Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela!

Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela!

Lissu na Dereva wake wamekufa au wapo hai!... lini jeshi limewataka waje watoe maelezo wakakaidi kuja?... Acha siasa kwenye roho za watu
Mtu anapigwa risasi zaidi ya 30 tena ndani ya eneo lenye usalama 24hr tena ulinzi wa serikali , halafu unakuja kutapika hapa.
Mbona walinzi hawajahojiwa?...walikuwa wapi?
Shenzi sana
Wewe nikuambie tu,Mchawi wa Lisu ni Lisu mwenyewe. Anayetakiwa apambane anapata haki yake ni Lisu. Huyo lisu kwanini asirud kudai HAKI yake?Au huko Ulaya ndio anadai haki yake?Haki inatafutwa, lini lisu katafuta haki yake?Kwamba Mwanasheria lisu anaamini haki yake ataipata kwa kuzurula Ulaya na kuandaa madesa fb na sio mahakaman?Kwamba haki ataipata kwa kuendelea kuleta story za Oooh eneo linalindwa masaa 24 mara kuja na story za kufikirika kwamba risasi 16 zilitua mwilini?Yaani hizo zilikua risasi au miiba?

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
A
Huyo lisu ndio anatakiwa apambane apate HAKI yake sio polisi. Siro alipoibuka na kusema tutaenda kumhoji lisu Nairobi, lisu akaibuka na visheria koko kuwa polisi Tanzania haiwez kwenda kumhoji huko. Huoni ni maajabu kwa Mgonjwa kuleta ujuaji mbele ya daktari?Palepale Nairobi lisu ilitakiwa kupitia mawakili wake hata kama yy angekua hajiwez angewatuma pamoja na dereva wake kuja kuhojiwa. Hapa tungesema kweli jamaa anataka haki yake, lkn yeye ndio namba moja kutuma kejeli kwa polisi na serikali, ye ndio namba moja kumkumbatia dereva wake. Serikali ina nini cha kupoteza kwa lisu?Huoni maajabu lisu alipata nafas ya kufanya conference Nairobi lkn hakuwa na nafas ya kuja kudai HAKI yake?Huoni ajabu Lisu kapata nafasi ya kudai HAKI yake lkn ndio kwanza anazurula ulaya eti kutangaza kilichomtokea?Huoni ajabu hadi saiz hujui dereva yuko huko Belgium na hujui anasoma nini na nani anamsomesha na kwanini asirudi nyumbani kutoa ushirikiano?FUNGUKA AKILI,USIENDESHWE KAMA TAIRI BOVU.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
unasema uongo bila aibu, lini polisi walisema eti wanataka kumfuata nairobi? Sanasana walituma mtu kumdhuru aksvurumishwa, kila siku lissu amekua akilalamikia kitendo cha polisi kutomhoji
 
Wanabodi,
Declaration of Interest
Naomba ku declare interest kuwa mimi sina chama, namfahamu Lissu na kumkubali sana tuu, pia na sympathize yeye kwa kilichompata, ila ninachofanya hapa ni being objective. Pia nafahamu fika kinachotokea kila ukifanya ukosoaji wa Chadema au viongozi wao wanaowaabudia, hivyo wale wa kutukana, be free to do so, the truth will always be the truth and will stand up to the end.

Hili ni bandiko la swali, "Kwa Mliomsikia Tundu Lissu Kwenye Hard Talk, Jee Unadhani Atarejea Nchini?. Mimi kwa upande wangu, I seriously doubt kama atarejea, na ikitokea kweli akarejea, then Tundu Lissu atakuwa ni shujaa mwenye ushujaa mkubwa kuliko hata ushujaa wa Nelson Mandela!.

Nimesema hivyo kwa sababu nimemsiliza kwa makini Tundu Lissu. him being a Lawyer, kwa yale aliyoyasema, kwa tuhuma alizoshusha bila ushahidi, I seriously doubt if Tundu Lissu will ever return home during this era, na ikitokea kweli akarejea, then Tundu Lissu atakuwa ni shujaa kuliko Nelson Mandela, kwa sababu Mandela alirejea kuendeleza mapambano bila kujua nini kitampata, na alipofungwa jela na kusurvive hadi kuja kuja kuwa rais wa SA, hakujua, lakini Lissu, being a lawyer, anajua kabisa huwezi kutuhumu na kutaja majina ya watu bila ushahidi, hivyo ukirejea nchini, anajua fika akikanyaga tuu ardhi ya Bongo, atapokelewa na nani, na anajua atafikia wapi, and kwa situation hii tulionayo sasa, with vitu kama polonium 210, I doubt kama he will be so lucky kama Mandela.

Hivyo huu ni wito kwa watu wa karibu na Lissu, mshauri tuu aendelee na matibabu, hata mwili ukipona kabisa, aendelee tuu na matibabu ya kisaikolojia, ila aandike barua kwa Spika kuelezea kuwa bado anaendelea na matibabu, na kabla hajarejea, atumie international fora, kujihakikia akirejea, hata pokelewa na wale mimi ninaodhania ndio watampokea na hata fikia kule mimi ninakodhania atafikia.

