Kwa Mshahara huu CCM msitafute Mchawi

Ndugu wengine tumesoma chemistry na biology pale UDSM naulikuwa mziki wa ukweli. uliza waliosoma enzi hizo nafikiri wanawajua vema Prof Othuman wa (Instrumental chemistry), Mdachi, Akwilapo, Forester nk, kule Zoology na Botany ndiyo usiseme ulizia course iliokuwa inaitwa Zl 121 na Zl 122 nk na course nyingine nyingi ambazo zilikuwa mziki mnene.
 

KAMA HUJATUMWA sijui!......unataka kuniambia hakuna walimu wenye DIVISION 1 MPAKA 3 au wewe umeona tu hiyo 4?...ni ivi ualimu huwa unaenda mpaka Div 4 KWA JILI YA MASLAI HAYOHAYO IVYO WATU WENGI HAWAENDI SASA NDO mana unaona ivyo!yaani hauna motisha!....!kumbe unaona sawa walimu kunyonywa?...siamini!
 
SAWA wewe ulifundishwa na jiwe na ukafaulu ivyo! MUNGU AKUBARIKI SANA NA UFANIKIWE MAISHANI!...ETI golden BOY! SASA nani asiyejua hayo!wewe didimiza tu ELIMU KWA KUWA NDUGU ZAKO WENGI WANASOMA ULAYA!
 
DIV 4 haiwezi kuwa sawa na div 1 & 2.

waacheni wana Afya wale kuku PCB ngumu jamani
 

Hahahahahah.....Acha wewe kuna mtu ana div 1! say PCB akawa mwalimu? nonononononononooooooooooooo huu utani
 
Mimi nina wasiwasi na ELIMU YAKO HATA WEWE INGEKUWA NO IVYO HATA AKINA mulugo wasingepata huo uwaziri kama inaangaliwa ivyo! mimi kuna watu nawajua kutoka ndni ya mioyo yao tu wanapenda fani ya ualimu na walifaulu vizuri mboan wapo ndani ya iyoiyo system ya mishahara?...yaani nimeamini mchawi wa mwalimu ni mwananchiimwenyewe! halafu hapa mnakuja kulalamika eti Wanafunzi wanafeli kwani zamani walikuwa wanafauluje?....na bado itakuwa 3 +3=9.....Unamwaga ugali wanamwaga mboga!
 
Hahahahahah.....Acha wewe kuna mtu ana div 1! say PCB akawa mwalimu? nonononononononooooooooooooo huu utani

Sawa kama ni ivyo wewe kwa akili yako unadhani tatizo ninini?mbona mnataka kuwakatisha tamaa walimu kiasi hiki?kusema ukweli wanalaumu sana!...sasa unataka kusema wafanyeje?na je wote wanaopata ilo daraja ni kwamba hawana akili?,,,,nakwambia ukweli mimi niliwai kusoma na mtu mwenye upeo mkubwa sana iyoiyo unaoita sijuiGOLDEN LAKINI AKAPATWA NA MIKASA YA MAISHA AKAJA KUPATA 4 ndo hao unaoona wanajinyonga au usahishwaji mbaya mwenyewe umeona matokeo ya mwaka jana ....usiseme ivyo ndugu yangu temea mate chini!kama si wewe ndugu yako yatamkuta!..maisha yalivyo magumu ivi unasapoti wanavyolipwa?unataka wakajiuze?nchi hii mbona keki inaenda kwa wengine?haya wabunge wangapi wamesoma mbona mfuo wa kulipana haupo ivi? ina mana wenyewe ndo watu? na je wanaopanga mishahara wameona kada ya ualimu ndo hawajasoma tu?kwa nini wasifanye ivyo hata kwa wanasiasa? afakari chukua hatua!
 
Wewe una div ngapi ya hkl?

Mimi niliiacha History tokea form 2, nilichukua pure math! so option zangu zilibaki PCM,PCB,PGM na EGM.


Narudia Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kwenda kusoma ualimu akiwa na DIV 1 ya PCB or PCM.......... kama wapo labda wale walioandaliwa deal maalumu somewhere.............Acheni kulalamika msome mkiwa vitandani kisha mtake mishahara sawa na wale waliosoma wakiwa miguu ndani ya maji baridi.
 
