Kwa Watanzania mnaoendelea kughiribiwa na Lowassa

Kwa Watanzania mnaoendelea kughiribiwa na Lowassa

mm bado kusema ukweli kura yangu ni kwa lowasa tu maana bado sijaona hoja ya mashiko nimnyime kura yangu
mimi kwa upande wangu agenda yangu kubwa ni change.hiki kinachoitwa sera tumekisikia for 50 years now still tupo hapa.ccm ing'oke kwanza then sera baadae
 
Yaani humu ndani tunavojadili tusikatae ushabiki. Ukisema EL alikodi watu useme na Magufuli alifanya hivohivo kwa njia tofauti. Kama matumizi wote wanatumia ila kwasababu kumsema EL ndosababu ila Mwaka huu hataiweje hamzui watz kufanya maamzi kwa kwakusema EL ni fisadi. Watz huku field wanaona. EL watu wanamkubali sana. Kabla hata hajakatwa kuna watu walikuwa wanasema EL akigombea ccm watapiga kura upinzani ubunge na udiwani ila upresda over.
 
Watu walikesha pale Arusha kwa kushushiwa mapombe ya kila aina na ng'ombe kibao kuchinjwa! we utaacha kufika!? jamaa anajua kutengeneza drama.
 
Nina hakika fedha za Lowassa ziko bank hawezi kuwa anafukia chini. Sasa kwa vile kaanza kutoa zamani na ni fedha nyingi hivyo hakuna siri tena. Sasa mbona ni ulalamishi tuu lakini hao viongozi na wapambe hawatuambii hizo fedha zake haramu ziko bank gani na ni kiwango gani? Kama wewe humtaki Lowassa usimpe kura full stop, waacheni wanaotaka kumpa wampe.
 
Binafsi nimekataa kufuata mkumbo, naiandaa kura yangu kumkwamisha fisadi el asikanyage magogoni.
Ndo option pekee uliyobaki nayo Mkuu,jitahidi uwashawishi na wengine wakuunge mkono other wise kichaka Chenu ccm kinaenda kuchomwa moto,utajificha wapi?ukiona umeshindwa kushawishi watu wa kukuunga mkono book nafasi Kabisa segerea au ukonga
 
Nina hakika fedha za Lowassa ziko bank hawezi kuwa anafukia chini. Sasa kwa vile kaanza kutoa zamani na ni fedha nyingi hivyo hakuna siri tena. Sasa mbona ni ulalamishi tuu lakini hao viongozi na wapambe hawatuambii hizo fedha zake haramu ziko bank gani na ni kiwango gani? Kama wewe humtaki Lowassa usimpe kura full stop, waacheni wanaotaka kumpa wampe.
Wakati huo huo serikali ya ccm ina kuja na magufuli eti tumpe Kura zetu sasa sijui afanye nini? Kama Lowassa ana pesa chafu why hakamatwi? Au matumizi ya fedha chafu chini ya serikali ya ccm ni ruksa? Kama anatoa rushwa kuhonga watu why wasimkamate? Kwakifupi ccm haifai si msikitini, si kanisani Wala kwa manga wa jadi
 
Jamani tuwe wakweli, Next Level angewezaje kununua watu maelfu waliojitokeza kumpokea Dar na Mbeya na Arusha na Zanzibar? Kama NL anaweza akawajaza mapesa watanzania mamilioni tulio na nia ya dhati ya kumpigia kura, hakika yeye ndio anayetufaa kuwa Raisi wetu. CCM wabinafsi mnakula nchi wenyewe na bado mnakuja mikono mitupu kuomba kura mkituhubiria injili ya kuukumbatia umaskini.
 
