Kwa mpango huu ni gharama sana kuishi Dodoma kuliko Dar, wananchi tunaliwa

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,885
Juzi (jumapili) nilishuhudia magari makubwa ya serikali zaidi ya mia mbili yakiwa kwenye mwendokasi yakitoka DSM wanakoishi watumishi wa serikali yakielekea Dodoma wanakofanyia kazi za wizara zilizohamia Dodoma. Hawa watumishi wa serikali makazi yao na familia zao zipo DSM na Wao wapo Dodoma.

Kila ijumaa mchana wanarudi DSM kwa magari ya serikali yanayotumia mafuta kwa fedha za serikali au za walipakodi na kurudi Dodoma Jumapili jioni. Watumishi hawa wapowapo tu Dodoma wengi wakirandaranda maeneo ya Chuo Kikuu Dodoma.

Naamini mojawapo ya hoja za kuhamisha serikali kwenda Dodoma ilikuwa kupunguza gharama na matumizi ya Serikali. Lakini kinachoendelea sasa ni KUONGEZA GHARAMA ZA KUENDESHA WIZARA. Hili inabidi tuliseme.

From intellectual in social network
 
Katika kubadilisha mwelekeo ambacho ni kitu kizuri. Wasiwasi wangu ni kama yupo balozi yeyote aliye tayari kuifuata wizara ya mambo ya nje maana nimesikia nao wamehama jana na hapo achilia mbali baadhi ya ndoa zilizo mashakani kwa kuhama kwa mmoja wa wanandoa.
 
Katika kubadilisha mwelekeo ambacho ni kitu kizuri. Wasiwasi wangu ni kama yupo balozi yeyote aliye tayari kuifuata wizara ya mambo ya nje maana nimesikia nao wamehama jana na hapo achilia mbali baadhi ya ndoa zilizo mashakani kwa kuhama kwa mmoja wa wanandoa.
Ni watumishi 40 tu wa mambo ya nje waliohamia Dodoma, wengine wote wapo Dar. Kuhusu balozi kuhamia Dodoma hakuna namna lazima watahamia tu. Hivi sasa wizara inajadiliana na mabalozi mpango mzuri wa wao kuhamia Dodoma na punde watakapoafikiana wataanza kuhama.
 
Halafu wanahama nusu nusu,wanaondoka makatibu wakuu,mawaziri na wakurugenzi,

Supporting staff/wafanyakazi wa kawaida wanabaki dar .....ukiwa na shida na waziri na umetoka mtwara au songea

unaenda dodoma,waziri anakuambia kamuone katibu mkuu,katibu mkuu anakwambia nenda kwa afisa fulani aliyebaki Dar atakusaidia,unapanda gari mpaka Dar,unalala,unamsubiri afisa huyo,anakusaidia,anakwambia hii ishu lazima ipitiwe na kupitishwa na katibu mkuu,unarudi dodoma unapanda basi,unamuona katibu mkuu

Hii gharama na italeta usumbufu,sijui kama ni kipaumbele kuhamia dodoma na tukihamia huko ndio shida za nchi zitakwisha
 
Juzi (jumapili) nilishuhudia magari makubwa ya serikali zaidi ya mia mbili yakiwa kwenye mwendokasi yakitoka DSM wanakoishi watumishi wa serikali yakielekea Dodoma wanakofanyia kazi za wizara zilizohamia Dodoma. Hawa watumishi wa serikali makazi yao na familia zao zipo DSM na Wao wapo Dodoma.

Kila ijumaa mchana wanarudi DSM kwa magari ya serikali yanayotumia mafuta kwa fedha za serikali au za walipakodi na kurudi Dodoma Jumapili jioni. Watumishi hawa wapowapo tu Dodoma wengi wakirandaranda maeneo ya Chuo Kikuu Dodoma.

Naamini mojawapo ya hoja za kuhamisha serikali kwenda Dodoma ilikuwa kupunguza gharama na matumizi ya Serikali. Lakini kinachoendelea sasa ni KUONGEZA GHARAMA ZA KUENDESHA WIZARA. Hili inabidi tuliseme.

From intellectual in social network

Inaruhusiwa watumishi wa umma kutumia magari ya umma kwa shughuli binafsi? Wikiendi si wapande ndege au watumie magari binafsi?
 
Ni watumishi 40 tu wa mambo ya nje waliohamia Dodoma, wengine wote wapo Dar. Kuhusu balozi kuhamia Dodoma hakuna namna lazima watahamia tu. Hivi sasa wizara inajadiliana na mabalozi mpango mzuri wa wao kuhamia Dodoma na punde watakapoafikiana wataanza kuhama.
Sijui nijiulize, nijijibu au nikuulize wewe kama Marekani wataliacha jengo lao la ubalozi na kujenga jipya Dodoma, au nao wataingia kwenye majengo ya UDOM!?
 
Moja ya mambo yasiyo na maana yaliyofanywa na serikali ni kuhamia Dodoma.

Hapakuwa na sababu za msingi za kuhamia Dodoma.

Hii serikali ya mikurupuko ni janga la kihistoria.
Nimeamini kuwa Rais wa Tanzania ana nguvu kubwa mno!!

Kwenye nchi ambazo kuna democracy ........ tusiende mbali ..... hapo Bondeni tu RSA, Rais hawezi kuhamisha serikali bila baraka za Bunge!!
 
Nimeamini kuwa Rais wa Tanzania ana nguvu kubwa mno!!

Kwenye nchi ambazo kuna democracy ........ tusiende mbali ..... hapo Bondeni tu RSA, Rais hawezi kuhamisha serikali bila baraka za Bunge!!
Kwenye nchi zenye demokrasi na Tanzania umeijumuhisha?
 
Back
Top Bottom