Waliomshambulia Lissu ni watu wasiojulikana, hivyo nilishauri humu
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Pia nikawatambulisha aina mbili za wasiojulikana
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Nikauliza
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums

Mwisho nikasema waandishi wenye uwezo wa IJ, wanaweza kumsaidia Kamanda Siro kuwabaini wasiojulikana hawa, na mimi ni miongoni mwa waandishi wa IJ,
Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija - JamiiForums

My Take.
The Hard Talk kwa Lissu was a waste, Chadema inabidi ianzishe kitengo cha International Politics kuwafunda makada wa Chadema, wakipata international foras, waseme nini in terms of International politics. That was a great opportunity kwa Lissu kuongea as a president in waiting na sio kuongea kama mwana harakati mwanzo mwisho. Hakupaswa kutoa tuhuma zisizo na ushahidi, pia hakupaswa kuponda mwanzo mwisho as if Magufuli is all that evil, and is doing nothing good for this country.

Kwa upande wa lingua, kiukweli Lissu ana flow, kwenye top 5 wetu, mtu pekee mwenye uwezo wa kuflow kivile ni Mama Samia, na labda Majaliwa, tukishuka chini zaidi kwa mawaziri, MFA na January they are good. Kwa upinzani, ikitokea mtu kama Zitto akakaribishwa Hard Talk kiukweli mtaona the difference, nawashauri Wapinzani the man to bank on ni Zitto, kwa sababu Lissu kaharibu, unless awe kaharibu makusudi ili akirejea apokelewe kule so that they can make big noises!.

Paskali
Rejea za Ushauri wangu kwa Tundu Lissu na Chadema
Swali la Morality: Je ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa? - JamiiForums

Mhe. Tundu Lissu, Please Acha Kumsulubu Spika Wetu!, Unammaliza Kabisa Hadi Ameshindwa Kazi!. - JamiiForums

CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA!. - JamiiForums

Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele! - JamiiForums

Vurugu za Bungeni: Mhe.Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!. - JamiiForums

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe! - JamiiForums

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele! - JamiiForums
Unaushahidi juu ya waliomshambulia ni wasio julikana? Hebu fafanua
Na unadhani kwa nini walimshambulia?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
A
unasema uongo bila aibu, lini polisi walisema eti wanataka kumfuata nairobi? Sanasana walituma mtu kumdhuru aksvurumishwa, kila siku lissu amekua akilalamikia kitendo cha polisi kutomhoji
Kama hufuatilii vitu ni bora ukabaki mkata mauno hapo ufipa. Sina mda wa kukuelezea hili.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Pasco kumtaja Lissu na Mandela kwenye sentensi moja ukiwahusisha kwenye harakati za kupigania haki ni kulikosea heshima jina la mpigania haki Nelson Mandela. Hebu tuamke kutoka kwenye usingizi WaTanzania tuache kupachika viongozi na kuwatunukia masifa kem kem sababu tu tuna kiu ya kuwa na kiongozi na kwa sasa kuna Ombwe la uongozi kwenye siasa zetu. Tuwaweke kwenye maeneo stahili viongozi wetu kutoka na uwezo wao wa kweli. Tindu Lissu bado sana, kwenye kundi lile kubwa la wanaharakati wanaojitolea kupigania haki huko sawa nae yupo lakini sio kuwa mbele ya msafara na kuongoza, ataongoza sababu hatuna viongozi lakini wafuasi lazima tujue sio kiongozi mahiri hivyo. Maskini Lissu naona mzigo mzito sana cha msingi kuwa mkweli kubali mapungufu yako na uwe tayari kutoa sifa na heshima pale unapoona ipo, unless hujui viwango kabisa.
Mbona mnapenda sana sifa?
 
ATAKUWA SHUJAA KWA MASHOGA WENZAKE
Kama alivyo Mahiga ambaye ameuthibitishia ulimwengu kwa niaba ya serikali.
Ukumbuke Lisu hana serikali na siyo msemaji wa serikali na ulicho kiona ni ushoga tu ndiyo utarudisha nyuma maendeleo, mashoga walikuwepo na wataendelea kuwepo,na wengine wapo kisirisiri na wengine wanaotuhumiwa kwa mfano mzuri ni Bashite.
Halafu mashoga wanaonekana wivu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulisikia nini alichosema kipindi hicho kuhusu yy kwenda kuhojiwa huko?Aliyeleta story za polisi Tanzania haiwez kwenda kumhoji huko Kenya ni nani?Kwanini huyo dereva asirud Tanzania kuhojiwa ila polisi Tanzania ndio wamfuate yeye?Kwanini huyo dereva baada ya kutoka Nairobi asirudi Tanzania na akapelekwa Belgium kutibiwa kisaikolojia na Mwisho tunaambiwa anasoma?Unaambiwa akina Lema ndio wamemtorosha hapa Tz na huko Belgium kwenyewe hana hati zozote za kusafiria toka Tanzania. Aliyekamilisha mipango hiyo ya dereva kwenda huko lengo nini kama kulikua na nia njema ya kusaidia polisi?Hujui shahidi namba moja na mbili ni Lisu na dereva wake na hakuna popote polisi watasema uchunguz umekamilika bila hao watu kuhojiwa?

