Kwa vyovyote vile Azimio la Arusha lisingependwa na halitapendwa na viongozi wa kimichongo michongo

Wolle Melkas Fernando

JF-Expert Member
May 4, 2016
218
297
Lengo kubwa la Azimio la Arusha lilikuwa ni kuweka misingi na itikadi ya Taifa iliyojikita kwenye "Ujamaa na Kujitegemea". Kufanya Kazi Kwa Bidii ndio kilikuwa kitovu cha itikadi hii ya Ujamaa na Kujitegemea.

Waasisi wa itikadi ya 'Ujamaa na Kujitegemea' wakiongozwa na Mwanafalsafa hii Hayati Mwal. Julius K. Nyerere walikusudia kulinda Uhuru wa Taifa na watu wake katika nyanja zote; kisiasa, Kiuchumi na Kijamii japo Uhuru wa kujiamria mambo yetu wenyewe ulikuwa tayari umeshapatikana mwaka 1961 na Azimio la Arusha lilifanyika 1967 lakini tulihitaji Uhuru wa Kujitegemea na ndio maana itikadi hii ya Ujamaa na Kujitegemea ilisimikwa kama mwongozo wa Taifa.

Msingi wa Azimio la Arusha ulikuwa kupambana na aina zote za Dhulma, unyonyaji, dharau, unyonge na kutwezwa utu yaani kutothaminiwa na zaidi kupambana kuondoa matabaka Kati ya walio nacho na wasionacho (haves & have not). Yote haya yalilengwa kutekelezwa kwa kuipa serikali nguvu ya kumiliki vyanzo vikuu vya Kiuchumi ili kusiwepo na mfanyabiashara au mtu yeyote wa kuiweka serikali mfukoni yaani mtu kuwa na jeuri zaidi ya serikali ndio suala la utaifishaji lilipoanzia.

Mwalimu Nyerere alifahamu kwamba tusipokuwa huru Kiuchumi tukategemea misaada na mikopo kutoka ughaibuni hatutakuwa huru ni sambamba na kauli ya aliyewahi kuwa Rais wa Burkina Faso Thomas Sankara, aliyewahi kuwa Rais wa Burkina Faso aliposema, "He who feeds You Controls You" yaani anayekulisha ndiye anayekutawala . Kwahiyo kwa kutambua hilo Azimio la Arusha, lilisisitiza wananchi kufanya Kazi Kwa Bidii katika uzalishaji.

Azimio la Arusha lilikuwa mwiba wenye ncha Kali sana kwa kiongozi yeyote mwenye nia ya kutaka kujipatia utajiri kwa kutumia cheo au kuhodhi Mali za umma. Azimio halikuwa rafiki kabisa kwa watu wa namna hii kutokana na miiko ya uongozi iliyowekwa katika Azimio la Arusha ambayo kwa baadhi ni pamoja na;
Cheo ni Dhamana sitakitumia Cheo changu kwa manufaa binafsi
Rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa. Na miiko mingine mingi tu.

Azimio lililenga kujenga misingi imara ya uongozi bora ambao ni Moja ya nguzo kuu 4 za Maendeleo yaani Ardhi, Watu, Siasa safi na uongozi bora. Mwalimu alitaka Uongozi uwe ni Kazi ya kujitolea kama ya sadaka sio ya kufaidika kama unataka kufaidika fanya biashara sio kugombea na kutaka Uongozi kwa nguvu zote.

Mambo yalianza kunoga pale Azimio la Arusha lilipoanza kutekelezwa lakini kwenye msafara wa Mamba na Kenge nao huwa hawakosi wanaliunga humohumo kwenye msafara na hapo viongozi wa kimichongo michongo walipoanza kujitokeza kimya kimya na kuhujumu Azimio la Arusha. (itaendelea)
IMG_20220509_090958_794.jpg
IMG_20220509_091024_435.jpg
 
Azimio la Arusha ndo limetuletea umasikini, matabaka kwenye Jamii huwezi yakwepa.
Lengo kuu la ujamaa ni kuwafanya watu wawe masikini Ili iwe rahisi kuwatawala.
Watu walipata mali zao toka enzi ya mkoloni tena kihalali kabisa wala mkoloni hakuwa na shida na mwafrika kumiliki mali, Nyerere alifanya makosa makubwa Sana kutaifisha mali za watu kwa kuwalazimisha watz wote wawe level moja haiwezikani ulingane watu level moja ya maisha wakati sio wapambanaji.
 
