Kwa waliozaa kabla ya ndoa


Umenena vyema kuna post ya Husninyo hapo ameeleza hili
 
Last edited by a moderator:
Ingekuwawewe mtoro ungeipendahii mpwa
 
Niliwahi kuishi na bro wangu pale Arusha miaka ya 2006, yeye kabla ya kufunga ndoa na mkewe tayari alikwishazaa nje watoto wa3, wakike yupo kateshi, wakike yupo mbulu na wakiume yupo kisongo ila hakuwa amemwambia mkewe.
Alipoamua kufunga ndoa mke wake wa sasa aliyezaa naye watoto wawili aliamua kutest zali la kumweleza mkewe na kwenda kumchukua yule mtoto wa kiume pale kisongo akiwa darasa la nne na kuja kuishi naye ngusero akisoma s/m sokoni one.
Maskini mtoto alinyanyaswa na kuteswa na yule shemeji mpaka huruma, akampa marufuku mama yake kuja kumwona pale nyumbani, shuleni wala kanisani au hata kuongea kwa simu.
Mtoto akawa anajaribu kutoroka kwenda kwa mama yake anakaa huko wk 2 basi akirudi pale home atasemwa na kusingiziwa kuwa katoka kuchukua madawa ya uchawi ya kumuua yule shemeji ili mama yake arudie ndoa na yule mtoto atanyolewa nywele zote za kichwani, kwapani mpaka matako.ni ili atolewe huo uchawi.
Hayo yalikuwa yanafanywa na shem bila bro kujua na kale katoto kalikuwa hakasemi ila alipokuja kugundua akaamua kumhamisha shule na kumpeleka kwa bibi yake huko songea ndo ikawa pona ya yule mtoto.
Baadhi ya wanawake ni makatili sana kwa watoto ambao sio wao na akipata mwanya wa kumfanya atakacho anamfanya kweli huyo mtoto.
 
Huyo mke wako ana visa kupitiliza.

Kwanini usimrudishe huyo mtoto kwa mama yake ukatoa hela ya matumizi huko?!Kuna sababu yoyote ya msingi inayozuia mtoto kuishi na mama yake?! Mwanzo kabla hujaoa kulikuwa na utaratibu gani kuhusiana na malezi ya mtoto?! Ni sababu zipi zilipelekea umchukue mtoto baada ya kuoa na sio kabla?! Mke wako anam-treat vipi huyo mtoto?!

Anaenyanyaswa KWELI hapo ni mama mtoto na mtoto wala sio huyo mkeo. Fanya umtendee haki mtoto na mama yake pia. Usisombwe na ubinafsi + visa vya mkeo ambavyo vinaonekana havina logic.
 
....wala mtoto hatakiwi kwenda kwake maana atamjaza ujinga.

Kweli kila mtu ana akili na roho ya kipekee.

Kwahiyo wewe kwa akili yako una uhakika kwamba huyo mkeo ndo atakuwa na positive effect+influence na mtoto kuliko mama yake mzazi. Nyie ndo huangalia watoto wakinyanyaswa kwenye himaya zenu day in day out kisa ulimbukeni wa mapenzi.
 

Unajuwa hizi kesi hazifanani kama mwanamke uliyezaa naye hajaolewa na mwanaume mwingine na angalau anayamudu maisha yake mpe mtoto akae naye wewe utatoa matunzo, ni uselfish uliopitiliza mtoto kukosa mapenzi ya wazazi wake, inabidi ni lazima mmoja wenu akae na mtoto, binafsi siwezi kukubali mama yangu kulea watoto wangu, alishanizaa nimekuwa kazi yake imekwisha kama ng wajukuu watamtembelea weekend na kuspend naye likizo inatosha na yeye wale good time na mume wake siku zao zilizobaki.
 
Umenena vyema kuna post ya Husninyo hapo ameeleza hili


Nimeiona ila nikakudondokea wewe....
Husninyo siku hizi hanisalimii vizuri aisee....lol!!

Ndoa yenye mtoto aliyezaliwa kabla ni changamoto sana na watu wasipokuwa waangalifu wanabwaga manyanga!

Kuna jamaa yangu alilazimika kuzuiwa kwenda kwa mzazi mwenzake na kumleta mtoto nyumbani kwa sababu walikuwa wanatumia hiyo nafasi kumsalimia mtoto na mama wa mtoto....(wazazi wengine wanakuwa mabazazi)!!
 

Pdidy katika ubora wake.
 
Asante my dear.

Huwa nashangaa sana mtu yeyote anaemnyang'anya mzazi mwenzie mtoto alafu anaenda kumtupa sijui kwa bibi au shangazi yake. What for?! Kama mtu hawezi kuishi na mtoto bila migogoro (mf huyu jamaa mtoa mada) aache mtoto aishi na mzazi mwenzie. Maana wanapofikiri wanamkomoa mzazi mwenza wanamkomoa mtoto zaidi wakati hakuomba kuwa kwenye situation aliyopo.
 

Hakuna kanuni hata moja Matola. Kila familia ni nchi huru hata ikiwa ndogo kama Vatican. Jambo la msingi ni kwa wahusika wote kuwekeana utaratibu ambao unaeleweka na usio na mambo ya kipuuzi.

Mke akihisi wanatumia huo mwanya itakuwa hatari kwa mtoto, ndoa au vyote. Inahitajika akili na busara tele!
 
Last edited by a moderator:

Hii itawezakana endapo huyo mama wa mtoto hayuko kwenye ndoa. Endapo yuko kwenye ndoa hali inaweza kuwa tofauti.

Mshikaji wangu alimchukua mtoto baada ya ugomvi na mkewe, ila baadaye walishindwa na kumrudisha mtoto kwa mama. Huyo mama naye aliolewa na ikabidi mtoto abaki na bibi.

Kwa ufupi ni maisha ambayo yana changamoto nyingi sana. Hakuna njia rahisi au ya mkato.
 
Hapo hakuna nafasi kwa ex ... No matter what.. Mwambie kuja home haiwezekani
 
 

Over my deadbody mama yangu hawezi kulea mtoto wangu jukumu lake alishamaliza.

Kama mtoto yuko under age abaki na mama yake na hata akiwa over age ruksa pia historia inaonesha kwenye situationa kama hii tena mtoto wenyewe utakuta ni mmoja aachwe amfariji mama yake, Baba unaclear bill tu. Umeoa mwanamke mwingine zaeni wa kwenu kama unadhani mpaka kuitwa Baba au mama au fulani ni mchezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…