UKITAKA KUNYWA SUPU YA MBWA, SHARTI IWE YA MOTO!!! Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu msemo huu. Maana ya msemo huu hainitatizi sana, kinachonitatiza ni kuwa kwa nini wahenga waliamua kutumia neno MBWA na si mnyama mwingine, ilhali wakijua kuwa katika jamii nyingi za kitanzania MBWA si chakula cha binadamu labda kwa ndugu zangu wahehe.