Kiukweli Azimio la Arusha limerudisha nyuma sana hii Nchi, baada ya azimio tuliingia kwenye vita vya kagera.Nchi ikaanguka kiuchumi. Ndipo tukakubali masharti ya SAP. Azimio limewafanya watanzania kuto jiamini. Azimio limesababisha hata maslahi ya watumishi wa umma yasiangaliwe.kazi ikawa wito. Lakini bado wapo wengi walitumia Mwanya wakutoulizwa kuiibia Nchi. Kenya waliingia ubebapari mapema wakatupita kiuchumi, Tanzania ilikua na private schools, hospitals n.k lakini zilitaifishwa,bila hata kuona uhalali wa umiliki wake. Jiulize investment iliyofanywa na St. Ugastine katika elimu, hospitali za kcmc,Bugando, Hydom, Peramiho nk. Msaada wake kwa wananchi. Kama tungeendelea na Azimio la Arusha hii Nchi ingekuwa maskini kuliko.
 
Kiukweli Azimio la Arusha limerudisha nyuma sana hii Nchi, baada ya azimio tuliingia kwenye vita vya kagera.Nchi ikaanguka kiuchumi. Ndipo tukakubali masharti ya SAP. Azimio limewafanya watanzania kuto jiamini. Azimio limesababisha hata maslahi ya watumishi wa umma yasiangaliwe.kazi ikawa wito. Lakini bado wapo wengi walitumia Mwanya wakutoulizwa kuiibia Nchi. Kenya waliingia ubebapari mapema wakatupita kiuchumi, Tanzania ilikua na private schools, hospitals n.k lakini zilitaifishwa,bila hata kuona uhalali wa umiliki wake. Jiulize investment iliyofanywa na St. Ugastine katika elimu, hospitali za kcmc,Bugando, Hydom, Peramiho nk. Msaada wake kwa wananchi. Kama tungeendelea na Azimio la Arusha hii Nchi ingekuwa maskini kuliko.
Azimio la Arusha lilikuwa na nia njema sana, lililenga kukomesha masuala ya ufisadi, kuondoa matabaka (classes) kuweka mgawanyo sawa wa lasirimali zote, kukomesha matumizi mabaya ya ofisi za umma. Tatizo ni pale tu walipojitokeza wenye tamaa na kuanza kuharibu miongozo ya Azimio lenyewe.
 
Azimio la Arusha ndo limetuletea umasikini, matabaka kwenye Jamii huwezi yakwepa.
Matabaka kwako yapi ni sawa (Gap ya walionacho na wasionacho) Je ni sawa kwa sasa kwa Security ya Dunia kwamba Asilimia 99.99 ya Utajiri ipo kwa asilimilia chini ya 1 ya watu ? Is that stable ?
Lengo kuu la ujamaa ni kuwafanya watu wawe masikini Ili iwe rahisi kuwatawala.
Masikini ndio rahisi kutawalika ? Kwamba people with nothing to loose hawana uhakika wala sababu ya kuishi ndio wanatawalika
Watu walipata mali zao toka enzi ya mkoloni tena kihalali kabisa wala mkoloni hakuwa na shida na mwafrika kumiliki mali,
Nyerere alisema watu wasimiliki mali ? Au aliweka misingi na Katazo la viongozi kumiliki hizo mali; Kwa maneno yake kama ukiwa na mali nyingi na unataka uongozi tunakuuliza ulizipataje ili na sisi utufundishe jinsi ya kupata..., Ukiongelea hao wakoloni hata kwao huko waulize mfumo wa Feudalism na Aristocracy kama hawakuuondoa
Nyerere alifanya makosa makubwa Sana kutaifisha mali za watu kwa kuwalazimisha watz wote wawe level moja haiwezikani ulingane watu level moja ya maisha wakati sio wapambanaji.
Tuchukue sasa hivi unadhani hao wabunge wanasiasa na walamba asali ni wapambanaji kuliko wale peasants waliopo vijijini? Kwamba ni wazembe ? Azimio la Arusha lilikuwa ni kuweka Katazo / Sheria za Viongozi wa wa CCM (sio wewe wala nani; ukitaka kupingana na hizo sheria maadili yao / usichukue ongozi) Wewe kama mdau wa kawaida all the best
 
Back
Top Bottom