Kwa uzungu huu na ukaidi wa viongozi wa simba kazi kesho tunayo

njaakalihatari

JF-Expert Member
Feb 12, 2019
4,084
8,663
sijajua ni uzembe wa meneja wa team, team haina watu wa security au makocha wazungu ndiyo pendeleo lao ama nini lakini hili la mashabiki kuangalia mazoezi ya simba linafikirisha sana.

Ni ujeuri na ukaidi tu, wanajua kesho tukifungwa watamtuma Ahmed Ally apooze watu na tararira mbili tatu maisha yaendelee ila uongozi mnachofanya ni ukadi wa kishamba sana.

Hata kama ni uzungu basi mmewazidi wazungu wenyewe sababu wao mazoezi yao ni mara chache sana kuhudhuriwa na mashabiki.

Mlisema mnaanza kujenga ukuta kwa zile milioni 150 zilizochangwa au MMEZILA? kama plan haijaanza si mngeenda hata kule boko mkodi uwanja? gharama ya kukodi uwanja inalingana na gharama ya kufungwa na utopolo kwa kukaribisha mimacho ya kila aina mazoezini?

Hapo bado hujasoma gazetini sasa"KOCHA ZORAN ALIKUWA MKALI KWA MABEKI WA PEMBENI WAKICHELEWA KUPANDA KWA KASI ALIKUWA ANAWATAKA WASHAMBULIAJI KUACHIA MPIRA MAPEMA, KIKOSI CHAKE KILIKUWA 4-4-2 HUKU MBELE AKIWA SERIUS SANA NA KIYOMBO NA PHIRI".

Hata kama hamtarogwa basi hao waandishi ni wachawi tosha mbona utopolo na ujinga wao wote mazoezi yao hata makanjanja hayajuagi kinachoendelea?
 
Mechi na Yanga sio kubwa kama fainali au nusu fainali ya klabu bingwa Afrika, hiyo ndio target ya Simba SC, au kombe la Shirikisho, usiwakuze hao waache wadumae peke yao.

Wacha mashabiki wakacheki mazoezi jumamosi tunaingiza timu uwanjani maisha yanaendelea tukiwaza mechi yetu ya kwanza na Wamalawi.
 
Mechi na Yanga sio kubwa kama fainali au nusu fainali ya klabu bingwa Afrika, hiyo ndio target ya Simba SC, au kombe la Shirikisho, usiwakuze hao waache wadumae peke yao.

Wacha mashabiki wakacheki mazoezi jumamosi tunaingiza timu uwanjani maisha yanaendelea tukiwaza mechi yetu ya kwanza na wamalawi.

Utazani mmewahi kunyanyua kwapa
 
Nadhani haya mambo kulazimisha iwe kama zamani ni ngumu kwa sasa, yanaondoka taratibu yenyewe.

Hata kipindi kile kuna watu walitupa lawama sana kitendo cha Simba kuacha kwenda kuweka Kambi nje ya Dar es salaam inapofikia mechi ya Watani wa Jadi.
 
Taratibu mambo ya ushirikina yanabidi yaondoke si katika mpira tu bali katika mfumo wetu mzima wa maisha.
 
Mechi na Yanga sio kubwa kama fainali au nusu fainali ya klabu bingwa Afrika, hiyo ndio target ya Simba SC, au kombe la Shirikisho, usiwakuze hao waache wadumae peke yao.

Wacha mashabiki wakacheki mazoezi jumamosi tunaingiza timu uwanjani maisha yanaendelea tukiwaza mechi yetu ya kwanza na Wamalawi.
Huku ni kukata tamaa
 
Back
Top Bottom