Kwa Watanzania mnaoendelea kughiribiwa na Lowassa

Kwa Watanzania mnaoendelea kughiribiwa na Lowassa

gimmy's

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2011
Posts
3,323
Reaction score
3,378
Moja kati ya technique kubwa ya EL ni kununua watu kwa makundi pamoja na media ambazo zitasaidia kupeleka ujumbe tena uliowekwa chumvi kwa wananchi kwamba yeye ni kipenzi cha Watz.

Tulianza kushuhudia hili tangu alipokua bado ana sare za kijani, makundi yaliyoghiribiwa yanafika kwa EL pasipo taarifa lakini cha kushangaza utakuta media tayari zipo eneo la tukio kabla hata haya makundi kufika zikiwa tayari zimejipanga kurusha matangazo. Tunaongopewa eti vijana wa bodaboda wemetoka Simiyu wakiendesha pikipiki kuja nyumbani kwa EL Dodoma kumuomba awanie urais, hii ni ishara kwamba hiki ni kiini macho.

Sote ni mashahidi, mkutano wa kwanza wa arusha EL alisafirisha watu kutoka kila kona ya TZ kwa gharama kubwa, mfano wapo waliokatiwa tiketi za ndege ili tu kutengeneza kiini macho kwamba yeye ni kipenzi cha watu.

Nina rafiki yangu yeye kwa mara ya kwanza kupanda ndege ilikua ni mkutano wa Arusha kwa hisani ya Mmasai. Asilimia kubwa ya mabasi yalikodiwa na EL kuelekea Arusha ili kutengeneza umati kutengeneza hiki kiini macho.

Leo tunashuhudia usafiri wowote ukikubali kuwa kwenye maandamano ya mapokezi yake mafuta ni bure, hii iwe ni bodaboda au magari.

Kweli pesa zilizopatika pasipo jasho lolote hutumika hovyo, leo tunafurahi ila hizi ni pesa zetu wenyewe zinatumika kutuzubaisha.

Kweli wanaomshabika EL aidha hufuata mkumbo au kutafuna hizi pesa zake ila swali la kwanza la kujiuliza ni wapi hizi pesa zimepatikana?
 
Katika yote ile ya makundi "kumvamia" nyumbani kwake "ghafla" ili kumshinikiza agombee urais ilivuka mipaka,lkn baadae alistuka baada ya Nape kumshauri awe makini na wapambe wanaombunia maigizo,akaacha na hakurudia tena
 
mimi nimeshawaelewa wa Tanzania...inavyoonekana hata leo hii Magufuli akihamia UKAWA tunampa nchi...yaonekana hatuna shida na record ya mgombea binafsi....wengi wanataka tu CCM itoke....Magufuli ni mgombea sahihi kabisa kosa lake kubwa ni kwamba anatokea CCM....so tatizo sio Lowassa ..tatizo ni CCM kama chama ndo watu hawakitaki
 
mimi nimeshawaelewa wa Tanzania...inavyoonekana hata leo hii Magufuli akihamia UKAWA tunampa nchi...yaonekana hatuna shida na record ya mgombea binafsi....wengi wanataka tu CCM itoke....Magufuli ni mgombea sahihi kabisa kosa lake kubwa ni kwamba anatokea CCM....so tatizo sio Lowassa ..tatizo ni CCM kama chama ndo watu hawakitaki

kama hukuwahi sikia kufilisika kimawazo basi ndio huku,
"Ni heshima kubwa kwa MUNGU kumzomea fisadi EL".
Leo yamebadilika na bla bla kibao,
tatizo ni mfumo mara tatizo ni kuiondoa CCM madarakani kwa njia yoyote.
Tusubiri October sio mbali tutaona nakutambua akili za wa tz vizur
 
Sijaona kipindi wanaCCM wana hofu kama kipindi hiki, yaani wanadiriki hata kuwashawishi wapinzani mgombea wa kumsimamisha badala ya Lowassa.
 
mm bado kusema ukweli kura yangu ni kwa lowasa tu maana bado sijaona hoja ya mashiko nimnyime kura yangu
 
Mkuu kama ndiyo hivyo basi ccm bye bye. kama anaweza kununua watu wote hao kwenye mikutano yake au kama watu wanaweza kufuata mkumbo kwenye mikutano why wasinunuliwe au kufuata mkumbo kwenye kupiga kura?
 
kama hukuwahi sikia kufilisika kimawazo basi ndio huku,
"Ni heshima kubwa kwa MUNGU kumzomea fisadi EL".
Leo yamebadilika na bla bla kibao,
tatizo ni mfumo mara tatizo ni kuiondoa CCM madarakani kwa njia yoyote.
Tusubiri October sio mbali tutaona nakutambua akili za wa tz vizur

EL haendi kokote huyo
 
Back
Top Bottom