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Hivi ingalikuwa ni PM ama Rais ndiye kashambuliwa na risasi namna ile halafu "washukiwa" wameenda nje ya nchi na polisi inajua nchi walipo....wangesubiriwa mpaka waamue wenyewe kurejea?

Kwa kifupi, polisi haionekani kama ina nia ya kufanya uchunguzi. Zipo taratibu za kisheria za kimataifa za kushughulikia watuhumiwa wa uhalifu waliopo nchi nyingine. Lakini (kwa bahati mbaya?), polisi hawajazitumia mpaka leo.

Na kwa kweli kama kuna sehemu serikali ilikosea (au ilishindwa kujisafisha) katika sakata la Lissu ni hapo. Hivi ni kweli kwamba uchunguzi haukufanyika kwa sababu dereva wa Lissu hayupo? Hakuna namna nyingine ya kuchunguza? Kweli? Hii mbona ni dharau kubwa kwa jeshi letu la polisi.

Kwa mtu yoyote sane, hatua ambazo polisi walipaswa kuchukua lakini hawajazichukua zinaleta mashaka makubwa. Si kwa sababu hili linamuhusu Lissu, bali hata lingemuhusu mtanzania yeyote mwingine.
 
Kwa uzoefu wangu Ni kwamba ukishaitangazia dunia kuwa fulani ndiye mbaya wako then uwezekano ni kwamba watajitokeza wengine kabisa wakutungue.TL ana mahasimu wengi tu kama ilivyo kwa wanasiasa wengine na wenye career yake.Wengine watamtandika tu kuichonganisha serikali na jamii kwa hiyo akirudi 100% Yuko kwenye nafasi yakuzioga tena.
Ndiyo mlivyopanga?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali assume Mwiguru Nchemba ndo alikuwa hardtalk leo halafu akaulizwa kama waziri wa mambo ya ndani jinsi alivyoshugulikia suala la Lisu how would he handle the question?? vipi kuhusu watu wote waliopotea na waliookotwa kwenye viroba stop jocking brother with peoples life!! Lisu sio investigator lazima awe na watu anaowashuku na majibu aliyoyatoa ni ya kimazingira ulikata aseme amechunguza
Angejibu lile lilliuwa shambulio la kawaida tu( that was an everday normal case).

hahahaaaa.

kama hawawezi.kwemda kuzima moto kule Hardtalk basi waifanyie hardtalk pale TBC1 wakiongozwa na kijana mahili wa kitanzania Mahela.
 
The Hard Talk kwa Lissu was a waste
Sometimes mzee Paschal huwa haupishani sana thinking yako na Viwavi Jeshi wa Lumumba.
So, unaungana na Humphrey Haraka Haraka kwamba mahojiano hayo ya Lissu yalikuwa sawa na vipindi vya pale TBCCM? Ninyi kama Journalists hapa nchini mmeshindwa hata tu kuandika habari huru kulinda makampuni yenu mnasubiri kuotea Interview za wenzenu muonekane nanyi ni waandishi wachambuzi.
Shame on you.
 
Hili ni bandiko la swali, "Kwa Mliomsikia Tundu Lissu Kwenye Hard Talk, Jee Unadhani Atarejea Nchini?
Hatimae nimesililiza mwanzo mpaka mwisho... sijaona chochote ambacho kinaweza kumfanya asijerejee! Sijaona tuhuma yoyote ya kutisha ambayo Tundu Lissu hajawahi kuisema ukiacha zinazohusu matukio yaliyotokea baada ya yeye kuwa nje ya nchi. Kwa mfano, hapa akielezea suala la Ben Saanane...



Na usisahau, hiyo ni December 14, 2016... bado watu walikuwa na matumaini ya kumuona Ben!

That's one but two, unless serikali ya JPM na watu wao, iwe through official au rogue agents, kwa interview ile kumgusa Tundu Lissu itakuwa political and diplomatic suicide kwa upande wa serikali!

Endapo Lissu atarejea nchini halafu serikali na watu wao wakamgusa kwa namna yoyote ile, basi yale yote ambayo ameyasema yatapata attention kubwa maradufu na kuaminiwa na kile mtu huko duniani hata kama kuna wengine walikuwa wanamtilia shaka!!

Sana sana mimi ningekuwa ndo serikali yenyewe kwenye maamuzi, ningempa ulinzi wa kutosha ili pamoja na mambo mengine, kuzuia uwezekano wa Flase Flag Assassination or any kind of False Flag Operation.

This false flag operation can be conducted by anyone or any group including rogue agents, not in favor of the government but those who're against the government!

I'm telling you, pale alipo the guy has finally become a radioactive material...

