Kwa wapenzi wa documentaries



Unaonekana hujui tofauti ya documentary na conspiracy theory. Documentary ni filamu ambayo inaongelea mambo ambayo sio hadithi (non-fiction) ili kuhifadhi historia au kuelimisha. Conspiracy theory ni pendekezo (explanatory proposition) kuwa mtu au kikundi cha watu fulani wamepanga na kutekeleza kwa siri mpango haramu ambao umesababisha madhara.

Conspiracy theory inaweza kuwa katika mfumo wa kitabu, documentary n.k. Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa conspiracy theory ikiwa kwenye mfumo wa kitabu hakitaitwa kitabu? Sababu ulizotoa hapo juu kuwa eti documentary za conspiracy theory huwa hazionyeshwi kwenye TV ni upuuzi kwa sababu mimi nishaziona nyingi tu mfano kifo cha Rais JFK. Si kila documentary lazima ionyeshwe kwenye TV.

Documentary pekee ya Michael Moore ambayo unaweza kusema kuwa ni conspiracy theory labda Fahrenheit 9/11 lakini nyingine zote ( nimeziona zoote) ni factual wala hakuna conspiracy yoyote.
 

Naweza kuipataje hii Darwin's nightmare?
 

Nimeangalia documentary ya mungiki ni mshkaj Wa bbc yaani wamepotray ujinga wote waliokua wanatuhumiwa mungiki mpaka utaona huruma
 
documentary nyingine zenye kuvutia na kuelimisha ni "cry freetown"-inaelezea vita iliotokea sierra leone mji wa freetown kiundani zaidi.
Nyingine ni "seal team six,the raid on Osama bin laden",hii nadhani iko clear on what its about
 

mkuu umetisha, mm napenda sana za sayansi na dini pia....apo juu nmeangalia kama tano hivyi, ni nzuri kwa kweli
 
kuna moja ya wacanada inaitwa major structure bt sina uwakika na jina, inahusu wakana kuchimba mchanga na kutengeneza mafuta kwa kiwango kikubwa.
 
hii niliwahi iona, zile ishu hata hapa zinaeza kutokea. niliona nyingine zina husu civil war huko sierra leone, ukiziona lazima ufreeze.

Hiyo inaitwa cry in free town iko powa sana and very intrested documentary +killing in Darfur
 
mkuu umetisha, mm napenda sana za sayansi na dini pia....apo juu nmeangalia kama tano hivyi, ni nzuri kwa kweli

mim pia ni mpenz wa documentaries ila nashndwa wap pa kuzipata na kipato chang ni kidogo kuweza kulipia dstv-so naomba mtusaidie 2naweza kuzipata wap kwenye form ya DVD ambyo ni rahsi zaid
 
mim pia ni mpenz wa documentaries ila nashndwa wap pa kuzipata na kipato chang ni kidogo kuweza kulipia dstv-so naomba mtusaidie 2naweza kuzipata wap kwenye form ya DVD ambyo ni rahsi zaid

Mkuu nimefurahi kujua kuwa na wewe ni mpenzi wa Documentaries humu JF. Mimi huwa na-download kutoka kwenye mtandao kwa kutumia torrents kama kickass torrents, torrent reactor, torrent room n.k ila inabidi uwe na software ya kuweza ku-download hizo torrents mfano Vuze, Aris n.k.
 

Mkuu kama unakubali kuwa farenheit 9/11 ni conspiracy ndio ilikuwa mantiki ya posti yangu ya mwanzo, kuwa baadhi ya ulizotaja hazina hadhi ya kuitwa documentary , lakini ulibisha kwa sababu unazozijua wewe.

Asante kwa kuniita mpuuzi lakini narudia tena documentary nyingi huwa zina reliable sources hasa news networks , Tv etc , kwa mfano kifo cha Jfk kimeelezwa kwenye filamu kadhaa nyingi kati yao ni conspiracy lakini hutakuta zinakuwa aired , zenyewe hutokea mitaani katika mifumo ya Dvd na haitamaye zinaingia kwenye mitandao kuwa shared , documentary si lazima ziwe katika mfumo wa video , kuna za audio pia .
 

Mkuu kwanza na-apologise kwa kutumia neno upuuzi. Halikuwa neno zuri kutumia kwenye mjadala. Lakini inaonekana bado mgumu kuelewa. Unapata wapi mantiki kuwa documentary zinazohusu conspiracy theory hazina hadhi ya kuitwa documentary? Sikutaka kuandika mengi lakini naona inabidi.

1. Kwanza sijakubali kuwa Fahrenheit 9/11 ni ya conspiracy theory. Maana yangu ilikuwa kwamba kuna baadhi ya vitu ( mfano Moore aliposema kuwa ndugu wa Osama waliruhusiwa kuondoka USA baada ya 9/11 wakati anga la US lilikuwa limefungwa ilikuwa ni kwa sababu ya uhusiano wa kibiashara kati yao na familia ya Bush) unaweza kusema kuwa ni conspiracy theory. Lakini mambo mengine mengi kwenye documentary hiyo ni ya kweli wala hayahitaji mtu kufikiri mara mbili.

2. Kwako wewe news networks pekee ndio reliable source? Je, waathirika wa tukio, watu waliokuwepo kwenye tukio, vyombo vya usalama n.k. sio reliable source?

