Kwa uchafu huu wa Mbowe anapata wapi uhalali wa kuendelea kuwa kiongozi na kwenyekiti wa CHADEMA?

Kibstec

JF-Expert Member
May 21, 2016
1,205
2,339
Ebu tuanze kuwabana kwanza hawa VIONGOZI wetu wanaongoza vyama PINZANI hapo ndipo tutakapo pata uhalali wa KUINDOA CCM madarakani.

Kwanini nasema hivi? Nasema hivi nikiwa na maana ya kwamba TUMESHUHUDIA uchafu mkubwa sana wa KIONGOZI mkubwa wa CHAMA kikuu cha UPINZANI kashfa zake za kukwepa KODI zikionyeshwa wazi wazi na serikali hii.

Juzi ilikuwa BILICANAS NA LEO NI HOTEL YAKE HUKO Kilimanjaro.

Sasa tujiulize hivi...

1. Mpaka sasa anapata UHALALI upi wa kuendelea kuwa kiongozi mkubwa ndani ya chama?

2. Je, anapata uhalali upi wa kuwatetea wananchi ili hali yeye mwenyewe amekuwa mstari mkubwa kukwepa kulipa KODI ambayo ingetumika kuwaletea wananchi maendeleo?

3. What if chama chake kingefanikiwa kuongoza nchi hii asingekuwa FISADI MKUBWA?

4. Kwa sasa anapata uhalali upi wa kutoka nje na kuikosea serikali hii?

5. Kwanini ni mtu wa ndimi mbili maana tulio wengi tunakumbuka yeye ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kuiita serikali ya JK ni legelege kwenye suala la kukusanya KODI ili hali yeye mwenyewe nae alikuwa mkwepa kodi mkubwa?

MKITAKA KUINDOA CCM madarakani EBU ANZENI KUJENGA MSINGI IMARA WA NYUMBA YA HAPO UFIPA KWA KUWAONDOA HAO WOTE NDIMI MBILI, mkifanikiwa hili CCM mtaitikisa ipasavyo.
 
Nia yako kubwa ilikuwa kumtukana Mbowe.Hivi Mbowe ni Protea ??Hivi hujui.kisheria Protea inashtakiwa kama MTU sababu inajitegemea??Ina management yake??Hivi hujui anayeshtakiwa hapo ni management ya Protea na si Mbowe??Shida yako kubwa ilikuwa kutafuta eneo la kumtukana Mbowe.

Tuambie aliyefanya ufisadi kwenye zile Bilioni nane za meli mbovu??Nyumba za serikali zilizogawiwa kwa.vimada??Barabara mbovu.

Issue ya kodi ya Protea ni Management ya Protea na si Mbowe.Mbowe ni shareholder na si Manager wa Protea.
 
Hii mbinu mliyojuja nayo ya kufunga wapinzani, kuwakamata eti hawalipi kodi ni ya kizee ile mbaya. Kwenye nchi ambayo mkuu anaongoza kwa chuki na jazba ya wazi dhidi ya wapinzani hata afanyeje watu wanaona ni chuki binafsi. Kwa hiyo mnadhani watu wataamini wapinzani ni wavunja sheria sana na wanaccm ni wema sana. Basi mmechemsha na tumieni ulevi wa madaraka kuwakomoa wapinzani mkidhani mtapendwa. Kila mtu anaona huu uonevu wa dhahiri, mnajichanganya mpaka mnatoa ubunge kwa waongo, hapo mnadhani bado mtaaminika tu?
 
Hii mbinu mliyojuja nayo ya kufunga wapinzani, kuwakamata eti hawalipi kodi ni ya kizee ile mbaya. Kwenye nchi ambayo mkuu anaongoza kwa chuki na jazba ya wazi dhidi ya wapinzani hata afanyeje watu wanaona ni chuki binafsi. Kwa hiyo mnadhani watu wataamini wapinzani ni wavunja sheria
sana na wanaccm ni wema sana. Basi mmechemsha na tumieni ulevi wa madaraka kuwakomoa wapinzani mkidhani mtapendwa. Kila mtu anaona huu uonevu wa dhahiri, mnajichanganya mpaka mnatoa ubunge kwa waongo, hapo mnadhani bado mtaaminika tu?
Kwani Mbowe wakwanza kudaiwa kodi kwa staili hiyo kama anajeuri ya kukwepa kodi akiwa mpinzani je akiwa madalakani sina chama ninachotaka kama anadaiwa alipe hatutaki porojo kama anabambikiwa aende mahakamani hatutaki visingizio eti sisiemu ndio maakama mbona Ester karudishiwa ubunge ni hiyohiyo mahakama haki haiji tu inadaiwa
 
Naomba kujua wale walioipindisha na kuiozesha nchi ambao "Angel all the way from Ma-go-goni " anawaongelea ni kina nani?

Na hao wenye makaburi mazito yaliyomshinda Malaika ni kina nani?

Ukinipa majibu nitarud
 
Sasahivi sharia haifuatwi, bali kuna kukomoana hasa kuwakomoa wapinzani,

Jiulize, Nchi hii ni Sumae tu ndio kiongozi asiye andeleza mashamba yake?