The Hard Talk kwa Lissu was a waste, Chadema inabidi ianzishe kitengo cha International Politics kuwafunda makada wa Chadema, wakipata international foras, waseme nini in terms of International politics. That was a great opportunity kwa Lissu kuongea as a president in waiting na sio kuongea kama mwana harakati mwanzo mwisho.
Seriously sijakuelewa! Ulitakaje yaani kwa mfano?! Mimi na wewe tusikiliza interview mbili tofauti au maoni yako unachanganya interview yake kwenye Hard Talk na ile BBC Swahili?

Nilichokiona na kukiskia toka kwa Stephen Sackur kwenye interview ambayo tayari ilikuwa na maswali yake na agenda in advance! Na wala sikumbuki kuona au kusikia open end question ambalo Tundu Lissu angelitumia kuiuza CHADEMA or his future possible presidency!

Halafu, hivi mtu kama Tundu Lissu mnamtaka asifie nini huko ughaibuni?! Kwamba aseme "...lakini pamoja na kunimiminia risasi kadhaa na kutaka kuniua, but on the other side of the coin Magufuli is doing a great job in the so called vita dhidi ya rushwa" wakati mwaka wa tatu unaenda hivi na hatujaona fisadi hata moja miongoni mwa mafisadi wazito wa serikalini waliofikishwa angalau Mahakama ya Mnazi Mmoja!

Yaani mtu unaweza kuamini kwamba, kumbe ufisadi woooooooooooote ambao tumekuwa tukilia nchi hii, mafisadi wakubwa ni Rugemalila na mwenzake Seith na huko serikalini, tangu zama za Mwinyi hadi za JK, wote walikuwa WASAFI, na kama huko serikalini kulikuwa na wezi basi ni wale middle level government officials ndio walikuwa wezi wakubwa na pengine ndio hawa wameficha mabilioni yetu huko Uswisi!

Look, at Steve mwenyewe kashindwa kutoa mfano wa maana wa vita dhidi ya ufisadi zaidi ya kutaja "wafanyakazi hewa!" Hivi kweli kuna mtu anaamini mafisadi wakubwa nchi hii walikuwa wafanyakazi hewa?! Btw, wako wapi wale waliowatengeneza Wafanyakazi Hewa?! How many Maafisa Utumishi waliokuwa sucked kwa kutuletea jeshi la Wafanyakazi Hewa?!
 
Wanabodi,
Declaration of Interest
Naomba ku declare interest kuwa mimi sina chama, namfahamu Lissu na kumkubali sana tuu, pia na sympathize yeye kwa kilichompata, ila ninachofanya hapa ni being objective. Pia nafahamu fika kinachotokea kila ukifanya ukosoaji wa Chadema au viongozi wao wanaowaabudia, hivyo wale wa kutukana, be free to do so, the truth will always be the truth and will stand up to the end.

Hili ni bandiko la swali, "Kwa Mliomsikia Tundu Lissu Kwenye Hard Talk, Jee Unadhani Atarejea Nchini?. Mimi kwa upande wangu, I seriously doubt kama atarejea, na ikitokea kweli akarejea, then Tundu Lissu atakuwa ni shujaa mwenye ushujaa mkubwa kuliko hata ushujaa wa Nelson Mandela!.

Nimesema hivyo kwa sababu nimemsiliza kwa makini Tundu Lissu. him being a Lawyer, kwa yale aliyoyasema, kwa tuhuma alizoshusha bila ushahidi, I seriously doubt if Tundu Lissu will ever return home during this era, na ikitokea kweli akarejea, then Tundu Lissu atakuwa ni shujaa kuliko Nelson Mandela, kwa sababu Mandela alirejea kuendeleza mapambano bila kujua nini kitampata, na alipofungwa jela na kusurvive hadi kuja kuja kuwa rais wa SA, hakujua, lakini Lissu, being a lawyer, anajua kabisa huwezi kutuhumu na kutaja majina ya watu bila ushahidi, hivyo ukirejea nchini, anajua fika akikanyaga tuu ardhi ya Bongo, atapokelewa na nani, na anajua atafikia wapi, and kwa situation hii tulionayo sasa, with vitu kama polonium 210, I doubt kama he will be so lucky kama Mandela.

Hivyo huu ni wito kwa watu wa karibu na Lissu, mshauri tuu aendelee na matibabu, hata mwili ukipona kabisa, aendelee tuu na matibabu ya kisaikolojia, ila aandike barua kwa Spika kuelezea kuwa bado anaendelea na matibabu, na kabla hajarejea, atumie international fora, kujihakikia akirejea, hata pokelewa na wale mimi ninaodhania ndio watampokea na hata fikia kule mimi ninakodhania atafikia.

Waliomshambulia Lissu ni watu wasiojulikana, hivyo nilishauri humu
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Pia nikawatambulisha aina mbili za wasiojulikana
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Nikauliza
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums

Mwisho nikasema waandishi wenye uwezo wa IJ, wanaweza kumsaidia Kamanda Siro kuwabaini wasiojulikana hawa, na mimi ni miongoni mwa waandishi wa IJ,
Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija - JamiiForums

My Take.
The Hard Talk kwa Lissu was a waste, Chadema inabidi ianzishe kitengo cha International Politics kuwafunda makada wa Chadema, wakipata international foras, waseme nini in terms of International politics. That was a great opportunity kwa Lissu kuongea as a president in waiting na sio kuongea kama mwana harakati mwanzo mwisho. Hakupaswa kutoa tuhuma zisizo na ushahidi, pia hakupaswa kuponda mwanzo mwisho as if Magufuli is all that evil, and is doing nothing good for this country.