3. Documentary kutokuonyeshwa kwenye TV ni suala la aidha sera za TV au kibiashara. Si lazima TV ionyeshe kila documentary na pia si kila anayetengeneza Documentary anataka ionyeshwe kwenye TV. Kwa taarifa yako Documentaries zote za Michael Moore huwa zinaonyeshwa kwenye Theatres kama movies za kawaida halafu ndio anatoa kwenye DVD. Kusema kuwa isipoonyeshwa kwenye TV sio documentary ni upotoshaji mkubwa.

4.Narudia tena kuwa documentary ambazo zina conspiracy theories huwa zinaonyeshwa kwenye TV. Mimi binafsi nimeshaziona nyingi tu mfano ni kama niliotoa hapo juu wa Killing JFK (kuhusu kama Mafia walihusika na kifo cha Rais JFK) nyingine ni Hoffa (kuhusu kama Mafia walimteka na kumuua James Hoffa), The Bermuda Triangle, Crop Cycles n.k.

5. Documentary kuwa katika audio sio ishu kwa sababu sifa inabaki kuwa ile ile kwamba ni documentary, by the way kila anayeingia kwenye hii thread anajua kuwa kinachuzungumziwa hapa ni DOCUMENTARY FILM.

6. Mwisho naomba unitajie kutoka kwenye orodha yangu Documentaries ambazo unafikiri zina conspiracy theories, maana umekuwa ukisema tu "baadhi ya ulizozitaja" bila ya wewe kuzitaja.

Asante.
 
kuna nyingine inaitwa taxi to the dark side. inahusu dereva taxi huko afghanistani aliyeshukiwa ni gaidi na mwishowe kuuwawa. inaelezea aina mbalimbali za mateso ambayo hutumika kucrack washukiwa na pia wanaonyesha na guantanamo. ni documentary inayosikitisha sana.
 

Thanx kwa apology !!! ni uungwana kubadilishana mawazo bila kukwaruzana , that's great!

Mkuu kuna tofauti ndogo sana kati (thin line between ) ya documentary na conspiracy, ingawa zinafafana sana namna ya kuleta ujumbe.,nadhani hata uienda wikipedia wamefafanua!. lengo la documentary ni kuleta uelewa wa wewe unayesikiliza au kuangalia kipindi hicho, ulike conspiracy lengo lake ni kukuchagulia upande wewe msikilizaji kwa kukupa taarifa za upande fulani, ndio maana nikakwambia kuwa mara nyingi huwa haziwi aired kwa kuwa contents zake ni uchochezi dhidi ya serikali au kikundi fulani.

Umekuwa ukirudia kuwa umeangalia documentary nyingi ,mi nasema nimeziona za kutosha !! naepuka kukwambia nimeziona ngapi sababu sikumbuki na wingi unaosemea siujui unatumia kipimo gani.katika list yako, smart guys (Enron) ni moja ya documentary ,ile ya farenheit 9/11 ni conspiracy.

Kifo cha rais JFK ni moja vifo vyenye conspiracy nyingi sana , kina husishwa na mafia , kuna wenye kuhusisha na russia's KGB , inner cycle haters , womenising habits za JFK .n.k, nimeangalia filamu za kutosha kuhusiana na kifo cha rais huyo ,mind you siku kennedy anauwawa body guard alikua Clinton Hill, maelezo yake ukisikiliza utagundua kifo kilichotokana na just one hatter.

next time chunguza unachoangalia !! ukiona narrator anaelemea upande fulani na wachangiaji wako upande wa msimuliaji jua umenasa kwenye mtego wa conspiracy, It's a bit tricky kufahamu hilo, kwa kuwa nao ni maexpert wa kufanya idea zao kuwa karibu na ukweli,
 
mim pia ni mpenz wa documentaries ila nashndwa wap pa kuzipata na kipato chang ni kidogo kuweza kulipia dstv-so naomba mtusaidie 2naweza kuzipata wap kwenye form ya DVD ambyo ni rahsi zaid

Mkuu kuongezea alivyo kushauri mdau mmoja ,njia rahisi kupata hiyo makitu ni torrents , au youtube , lakini nzuri zaidi ni torrents , sababu pale movies nyingi ni dvd rips , quality ya video na audio ni safi, for some reason pendelea kudownload zenye best quality ili uweze kuinjoy pure sounds na picture na pia utaangalia between different sources ie tv bila kuhisi tofauti.
kama unatumia simu za android, install program inaitwa Lt torrent kutoka playstore, then tafuta 16gb sd card weka kweye simu,kisha search keywords za documentary unayoitafuta, you are good to go, hakikisha una data plan ya kutosha ,prefferebly voda unlimited, as haya makitu yanakula sana bytes.

waweza kutumia kompyuta pia na kudownload kama alivyushauri mdau
 
nilukuwa natafuta hiyo documentary ya enron nimeikosa ila nimepata kitabu, kiko bomba sana
 
kuna nyingine inaitwalast train home. inahusu shida wanazopata wafanyakazi wa kuhamahama nchini china. wachina wanamaisha tight sana.
 

Hiyo nimewahikuisikia kwa njia ya audio tu kutoka bbc/podcast , sikuwahi kudhani kama kuna video yake , nitaitafuta. Hata mimi ilinisikitisha sana kifo cha "aliwar "taxi driver.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…