Administer
JF-Expert Member
- Feb 9, 2020
- 930
- 1,408
Kwa uchache tu Mwambe,Sumaye na wengine mliotuaminisha kwamba mnahama CHADEMA kwenda CCM kwa sababu mnatafuta DEMOKRASIA na DEMOKRASIA hiyo haipo CHADEMA ipo CCM ,mimi nawakumbusha tu sasa ni wakati wenu wakuchukua fomu ya kugombea urais kupitia CCM wakati ndiyo huo msisubiri muda unayoyoma.Mwambe na Sumaye kule CHADEMA mlikuwa mnagombea nafasi za chini Uenyekiti wa chama ngazi ya Kanda na Taifa mkashindwa hatimaye mkatimka.Sasa huku kuna nafasi kubwa ya urais tumieni hiyo fursa kutimiza ndoto zenu.Nawatakia kila la kheri ktk kupigania DEMOKRASIA ya kweli