Kwa upande wa lingua, kiukweli Lissu ana flow, kwenye top 5 wetu, mtu pekee mwenye uwezo wa kuflow kivile ni Mama Samia, na labda Majaliwa, tukishuka chini zaidi kwa mawaziri, MFA na January they are good. Kwa upinzani, ikitokea mtu kama Zitto akakaribishwa Hard Talk kiukweli mtaona the difference, nawashauri Wapinzani the man to bank on ni Zitto, kwa sababu Lissu kaharibu, unless awe kaharibu makusudi ili akirejea apokelewe kule so that they can make big noises!.

Paskali
Rejea za Ushauri wangu kwa Tundu Lissu na Chadema
Swali la Morality: Je ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa? - JamiiForums

Mhe. Tundu Lissu, Please Acha Kumsulubu Spika Wetu!, Unammaliza Kabisa Hadi Ameshindwa Kazi!. - JamiiForums

CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA!. - JamiiForums

Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele! - JamiiForums

Vurugu za Bungeni: Mhe.Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!. - JamiiForums

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe! - JamiiForums

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele! - JamiiForums
Kweli kabisa Pascal, kuna tatizo kubwa kwa wafuasi hadi wanachama wa hivi vyama kuelewa sera na itikadi ya vyama vyao ndio maana wanapinga kila kitu hata kama ndio sera yao kwavile tu anaitekeleza JPM. Sera ya ushoga umeona ilivyompa shida Lissu ingawa wafia vyama watamtetea. Kuhusu kurudi atarudi tu, mbona Zitto anaropoka kila siku na afanywi chochote?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mniwie radhi kwa kuwakwoti nyie wote wawili kwa pamoja ili nami nichangie...

Nimesoma mlichokiandika mara mbili ama tatu. Nikarudi kutazama na kusikiliza tena mahojiano kati ya Tundu Lissu na Steven Suckur...

Nikaona you all missed something. Sina hakika ni lugha ama uwezo wa kuelewa mantiki au evil intentions behind you...

Mimi hoja yangu si Tundu Lissu kurudi nchini kwake ama kuendelea kuwa mkimbizi wa kisiasa huko aliko. Siko huko.....

Lakini nilicho na uhakika nacho ni kuwa Tundu Lissu atarudi Tanzania tena si muda mrefu kwa sbb all he said are not new at all. Ameyasema mara nyingi tena kwa lugha kali kuliko hiyo akiwa London, hakuwahi kukamatwa...

With due respect, hoja yangu kubwa ni kujaribu kutafakari hiki unachojaribu kukiingiza kwenye akili ya vichwa vyetu, kwamba Tundu Lissu alitumia fursa vibaya aliyoipata kwa kutoeleza hata moja zuri la Magufuli....

Aeleze mazuri ya Magufuli kwani yeye ni mke wa Magufuli? Msemaji wa "serikali ya Magufuli?" Msemaji wa CCM?...

Ungesema mazuri ya NCHI mama Tanzania ningekuelewa. Lakini hakukuwa na swali lenye muelekeo huo moja kwa moja!!

Na kwa hoja hii haraka haraka nikajifunza mambo mawili kuwa:

1. Kumbe viongozi wetu kupitia ujumbe wako wanahitaji fursa kutumia international media platforms kama BBC, CNN, Sky News, Al Jazeera nk ktk kusema serikali wanazoziongoza zimefanya hili ama lile...

Kwa fursa aliyoipata Tundu Lissu, wengi imewauma sana hususani watu wa serikali (watawala) na wanaowaunga mkono....

Si kwa sababu ameongea uongo, ama uzushi .... la hasha....

Isipokuwa kaongea mambo ambayo kwa wengi wanaona kama amevunja "taboo" moja inayopaswa kulindwa sana.... kutosema mabaya ya serikali na hususani Rais Magufuli😳😳!... And that's the problem we have right now....

2. Uwezo mdogo wa wengi wa waandishi habari wetu wa Kitanzania (ukiwemo wewe Paschal Mayallah ktk hili) wa kuelewa mantiki na kuchambua mambo/hoja kwa kuzingatia "context"...

Mfano kuna mmoja (si wewe, lakini naamini ni journalist) kamtukana kweli Tundu Lissu eti tu kwa sababu katika mazungumzo yale amemsikia muuliza maswali (Stephen Sucker) katika moja ya maswali yake akitumia maneno "baseless allegations"....

Hitimisho lake huyu mwandishi ni kuwa, hata mtangazaji alimwona Lissu akiwa na madai yasiyo na ushahidi (baseless allegations)...