Wewe una div ngapi ya hkl?

kweli wewe ni mume mwema! mwambie atuonyeshe cheti! au ndo hawahawa wanaopanga mishahara na walimu walifa wanaendelea kuchukua mishahara ya walimu ndo mana anashadadia hii kitu yaani hana hata haya!
 
wacha uongo wako. Kuna wahadhiri wengi wameunga sana tu, mfano mzuri ni Michael Kadege. Unajua àlikotokea?
 
NARUDIA TENA wewe UMETUMWA!na Namuomba MUNGU AKULAANI KWA KUWAKANDAMIZA WALIMU! ETI WLIFELI SIO WOTE! basi na hyo masomo ungejifundisha bila haohao walimu,ualimu ni wa kuheshimika!je mapolisi na wanajeshi na vitambi vyao ndo walifaulu? yani ningekuona ningekukunja shati!
 
Hahahahahah.....Acha wewe kuna mtu ana div 1! say PCB akawa mwalimu? nonononononononooooooooooooo huu utani

duh, wajinga wengi sana kumbe. Hivi utaipoata hyo div. 1 bila kuwa na mwalim wa kiwango hicho? Usione matokeo shule za serikali yanashuka kila siku, pengine ni kwa sababu walimu wanaambiwa maneno ya namna hii. Uliza kila mtu aliyefanya vizuri, lazma àtakutajia walimu wake waliomwezesha. Hata wewe unajua hilo,
 
walimu wenye div 4 labda wa primary school, hamna mwalimu wa degree mwenye div 4 Tanzania labda kama amesoma SUA, Maana hata huyo anaechaguliwa kusoma Kilimo SUA anakuwa ameshindwa cutoff point UDSM hata za huo ualimu maana hakuna kilaza anachaguliwa UDSM. Acheni mbwembwe
 
Apa serikali lazima itenganishe kati ya walimu wa sayansi na hawa wengine kwani hivi ni vitu viwili tofauti kabisaa ata density na concentration ya masomo yao ni tofauti kabisaaa....Lazima serikali ielewe mikiki na uzito wa aya masomo ya sayansi ni lazima WALIMU WA SAYANSI wawe group moja la madaktari na watu wa AFYA wengine ni porojo tu na tusitegemee TAIFA kuendelea km litaendelea kuwaweka sawa science teachers and the rest...inshort mishahara ya science teachers should be 15 times more than wengine....
 

Aliyekwambia Ualimu unasomewa kitandani nani? Nenda UDSE ukaone. Ukichunguza vizuri hii mijitu inayodharau walimu utakuta hata shule haijaenda na kama imeenda wala haikuelimika.

Tatizo pekee la sekta ya Elimu ni kutokuwa na mazingira ya kuwavutia wanafunzi wengi. But that doesnt mean Daktari anamzidi lolote mwalimu aliyeelimika.
Miaka ile tunamaliza kidato cha sita wapo wenzangu tuliosoma nao PCB walienda Muhimbili. Prestigous kuwa daktari sio? Tupo tulioenda kufanya Bsc. Ed na hawatuzidi lolote kimaisha. Nilifundisha Chem/Bio shule binafsi kwa miaka miwili nikilipwa far better than them. Ulipofika wakati wa kwenda penye uvyevu unyevu zaidi nikaondoka.
We baki na kelele za walimu wamefeli.
 

......and who is the Division Maker?
 
Wote mnaowadharau walimu naona upungufu katika fikra zenu.
Msiishie kuwatusi na kuwashusha tu ila ni bora mkawachukue na ndugu zenu wote wasomao kwenye shule wafundishazo kisha muwafundishe wenyewe.Kupata div iii au div iv haimaanishi kukosa akili,ni mengi yanachangia kuanzia mifumo,mazingira nk.

Nawafahamu wengi ambao o-level walionekana hawako smart sana lakini mazingira ya a-level yalipobadirika wakawa safi zaidi ya wale waliowashusha,na chuo the same thing happened kwani kuna waliopata admission kwa points ndogo zaidi ya wengine mwishowe wamekuwa na G.P.A kubwa kuliko wale walioonekana vinara a-level.

Pia kuna wengine ambao wamegraduate kwa pass au lower second ila practically wako mail 1000 zaidi ya wenye first au upper second.....
Fanyeni utafiti ndo mtajua,binafsi natambua hilo ndo maana sijawahi jivunia matokeo yangu yoyote na kubeza ya mwingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…