Kwa ubambe huu unao tumika bungeni, demokrasia hapa kwetu itabakia ni ndoto.

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Katika hali ya kawaida bunge letu linapashwa kuwa ndicho kielelezo cha demokrasia ya kweli hapa nchini. Lakini mambo ni tofauti; hivi sasa Spika anadiriki kuwakemea wabunge kama kwamba ni watoto wa chekechea. Kwa mfano, leo hii asubuhi, baada ya waziri mkuu kumaliza kujibu maswali ya moja kwa moja, kuna mbunge aliyeomba mwongozo wa spika akitaka kujua ni hatua zipi mbunge anaweza kuchukua, iwapo kiongozi wa ngazi ya juu kama waziri mkuu, atalidanganya bunge. Badala ya kumjibu swali lake, spika alianza kumshambulia yule mbunge, akihoji iwapo mbunge yule alikuwa na maana ya kuwa waziri mkuu ameliongopea bunge; na kuongeza kuwa kama ni hivyo aiweke kimaandishi. Ni maoni yangu kuwa huo ni ubabe tu, maana muuliza swali hakusema kuwa hali hiyo tayari imejitokeza, alichotaka kujua ni kama hali hiyo ikijitokeza mbunge anaweza kuchukua hatua gani.
 
muda ndio utakao waumbua kwani watanzania wa leo wanajua pumba ni zipi na mchele ni upi..........
 
Katika hali ya kawaida bunge letu linapashwa kuwa ndicho kielelezo cha demokrasia ya kweli hapa nchini. Lakini mambo ni tofauti; hivi sasa Spika anadiriki kuwakemea wabunge kama kwamba ni watoto wa chekechea. Kwa mfano, leo hii asubuhi, baada ya waziri mkuu kumaliza kujibu maswali ya moja kwa moja, kuna mbunge aliyeomba mwongozo wa spika akitaka kujua ni hatua zipi mbunge anaweza kuchukua, iwapo kiongozi wa ngazi ya juu kama waziri mkuu, atalidanganya bunge. Badala ya kumjibu swali lake, spika alianza kumshambulia yule mbunge, akihoji iwapo mbunge yule alikuwa na maana ya kuwa waziri mkuu ameliongopea bunge; na kuongeza kuwa kama ni hivyo aiweke kimaandishi. Ni maoni yangu kuwa huo ni ubabe tu, maana muuliza swali hakusema kuwa hali hiyo tayari imejitokeza, alichotaka kujua ni kama hali hiyo ikijitokeza mbunge anaweza kuchukua hatua gani.

Kila sehemu in taratibu zake.

unawezakuuliza swali gumu kwa lugha ya kistaarabu kama alivyofanya Mh. F. Mbowe na ukasikika.ila kumwita waziri Mkuu muongo si ustaarabu hata kidogo! Mh. Mbowe pamoja na kwamba ndiye mwnyekiti wa CDM na kiongozi wa kambi ya upinzani, ameuliza swali zito kwa ufasaha bila jazba wala kejeli na imependeza kwani sii lazima utukane uonekane mpinzani wa kweli.

Mh. Lema akumbuke anaitwa "Mheshimiwa Lema" na sii Lema tena so inapostahili aonyeshe ustaarabu na ustaarabu ni pamoja na kuwaheshimu na kutowadharau wenzako na hasa viongozi wako. Waziri Mkuu ni kiongozi wa kitaifa hata usipo mheshimu yeye kama Pinda lakini kama PM inabidi apapewe heshima ya u PM!

Ila wamsamehe tu Mh. Lema, maana he is still new in the house na bado illusions za wakati wa uchaguzi hazijaisha, he will learn and he will cope.
 
me nafikiri huu ni mwelekeo mzuri from hapa ndio watu watajipanga vizuri katika kusimamia na kukabiliana na changamoto zinazo kabili nchi hii na sio kupoteza muda wa kisifia hotuba ya Rais na mifano kama hiyo
 
Back
Top Bottom