Duuh, nilishangaa na kupigwa na butwaa kuliko maelezo!!

Tukirudi kwenye hoja, kwanza tukubaliane na wewe Paschal Mayallah kuwa kuna uwezekano mkubwa hujatazama wala kusikiliza mahojiano hayo mwanzo mwisho...

Ama kuna possibility number two, kuwa, hukujipa nafasi ya kutosha kupata logic ya kila kilicho zungumzwa na Tundu Lissu.

Nitaeleza......

1. Mahojiano yalikuwa ya kipindi cha takribani dakika 24 tu. Mimi naamini kwa style yako ya kuuliza maswali, kama ungekuwa Stephen Sucker ungeuliza swali moja na kuishiwa muda...

Ama kwa style yako ya kujieleza, ungeishia kujibu swali moja tu na muda kukuishia na kumwacha mtangazaji akitia kikapuni maswali na kurudi nayo kwa mhariri wake...

2. Lengo la kipindi ilikuwa ni Tundu Lissu na yaliyompata na kwa kuhusianisha jaribio la kuuwawa kwake na harakati zake za kisiasa, ukosoaji wake wa sera za utawala wa Rais Magufuli....

Ndiyo maana swali la kwanza la ufunguzi (opening question) lilikuwa, vipi Tundu Lissu na unajisikiaje hali yako kwa sasa?

Lililofuata na ni description ya tukio kwa ujumla na kwa ufupi...

Kisha swali muhimu na ambalo ndilo "backbone" ya mjadala mzima na kuzaa mengine yote yaliyofuata ni hoja ya kurudi ama kutorudi Tanzania ni:

Aliulizwa: Unadhani jaribio la kutaka kukua lina uhusiano na harakati za kuukosoa Utawala wa Rais Magufuli, sera zake na kumuita petty dictator??

Hili ndilo lililozaa maswali mengine yote kuhusu uwekezaji, sijui ghost workers, conrsevative controversial govt statements aginist human right as quaranteed by constitution such as "right to privacy" nk nk

Na hili la human rights na msingi wake ikiwa ni vita ya ushoga vs mkakati wa Paul Makonda (Daud Albert Bashite) RC wa Dsm kupambana nao, Tundu alijibu very clearly unless mtu awe na matatizo yake tu ya uelewa wa mambo kushindwa kumwelewa TL...

Alisema wazi kabisa, kuwa, jambo lolote lililo kinyume na katiba siku zote ni unconstitutional kwa mujibu wa katiba ya JMT ikiwemo "right to privacy"......

Na hili ni kweli kabisa, kama mtu ni shoga ama msagaji na anafanya mambo yake ndani ya chumba chake, how does it concern me and you? Tunapata wapi audacity ya kuingilia mambo ya sirini ya mtu huyo?.....

Kwani ni viongozi wangapi wakubwa ndani ya serikali ni mashoga na wasagaji so long as wanafanyia mambo yao sirini? Si hata Paul Makonda mwenyewe anatuhumiwa kuwa ni shoga? Alionekakana anafanya ushoga wake hadharani? Mimi na wewe hatujui na kiukweli haituhusu....

Itatuhusu tu pale vitendo hivyo vikifanyika hadharani maana hapo itakuwa kinyume cha sheria za Tanzania.... violation of right to privacy!!

Na swali moja kabla ya lile la mwisho kabisa lilikuwa ni aidha kurudi ama kutorudi Tanzania.....

Na kwamba umejiandaaje kurudi Tanzania wakati waliojaribu kukuua hata hawajakamatwa, hakuna kesi, hakuna uchunguzi....huogopi?

Hili sasa ndiyo likazaa swali la mwisho la kufungia HARD TALK la kujibiwa na Tundu Lissu kwa ufasaha ndani ya sekunde 50....

Ni kuhusu ku- fight against Magufuli through ballot paper box...

Tundu Lissu kwa ufasaha kabisa akajibu ".......If my fellow members of the party see me a correct person.....I am more than enough to face Magufuli...!!!"

3. Hakuna mahali katika mazungumzo mwanzo mwisho alipoulizwa direct aeleze mazuri ya serikali na ya Rais John Pombe Magufuli ama sera za CHADEMA...

Ulitaka awe anatoka nje ya hoja kwa mitego ya Muuliza maswali kama Rais Magufuli wakati ule wa press conference kule Uganda hata kusaidiwa kujibu maswali na mwenyeji wake Rais Museven? Anaulizwa hivi, yeye anajibu vile? Au anaulizwa swali la maana yeye anatoa majibu ya kitoto na kijeuri tu???

Na kwa taarifa yako, siyo jukumu lake kueleza mazuri ya "serikali" ama ya Rais Magufuli. Wenye kazi hiyo ni yeye mwenyewe Magufuli, ama Polepole ama waziri wake yeyote...

Kazi ya Tundu Lissu (kama angeulizwa lakini bahati mbaya hakukuwa na swali hilo) ni iwapo angeulizwa kueleza MAZURI YA NCHI YA TANZANIA na mpango wake wa kuyaendeleza mazuri ya nchi mama Tanzania....

