Kwa nini mkeo akuibie pesa??

wengine wanachangia ila wamo humu humu wamejaa tele hawajui kutunza wake zao zaidi ya kukimbilia hao wauza bar na kisomo chao cha msaada wa serikali jamani washindwe na wafungiwe tuwataje
 
Natamani wafunguke ili tujue sababu labda tunaweza okoa baadhi ya familia.


wengine wanachangia ila wamo humu humu wamejaa tele hawajui kutunza wake zao zaidi ya kukimbilia hao wauza bar na kisomo chao cha msaada wa serikali jamani washindwe na wafungiwe tuwataje
 
pole Kongosho huo ni mtihani....

ongea na huyo baba specific,kama bado anaipenda nyumba yake,mtafute akiwa sober mwambie aachane na ulevi,watoto wake wanamuhitaji na mkewe.....kama ni beer ndio zinampeleka bar awe ananunua chache awe anakunywa nyumbani,weekends watoke wote kama familia na kama anaboreka ajiunge hata na gym ya kufanyia mazoezi,

ila ulevi noma sana kuna stage ikifika unaogopa mtu anapoelekea mie nina kaka yangu hatujui tumfanye nini jinsi alivyojikita kny pombe.....
 
Kwa kweli hii tabia ipo sana kwa sisi wanaume, kuna wakati utafikiri mtu umelogwa, eti nyumbani hakuna hela ukizipata tu kwa machangu, its too bad, unakuta mama ndiyo anahangaika huku na kule jamaa akipata pesa nyumbani hakai, nimeona sana ujinga huo, aibu tupu. Mi nasema hata ukimkuta utupu ukubai kudanganywa ....teh teh, sifurahii maana ni aibu kabisa, unafikiri yeye ataishije, jamaa likifika home ni usingizi tu, in two days mama akakope mahali ndio wale, wehu kabisa. Wanaume tubadilike jamani. Mwanake nyumbani lazima awe mke jamani dont tyake that easy, eti mama ana hela ni zake, lazima akufpiki chakula hata kama ni waziri, na sisi tutimize wajibu mnunulie hadi chup.i,lakini hii ya kusubiri mke hadi aibe its too much na wengi wanaiba, kabisa,
MEN TUTIMIZE WAJIBU WETU.
jamani kwa wanamme mlooa

inakuwaje mkeo hadi akuibie pesa? Tena kwa kushirikiana na watoto wake mwenyewe?

Mie nadhani hapa kuna tatizo kubwa zaidi ya pesa. Hapa baba anaonekana kama 'intruder' nyumbani kwake mwenyewe.

Mke aliyemuoa hana tabia ya wizi wala udokozi leo kageukaje mwizi? Au kweli wababa wanapenda kusaidiwa kutunza mke?

Mme ana pesa kama nini anahonga tu afu mke hata hela ya mafuta ya kujipaka hadi auze ubuyu? Why?

Eti mie ndio naambiwa nisuluhishe, nisuluhisheje jamani hii familia?

Nataka niwaambie wakae wa-review kama wana haja ya kuendelea kuishi pamoja vinginevyo bora kila mtu akamate njia yake.
 
Kongosho tupe up-date kikao kilikuwa saa kumi...........Ingawa tunajua msimamo wako ulikuwa kila mtu achukue hamsini zake
 
Last edited by a moderator:
my bro blaine n kurt thanks for calling be blessed.

mdogo wangu Kongosho kwanza pole manake naona jinsi ulivyokuwa nervous sana juu ya hili swala. yawezekana kabisa nimetoa ushauri wangu at late times but naomba tu niseme kwani kuna kitu kimenigusa sana hapo.

kwanza nianze na wewe, Kongosho ndugu yangu unapoitwa kusuluhisha swala la kifamilia kama hili yakupasa uelewe kwamba hutakiwi kwenda ukiwa na negativity wala ukiwa na majiabau tayari. siku zote nenda kwenye kushauri kama vile mtafiti anapoingia maabara ili avumbue kitu, haendi akiwa na majibu bali anakwenda akiwa na focus kwamba mwisho nataka nipate nini? kwa jinsi nilivyousoma uzi huu its like tayari unayo majibu ya nini utakacho pata na kibaya zaid ukaenda ukiwa na focus ambayo kwangu mimi nisinge iwaza kabisa manake siku zote huwa nategemea nipate majibu mazuri. ingawa hili doesn't work out every time.

