Kwa wale vijana tuliosoma sekondari Dar miaka ya nyuma hebu tukutane hapa

Bata batani

JF-Expert Member
Nov 11, 2011
3,182
3,547
Kwa wale vijana tuliosoma secondary hapa dar hebu tukutane hapa na kujikumbushia haya yafuatayo MIAKA 95 HADI 2005
KIPINDI HIKI

1.Shule ya azania , pugu na tambaza zilikuwa zinajulikana kwa fujo na vurugu pamoja na kuwazingua makonda wa daladala.

2.Shule ya makongo na jitegemee zilikuwa ni shule za jeshi ila zilipata umaarufu kwa kutoa wasanii wa bongo fleva, movie na wachezaji mpira.

3.St.Arthony na loyola zilijulikana kama shule za watoto wa kishua zenye kufaulishaa.

4.Perfect vision, st.Methew , green acreas na happy skilful zilijulikana kwa feki coz kuna miaka waliwahi kufutiwa matokeo.

5.Airwing secondary ilijulikana kama shule ya mpera mpera na ukakamavu

6.Zanaki na jagwani zilijulikana umaarufu wa zinaongoza kwa umalaya na usistaa duu kwa sana.

7.Forodhani ilijulikana kwa vijana wengi kuwa mabishoo
Na masistaa duu

8.Kisutu pia ilijulikana kwa masistaa duu

9.Pia kulikuwa na shule kama kibasila, benjamini, dar es salaam,juhudi hizi zilikuwa zinaitwa shule za wastarabu

10.Lakini yote tisa kumi tukisikia mtu anasoma shule zifuatazo ilboru, mzumbe, tabora boys, tabora girls, msalato,ifunda, iyunga, kibaha boys basi mtaani alikuwa anaogopeka na anaheshimika kwa sababu kule ilikuwaga ni kipaji maalumu wenye akili sana ndo walikuwa wanaendaa.

Haya jamani hebu tukumbushane kidogo yaliyojiri wakati ulee
 
Ungeweka mpaka wa miaka mkuu, maana unapoitaja benjamin hapo nahisi ilikuwa ni mpakani mwa waliosoma zamani na waliosoma miaka ya karibuni, huenda usipotaja miaka watakuja watoto waelezee humu experience za mwaka 2010 kumaliza form four, wakati huo shule kama forodhani ilisharudishiwa kanisa la r.c zamani sana,
 
Kweli kila Mmoja ana zamani yake

Nilipoona Airwing, Green Acres, Loyola, St Anthony nikajua hii zamani inayoongelewa hapa si Yangu!
 
Ebu weka limit ya miaka unayoizungumzia tuanze kutiririka.
Ila namba moja nimeipenda
 
Back
Top Bottom