Kwa hiyo ni vyema tukatofautisha NCHI YA TANZANIA na SERIKALI YA AWAMU YA TANO YA BWANA JOHN POMBE MAGUFULI....

Tundu Lissu was absolutely full of composure and understable na nikuhakikishie hata huyo Mzungu amemkubali kama tunavyomkubali sisi wengine huku!!
 
Hatimae nimesililiza mwanzo mpaka mwisho... sijaona chochote ambacho kinaweza kumfanya asijerejee! Sijaona tuhuma yoyote ya kutisha ambayo Tundu Lissu hajawahi kuisema ukiacha zinazohusu matukio yaliyotokea baada ya yeye kuwa nje ya nchi. Kwa mfano, hapa akielezea suala la Ben Saanane...



Na usisahau, hiyo ni December 14, 2016... bado watu walikuwa na matumaini ya kumuona Ben!

That's one but two, unless serikali ya JPM na watu wao, iwe through official au rogue agents, kwa interview ile kumgusa Tundu Lissu itakuwa political and diplomatic suicide kwa upande wa serikali!

Endapo Lissu atarejea nchini halafu serikali na watu wao wakamgusa kwa namna yoyote ile, basi yale yote ambayo ameyasema yatapata attention kubwa maradufu na kuaminiwa na kile mtu huko duniani hata kama kuna wengine walikuwa wanamtilia shaka!!

Sana sana mimi ningekuwa ndo serikali yenyewe kwenye maamuzi, ningempa ulinzi wa kutosha ili pamoja na mambo mengine, kuzuia uwezekano wa Flase Flag Assassination or any kind of False Flag Operation.

This false flag operation can be conducted by anyone or any group including rogue agents, not in favor of the government but those who're against the government!

I'm telling you, pale alipo the guy has finally become a radioactive material...

Seriously sijakuelewa! Ulitakaje yaani kwa mfano?! Mimi na wewe tusikiliza interview mbili tofauti au maoni yako unachanganya interview yake kwenye Hard Talk na ile BBC Swahili?

Nilichokiona na kukiskia toka kwa Stephen Sackur kwenye interview ambayo tayari ilikuwa na maswali yake na agenda in advance! Na wala sikumbuki kuona au kusikia open end question ambalo Tundu Lissu angelitumia kuiuza CHADEMA or his future possible presidency!

Halafu, hivi mtu kama Tundu Lissu mnamtaka asifie nini huko ughaibuni?! Kwamba aseme "...lakini pamoja na kunimiminia risasi kadhaa na kutaka kuniua, but on the other side of the coin Magufuli is doing a great job in the so called vita dhidi ya rushwa" wakati mwaka wa tatu unaenda hivi na hatujaona fisadi hata moja miongoni mwa mafisadi wazito wa serikalini waliofikishwa angalau Mahakama ya Mnazi Mmoja!

Yaani mtu unaweza kuamini kwamba, kumbe ufisadi woooooooooooote ambao tumekuwa tukilia nchi hii, mafisadi wakubwa ni Rugemalila na mwenzake Seith na huko serikalini, tangu zama za Mwinyi hadi za JK, wote walikuwa WASAFI, na kama huko serikalini kulikuwa na wezi basi ni wale middle level government officials ndio walikuwa wezi wakubwa na pengine ndio hawa wameficha mabilioni yetu huko Uswisi!

Look, at Steve mwenyewe kashindwa kutoa mfano wa maana wa vita dhidi ya ufisadi zaidi ya kutaja "wafanyakazi hewa!" Hivi kweli kuna mtu anaamini mafisadi wakubwa nchi hii walikuwa wafanyakazi hewa?! Btw, wako wapi wale waliowatengeneza Wafanyakazi Hewa?! How many Maafisa Utumishi waliokuwa sucked kwa kutuletea jeshi la Wafanyakazi Hewa?!
Serikali anayosema ilitaka kumuu ndo impe ulinzi?? Imlinde ili jamii ya kimataifa ijenge imani na serikali?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulisikia nini alichosema kipindi hicho kuhusu yy kwenda kuhojiwa huko?Aliyeleta story za polisi Tanzania haiwez kwenda kumhoji huko Kenya ni nani?Kwanini huyo dereva asirud Tanzania kuhojiwa ila polisi Tanzania ndio wamfuate yeye?Kwanini huyo dereva baada ya kutoka Nairobi asirudi Tanzania na akapelekwa Belgium kutibiwa kisaikolojia na Mwisho tunaambiwa anasoma?Unaambiwa akina Lema ndio wamemtorosha hapa Tz na huko Belgium kwenyewe hana hati zozote za kusafiria toka Tanzania. Aliyekamilisha mipango hiyo ya dereva kwenda huko lengo nini kama kulikua na nia njema ya kusaidia polisi?Hujui shahidi namba moja na mbili ni Lisu na dereva wake na hakuna popote polisi watasema uchunguz umekamilika bila hao watu kuhojiwa?