Jengo la Bilcamas si lilikuwa linamilikiwa kwa shea na Mbowe ndio aliluwa na asilimia 75% kilitokea nini?

Mada yako Mfu kabisa.
Kaeni mkijua mnazidisha chuki kwa siasa zenu taka.

Mbunge wa CCM kakamatwa kwa ujangiri na masiraka 10 na kitu lakini yupo huru, LEMA na kuhamasisha UKUTA, mikutano na Maandamano ambayo yako kikatiba yuko ndani mwezi wa 3 sasa. Sharia ipi hiyo,

Wakomoeni tu lakini hamjengi
 
Nia yako kubwa ilikuwa kumtukana Mbowe.Hivi Mbowe ni Protea ??Hivi hujui.kisheria Protea inashtakiwa kama MTU sababu inajitegemea??Ina management yake??Hivi hujui anayeshtakiwa hapo ni management ya Protea na si Mbowe??Shida yako kubwa ilikuwa kutafuta eneo la kumtukana Mbowe.

Tuambie aliyefanya ufisadi kwenye zile Bilioni nane za meli mbovu??Nyumba za serikali zilizogawiwa kwa.vimada??Barabara mbovu.

Issue ya kodi ya Protea ni Management ya Protea na si Mbowe.Mbowe ni shareholder na si Manager wa Protea.
Kwa hiyo unakiri nbowe FISADI...ila unamlinganisha na FISADI mwingine...sio??
 
tofautisha kodi rent na kodi tax mbowe aliktduwa anadaiwa rent sio tax!afu hizo ni siasa za chuki jamaa anazitengeneza kutisha wapinzani tumpinge dikteta
 
Napata wasi wasi na uadililifu wa kiongozi wangu Freeman mbowe,ndiyo maana JPM anatudhalau sasa,coz kashajua madudu ya Mshika kamba. Shame on You Freeman mbowe.
Hili Bonge la neno..Jamaa alishasema hao wanaoongea sana ndio wamekopa hadi kuiua twiga bancorp..wanadaiwa madeni..anawajua vizuri sana na unafiki wao..jpm anajaribu kutulinda dhidi ya unafiki wao...ndio maana anawabana hadi mikutano yao ya propaganda kwa wananchi..kina mbowe waliitumia siasa muda mrefu kufanya biashara na kukwepa kodi..kwamba akiguswa ataichafua serikali kama alivyoanza kwenye ishu ya nhc akakutana na mkono wa chuma usiojali malalamiko ya kijinga.
 
Nia yako kubwa ilikuwa kumtukana Mbowe.Hivi Mbowe ni Protea ??Hivi hujui.kisheria Protea inashtakiwa kama MTU sababu inajitegemea??Ina management yake??Hivi hujui anayeshtakiwa hapo ni management ya Protea na si Mbowe??Shida yako kubwa ilikuwa kutafuta eneo la kumtukana Mbowe.

Tuambie aliyefanya ufisadi kwenye zile Bilioni nane za meli mbovu??Nyumba za serikali zilizogawiwa kwa.vimada??Barabara mbovu.

Issue ya kodi ya Protea ni Management ya Protea na si Mbowe.Mbowe ni shareholder na si Manager wa Protea.


Duh! Kama ndivyo basi urais na uwaziri ni taasisi mkuu. Hatutapata wa kumlalamikia kila maali. Jaribu kufikiria upya nitarudi kwa ajili yako ngoja nikasali.
 
Hizo ni propaganda tu,mbona pale llumumba mbunge alikamatwa kwa ujangili mkamficha jina,kesi haijulikani iko wapi mpka leo,pale lumumba wangapi wanakwepa kodi katika biashara zao mbona hamuwasemi,acheni majungu.
 
Nia yako kubwa ilikuwa kumtukana Mbowe.Hivi Mbowe ni Protea ??Hivi hujui.kisheria Protea inashtakiwa kama MTU sababu inajitegemea??Ina management yake??Hivi hujui anayeshtakiwa hapo ni management ya Protea na si Mbowe??Shida yako kubwa ilikuwa kutafuta eneo la kumtukana Mbowe.

Tuambie aliyefanya ufisadi kwenye zile Bilioni nane za meli mbovu??Nyumba za serikali zilizogawiwa kwa.vimada??Barabara mbovu.

Issue ya kodi ya Protea ni Management ya Protea na si Mbowe.Mbowe ni shareholder na si Manager wa Protea.
endelea kujipa moyo unajitia upofu kwakufikiri kusema management ndio hatuelewi yaana kwa akili zako za ucku na za ufipa unafikiri kuwa mmiliki anajitoa ktk sakata la wizi unabwabwaja huku ukijua fika Mbowe ndiye CEO wa Protea yaani umeonyesha ukichaa wako leo
 
Hivi Faru nanihii na Mbowe nani ni Fisadi? Sema CCM mnajitia tu upofu, mngesoma maswali ya Ulimwengu ambayo Faru alishindwa kuyajibu hadi Leo hii..... Tunajua tumekaa kimya. Kipindi hiki CCM mtatukana mnavyotaka, mko juu ya sheria
 
Back
Top Bottom