Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Siku ya Ijumaa CUF walifanya mkutano wao wa uzinduzi wa kampeni pale Kidongo Chekundu maeneo ya Gerezani jijini Dar. Jee hii ni kutokana na kupungukiwa wafuasi na kuona kuwa kule Jangwani wangeonekana wanapwaya? Kwa maana nyingine jeuri ya kuitisha mikutano mikubwa mikubwa kama vile ya 2000 na 2005 imepotea?
Tukumbuke hadi sasa CUF ndiyo ina rekodi ya kufanya mkutano uliofurika watu pale Jangwani mwaka 2000, mkutano wa kampeni ambao watu wenye kumbukumbu walisema unakumbushia mikutano ile ya kudai Uhuru miaka 50 iliyopita (ingawa mimi bado siliamini sana hilo kwani Dar wakati ule ilikuwa na wakazi si zaidi ya laki 3.)
Ni kweli, mkutano wa CUF wa Kidongo Chekundu siku ya Ijumaa ulionekana kufurika watu lakini uwanja huo ni mdogo sana ukilinganisha na ule wa Jangwani.
Halafu isitoshe CUF walichagua siku ya Ijumaa kufanya huo mkutano wao kwa sababu moja kuu kwamba ni siku Waisilamu wengi maeneo ya jirani waliokuwa kwenye sala ya Ijumaa walipomaliza tu wakaenda mkutanoni kutokana na ukaribu. Hali kadhalika wafanyakazi waliotoka maofisini.
Hii pia inaongeza ile hoja kwamba CUF ni chama cha Kiisilamu. Halafu kama ulichunguza sana picha za magazeti zilizoonyesha mkutano huo na ule wa Chadema kule jangwani siku ya pili yake utaona ule wa CUF wahudhriaji weni walikuwa wamevalia baraghashia kuliko ule wa Chadema. Ziangalieni hizo picha tena.