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
unarukaruka tu
mgonjwa atoke kitandani arudi tanzania kuhojiwa!!!!
tuchukulie lisu na dreva waliuliwa kwwenye tukio,kwa hiyo uchunguzi usingefanyika?
 
Hivi ingalikuwa ni PM ama Rais ndiye kashambuliwa na risasi namna ile halafu "washukiwa" wameenda nje ya nchi na polisi inajua nchi walipo....wangesubiriwa mpaka waamue wenyewe kurejea?

Kwa kifupi, polisi haionekani kama ina nia ya kufanya uchunguzi. Zipo taratibu za kisheria za kimataifa za kushughulikia watuhumiwa wa uhalifu waliopo nchi nyingine. Lakini (kwa bahati mbaya?), polisi hawajazitumia mpaka leo.

Na kwa kweli kama kuna sehemu serikali ilikosea (au ilishindwa kujisafisha) katika sakata la Lissu ni hapo. Hivi ni kweli kwamba uchunguzi haukufanyika kwa sababu dereva wa Lissu hayupo? Hakuna namna nyingine ya kuchunguza? Kweli? Hii mbona ni dharau kubwa kwa jeshi letu la polisi.

Kwa mtu yoyote sane, hatua ambazo polisi walipaswa kuchukua lakini hawajazichukua zinaleta mashaka makubwa. Si kwa sababu hili linamuhusu Lissu, bali hata lingemuhusu mtanzania yeyote mwingine.
Nafikiri huelewi au umeamua kutoelewa ndio maana unakuja na mifano butu. Hao uliowatolea mfano tabia zao zingekuwa kama za lisu ni wazi hamna lolote ambalo lingefanyika. Lisu sio mtuhumiwa, huyu ni shahidi lkn ukiangalia tabia za huyu shahidi zinatia shaka sana na kuna mda naye unaweza mweka kundi la watuhumiwa kama ukiwa SMART. Lisu kama mhanga na anatakiwa kupata haki yake nilitegemea kwa vyovyote vile yeye awe mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa vyombo husika kuhakikisha wahusika wanapatikana. Maajabu mhanga huyu tayar ana watuhumiwa wake kashawapata na kawahukumu. Serikali ifanye nini?Zaidi ni kumsubiri tu kuthibitisha hao aliowahukum kuwa ndio wahusika.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Lissu amesema na kusisitiza USHAHIDI WA KIMAZINGIR A na akatoa mifano, ni mzigo wa anejitetea kufanya hivyo na they WILL NEVER do so, hizi tuhuma hazikuanza leo, wanaogopa wakianza kujibu dots zitaunganishwa, na kama kuna mtu amekashfiwa aende mahakamani, mahakama itamwita lissu
Who is lisu kwamba kila anachoongea ndio sahihi?Eti lisu amesema na kusisitiza hahahahahahah. Kwamba wewe huna lolote la kumhoji lisu?

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Serikali anayosema ilitaka kumuu ndo impe ulinzi?? Imlinde ili jamii ya kimataifa ijenge imani na serikali?

Sent using Jamii Forums mobile app
Unahoji yeye kusema serikali ilitaka kumuua na jambo ambalo ni kweli au unahoji hoja ya serikali kulazimika kutoa ulinzi?! All in all, jibu ni NDIYO lakini sio kwa ajili ya jamii ya kimataifa unless kama umeshindwa kuelewa nilichosema!
 
Nafikiri huelewi au umeamua kutoelewa ndio maana unakuja na mifano butu. Hao uliowatolea mfano tabia zao zingekuwa kama za lisu ni wazi hamna lolote ambalo lingefanyika. Lisu sio mtuhumiwa, huyu ni shahidi lkn ukiangalia tabia za huyu shahidi zinatia shaka sana na kuna mda naye unaweza mweka kundi la watuhumiwa kama ukiwa SMART. Lisu kama mhanga na anatakiwa kupata haki yake nilitegemea kwa vyovyote vile yeye awe mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa vyombo husika kuhakikisha wahusika wanapatikana. Maajabu mhanga huyu tayar ana watuhumiwa wake kashawapata na kawahukumu. Serikali ifanye nini?Zaidi ni kumsubiri tu kuthibitisha hao aliowahukum kuwa ndio wahusika.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Issue ya kushambuliwa Lissu sio la madai bali ni jinai. Kwenye makosa ta jinai, Jamuhuri ndio inayoshitaki. Hii maana yake ni kuwa kisheria aliyeumizwa hawezi kuzuia Jamuhuri kufanya wajibu wake wa kuwawajibisha waliomuumiza. So strictly ni kichekesho kikubwa kusema Lissu ama wafuasi wake wanamkingia kifua mtuhumiwa kwamba hiyo ndio inawafanya polisi wasifanye wajibu wao. Polisi wanapaswa kuwa objective tu. Kama mtu anazuia uchunguzi sheria zipo wazi wanatakiwa wafanye nini. Ndio sababu nasema serikali/polisi wamechemka sana katika suala hili. Ndio sababu imekuwa rahisi kwa wasioipenda kuiangushia zigo la kuhusika kwake.
 
Back
Top Bottom