Sijaona kipindi wanaCCM wanahofu kama kipindi hiki yaani wanadiriki hata kuwashawishi wapinzani mgombea wa kumsimamisha badala ya Lowasa.

wait kwani october si mbali,
"El ni miongoni mwa mafisadi tuliowataja mwembe yanga ambaye amelisababishia taifa liingie kwenye hasara kubwa",Dr Slaaa.
Leo mnatuletea mtu huyo huyo kwasababu mnatuona watanzania hamnazo kwa mawazo yenu ila tutawadhihirishia kwamba kichwani tupo vizur
 
Safari hii hatudanganyiki siku zote tangu tumeanza kuwachagua CCM hawajawahi kutuambia hata siku moja kuwa mchagueni mgombea wetu kwa kuwa ni mwizi na mnyang'anyi.

Siku zote CCM wamekuwa wakituhadaa kwa kutuambia kuwa mchagueni mgombea wetu kwa kuwa ni mtu safi mpole,ni mtu wa watu,mchapa kazi,ana penda watu,muadilifu na sifa nyingi nzurinzuri na hawajawahi kusema hata siku moja kuwa mgombea wao ni mwizi.

Wananchi tunapozikubali hadaa hizo za CCM na kumchagua mgombea wao walietuaminisha kwa sifa nyingi nzuri matokeo yake tunaibiwa na hata tunapopiga kelele hakuna anayetusaidia.

Safari hii ni bora tumchague mtuhumiwa mwenye sifa mbaya ambaye wizi wake na ufisadi wake haujathibitishwa,kwa kuwa tunajua kuwa iko siku moja kama ni kweli alikuwa fisadi na kama hajaacha ufisadi wake na wizi wake atakuja kubadilika na kuacha ufisadi na wizi wake.

Kuliko kumchagua mtu ambaye tumeaminishwa kuwa ni mtu safi,ni muadilifu,mcha mungu,siyo mwizi,siyo fisadi na mchapa kazi,akienda msalani ana toa dhahabu tupu tofauti na binadamu wenzake.

Tukisha mchagua ana badilika na kuwa tofauti kabisa na jinsi tulivyoaminishwa,ana kuwa mwizi na fisadi hata kumzidi kibaka wa kila siku na hata tukipiga kelele kuwa tunaibiwa hakuna anaye tusikiliza wala kutusaidia wanasubiri uchaguzi mwingine uje waje na hadaa zingine tena.Safar hii hatudanganyiki.
 
Hata mseme nini,awe mwizi,mchawi,kibaka,malaya na vyovyote mtakavyoona inafaa kumuita,tumeishaamua kusonga naye hatuambiwi wala hatusikii,mwaka huu mtatokwa povu mpaka likauke kamwe haturudi nyuma!!
 
Hata mseme nini,awe mwizi,mchawi,kibaka,malaya na vyovyote mtakavyoona inafaa kumuita,tumeishaamua kusonga naye hatuambiwi wala hatusikii,mwaka huu mtatokwa povu mpaka likauke kamwe haturudi nyuma!!

Sio kwa tz hii ninayoifaham na kwa EL,ni vema mkapunguza munkari kwani magogoni EL ataendelea kufika matembezini kusalimia lakini kama raisi hili sahau,nasema mpunguze munkari kwani msipokua makini mnaweza mkakimbilia msituni baada ya uchaguzi kwani watz si wajinga kiasi hicho
 
Tumetapeliwa zaidi ya miaka 50 na bado hashtuki. Mtu mwingine anazoelea kunyanyaswa hadi anaufanya kuwa sehemu ya utaratibu wake wa kawaida wa maisha. HII NI ROHO kabisa. Roho ya ulimbukeni. Nendeni kwa viongozi wa dini mkaombewe. Hii sio kawaida, kuishabikia ccm karne hii lazima ujitoe ufahamu.
 
Nina hakika fedha za Lowassa ziko bank hawezi kuwa anafukia chini. Sasa kwa vile kaanza kutoa zamani na ni fedha nyingi hivyo hakuna siri tena. Sasa mbona ni ulalamishi tuu lakini hao viongozi na wapambe hawatuambii hizo fedha zake haramu ziko bank gani na ni kiwango gani? Kama wewe humtaki Lowassa usimpe kura full stop, waacheni wanaotaka kumpa wampe.