sasa nirudi kwa familia husika, jamani hivi kweli sawa silazimish watu wawe kama mimi na hili siwez kumwambia mtu afanye kwani lahitaji imani ya kweli tena isiyotetereka kitu ambacho ni kigumu sana miongoni mwa watu.

kutoka kwa huyu mama nimejifunza jambo moja kubwa sana ya kwamba anaweza kukaa na watoto wake waapanga njama za kumuibia baba lakini jamani hivi sasa huyu baba akishajua kuwa mnamsachi akawa akirudi nyumbani wallet ni nyeupe je wataiba wapi tena? manake anao uwezo wa kuzificha hela hata kwenye gari ama kwa kimada ili mkose.

jamani naomba nisiseme nini kifanyike manake...............

Hapo kwenye red ndipo nimepaona kwanza!
Kwenye blue usiogope mitazamo yabisi ya wengine kuhusu kile unachoamini kwa dhati......Kila mtu ana namna yake anavyopokea ushauri.................Ni heri ushauri "mbaya" wa yule anayeamini kwa dhati ya moyo wake kuliko ushauri wa kizandikii wa kufurahisha baraza au kupakazana usasa wa kuiga!

Endelea.................................
 
Nimesahau.......ngoja nielekee disco vumbi.......Hali ngumu ya maisha lakini hata kufurahi tushindwe...kha!
 
Hapo kwenye red ndipo nimepaona kwanza!
Kwenye blue usiogope mitazamo yabisi ya wengine kuhusu kile unachoamini kwa dhati......Kila mtu ana namna yake anavyopokea ushauri.................Ni heri ushauri "mbaya" wa yule anayeamini kwa dhati ya moyo wake kuliko ushauri wa kizandikii wa kufurahisha baraza au kupakazana usasa wa kuiga!

Endelea.................................
platozoom siokwamba naogopa bali najua nitakayosema ni mazito na ambayo pengine wengine hawayawazi kabisa.wale waliaokutana na mimi kwenye maswala ya ushauri wanaweza kukuthibitishia hili. kwa sasa Kongosho amesha kwenda shaurini so haina maana tena.
 
Last edited by a moderator:
Natamani wafunguke ili tujue sababu labda tunaweza okoa baadhi ya familia.

Hapa mbaba amemchukua binti wa watu na kumwachisha kazi wakati maisha yetu kibongobongo unatakiwa utoe support japo kidogo kwa wazazi sasa hapo ndio inakuwa shida, mwanaume anaamini ela yake ni kwa ajiri ya familia yake pamoja na wazazi wake kijijini na inapokuja shida upande wa mkewe mwanaume anakuwa tindo hapo ndio mchezo unapoanza, mwanaume anaehonga sidhani kama hata atakuwa na salio nyumbani labda kama utakuwa na password ya ATM yake
 
Baba kama ni mchumi kupitiliza hupatwa na tatizo hili.
Baba kama haachi matumizi nyumbani lazima yamkute haya.

Lakini tusi sahau kuwa watoto na mke wanaweza kuwa na tabia za udokozi tu na wakafanya hivyo.
Hila mara nyingi ukiona wameungana na mama yao ujue lazima kuna sababu hasa pengine mume haachi pesa nyumbani.
 
Kwa mawazo yangu tabia ya mkeo kukuibia pesa inachangiwa na mambo yafuatayo;
  • Kutokumshirikisha mkeo katika mipango yako ya Maendeleo
  • Kuwa msiri kwa mkeo hasa kwa kipato unachopata katika mshahara wako kama wewe ni muajiriwa
  • Kutokumpa mkeo majukumu hili litamfanya asijione kama na yeye ni mmiliki wa mali yenu
  • Kuwa na tabia ya kutumia pesa zako hovyo hasa kwa kuhonga
  • Kutokumshirikisha mkeo kufahamu vyanzo vyako vingine vya mapato
  • Kutokukaa na familia na kupanga mipango yenu na malengo ya familia kwa mwaka mzima
 
Wanaume wengine ni wabahili hata kama ana pesa vipi! Akitoa pesa roho inamuuma,

kumsaidia ni kumwibia na wala hata ha note ili kumuepushia maumivu ya moyo wake ulio bahiri hadi masaburini!
 
Mke wako ana haki na pesa yako akichukua sio wizi....Mwambie yule mjinga kama hana uwezo wakuoa asioe.

Sijawahi kusikia mke anaiba pesa za mme wake, isipokuwa kwa wale wajinga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom