kwa watu maskini kabisa wanaoishi kwenye vijiji vya nchi hizo, lakini lakini kwa bahati mbaya nimekosa kuyaona hayo manufaa.

............di.

Sasa EAC ndio imetuma Ujumbe Burundi kwenda "kufahamu" nini kinaendelea wakati nchi za mbali na hata jumuiya nyingine kama UN zikiwa zimeanza mapema kuchukua hatua dhidi ya mgogoro wa Burundi. Baada ya tume kurejea na kuandaa ripoti ndio viongozi ( akiwemo na mwanzilishi wa dhahama hii, Nkurunziza) wa chi wanachama watakutana ili kubaini hatua za kufanya.

Najiuliza tu, Jumuiya hii iliyoko katika ncjhi za ukanda wenye historiaya machafuko ya mara kwa mara, inacho chombo ambacho kinaheshimiwa kwamba kikitoa maamuzi ya haraka na yatatekelezwa?
EAC haina mpango wowote wa kusaidia raia wake! tuikatae na mambo yake yote.

Nani amewaambia EAC imeundwa kwa ajili ya Burundi?

EAC wenyewe ni Kenya, Uganda na Tanzania.
 
Kwani katiba iliandikwa lini na inasemaje? Si inasema Rais achaguliwe kwa kupigiwa kura na Wanachi, je Nkurunzinza amepigiwa kura na Wananchi mara ngapi? Mara moja tu - kwa hiyo ana haki ya kuchaguliwa kidemokrasia kwa mara ya pili - ndivyo katiba inavyo sema, sasa wajanja wanaingiza mambo ya ukabila chini chini kutimiza malengo/ndoto zao za kuhunda Empire - na hiki ndicho kinaendelea Burundi.
Siyo sahihi kusema kuwa Nkurunziza amechaguliwa mara moja na wananchi,awamu ya kwanza alichaguliwa na wawakilishi wa wananchi ambao pia walichaguliwa na wananchi.hii ni njia mojawapo ya chaguzi za kidemokrasia.Anachotaka Nkurunziza ni udikteta ambao unatokana na uroho wa madaraka.muonja asali hachovyi mara moja.
 
Back
Top Bottom