Sasa bosi mbona kama unakasirika tena
 
Nakusapoti kabisaa.haya madude yakishachaguliwa hutusahau kabisa.ukiwaambia escrow ni pesa ya nchi watakupuuza na kukwambia ni ya mtu binafsi.ukiambiwa pesa za rada unaambiwa utaratibu ulifuatwa.chengi ya rada tutanunua madawati kwa ajili ya wanafunzi.hata hivyo hadi leo maelfu ya wanafunzi wanakalia mawe nakuandikia kwenye meza za asili(mapaja yao)huku waheshimiwa wakitafuna
.tumechoka.CCM iondoke ,ikae pembeni au iende makumbusho.
 
Kwahiyo unashauri nn ? Mm ni bodaboda mtu wa magufuli akaja kuniomba niwepo kwenye msafara wa kumppkea na akasema nitakupa Lita 2 za mafuta na book 10. Kwahiyo tuzikatae ? Mbona kwenye harusi tunaombwa na tunafanya hivyo tena wakat mwingine tunajitolea
 
hawajitambui hao na kura yangu haipati na ukoo mzima hizi fedha atazirudshaje
 
Mimi nashauri mjiulize kuwa hao marafiki zake wana maslahii gani kwa Tanzania kwamba watoe hela hovyohovyo? Kama kweli wanawapenda watanzania kwanini wasizitumie hizo hela kuchimba visima,kupeleka dawa kwenye mahospitali, kusaidia watoto yatima,wajane,wazee na walemavu na badala yake fedha hizo zinatumika kwenye madereva bodaboda na harakati za kutaka mtu achukue urais? Hapo ni kwamba wanataka kuchukua nchi ili kujinufaisha kwa kujimilikisha rasilimali za nchi.

Na wanafahamu kuwa ukifadhiliwa unakuwa mtumwa kwa mfadhili wako hivyo wakimuweka rais wao maana yake huyo rais atafanya kila atakaloelekezwa na hao wafadhili. Hapo ndugu zanguni ni kwamba tutakuwa masikini kuliko tulivyo sasa. Maana hapatakuwa na kiti cha kumuinua mnyoonge. Rasilimali zite zitakuwa ziko kwenye mikono ya matajiri wachache na masikni watakuea wengi sana. Kazi kwenu nyinyi mnaocheza ngoma msiyoijua. Jiulizeni kuna hela ya bure duniani? Hakuna anayetoa hela bila ya kuwa na mkakati wa kuirudisha.

Hata anaehonga anajua kuwa atarudusha kwa kumpata anayemuhonga. Siku zote hakuna urafiki baina ya tajiri na masikini. Tajiri huwa anawatumia masikini kufanikisha miradi yake itakayomletea utajiri zaidi yeye na huku akimuacha masikini kuwa maskini zaidi ili aweze kumtawala zaidi na kumnyonya zaidi ili yeye azidi kuwa tajiri zaidi.
 
Nilifikiri ccm itajivua gamba baada ya lowassa kujitoa lakini baada ya kusikia change aka nyoka wa makengeza jina lake limepitishwa na wanaojinasibu eti lowassa ni fisadi mpaka sasa ccm basi mimi kura yangu na familia yangu ni ukawa hata kama mgombea ni nguruwe nitampigia kura hawa ccm wameniudhi sana namhurumia sana magufuri credbility yake inaenda kuchafuliwa na maccm atakaposhindwa oct 25

NB: Usijisumbue kunishawishi nibadili msimamo unatwanga maji kwenye kinu
 
mimi nimeshawaelewa wa Tanzania...inavyoonekana hata leo hii Magufuli akihamia UKAWA tunampa nchi...yaonekana hatuna shida na record ya mgombea binafsi....wengi wanataka tu CCM itoke....Magufuli ni mgombea sahihi kabisa kosa lake kubwa ni kwamba anatokea CCM....so tatizo sio Lowassa ..tatizo ni CCM kama chama ndo watu hawakitaki

Tumefika mbali aisee
 
Back
Top Bottom