Kwa Watanzania waishio Marekani

Kwa Watanzania waishio Marekani

Zimebaki siku 10 [kama sijakosea] mpaka kufika ile siku ya siku...yaani ile siku ya “maandamano” dhidi ya rais Magufuli.

Maandamano ambayo kwa ufahamu wangu yamepangwa kufanyika kitaifa na kimataifa [kwa Watanzania waliopo ughaibuni].

Nakumbuka ililetwa taarifa humu kwamba kutakuwepo pia na maandamano nje ya nchi ambayo Watanzania waishio huko watashiriki.

Moja ya hizo nchi za nje ni Marekani. Watanzania waliopo Marekani watajikusanya na kwenda kuandamana huko Washington D.C.

Sina uhakika yatafanyika katika sehemu zipi huko D.C. lakini nadhani moja ya sehemu ni mbele/ nje ya ubalozi wa Tanzania na labda mbele ya White House.

Sasa ningependa kujua kama hayo maandamano ya huko Marekani bado yapo.

Kama yapo, yapo siku gani hasa. Tarehe 25 au 26?

Yatafanyikia wapi hasa? Mtaa, kiunga/ viunga?

Muda gani? Mratibu wake ni nani?

Watu watakutania wapi? Na kadhalika.

Kwa ufupi ningependa kupata taarifa zaidi.

Yakiwepo nami ntaenda na bango langu

Mzee Mwanakijiji Kiranga Bufa na wengineo wabeba boksi....nyie mnazo taarifa zaidi za hayo maandamano?

USA baby
wewe ni mnafiki
 
Yaani siku iyo mange akienda tuu wamemdaka na watapata kisingizio
 
Nyani siamini kama utaenda kuandamana, nahisi umetumwa kumdhuru Mange Kimambi
 
Back
Top Bottom