Kwa Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela - Mwanza

Shagiguku

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
407
133
Habari za leo wanaJF

Ndugu yangu mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela Mwanza, kama mimi ningekuwa ndiyo weye (Mkurugenzi wa Manispaa Ilemela) basi ningemuagiza mhandisi wa manispaa kushughulikia barabara ya National hadi wilayani kwa kujenga mitaro imara ya kusafirisha maji.

Na ningemwagiza aweke makaRavati katika eneo la shule ya msingi Gedeli, Buswelu center na Bondeni ili kuifanya barabara isiharibike kwa maji ya mvua yanayopita juu ya barabara.

Lakini kikubwa kuliko vyote ningeifanya barabara hiyo kupitia fedha za makusanyo ya halmashauri ijengwe kwa kiwango cha lami kuanzia hapo National hadi eneo maarufu la "Mbogamboga" hapo Buswelu center.

Bahati mbaya tu ni kwamba mimi siyo mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela.
 
Hivi hiyo barabara ambayo na mie ni mtumiaji wake wa kila siku, iko chini ya halmashauri au TANROAD? Halafu nilisikia kuwa wamekwama kuweka lami kwa kuwa hawana fedha za kuwahamisha waliojenga karibu na barabara kuanzia hapo mbogamboga hadi kule corner bar!!
 
Kutoka National hadi IGOMBE ni kama kilomita 40 hivi, ina maana Serikali haiwezi kujenga hii barabara kwa kiwango cha lami kwa kutenga sh. Bilioni 10 kila mwezi kwa mkandarasi?

Na hii barabara ya Sabasaba hadi Buswelu nayo bado haijaanza kujengwa kwa lami sijui tatizo ni nini? kila mara ahadi-ahadi...
 
Kutoka National hadi IGOMBE ni kama kilomita 40 hivi, ina maana Serikali haiwezi kujenga hii barabara kwa kiwango cha lami kwa kutenga sh. Bilioni 10 kila mwezi kwa mkandarasi?

Na hii barabara ya Sabasaba hadi Buswelu nayo bado haijaanza kujengwa kwa lami sijui tatizo ni nini? kila mara ahadi-ahadi...


Tuuunganeni kwa pamoja wakazi wa Buswelu Majengo mapya, Nyamadoke, Ilalila, Buteja, Buyombe, Kigala, Bujingwa, Mbogamboga nk kwa kupiga kelele kila siku humu JF ili mkurugenzi asikie kelele zetu.

Namfahamu mkurugenzi ni member humu na hizi post anazisoma saaaana, hivo kwa pamoja tutamfanya achukue hatua.


Na ninaaamini tukipiga "kelele" kwa namna pia ya kutoa ushauri atatuelewa zaidi kwa kuwa yeye ni mtu muelewa.
 
Ni kuondoa tu huyo mbunge wa hapo ilemela,hilo jimbo ni la chadema,

Kazi imemshinda,

Ajiandae kufungasha na kuondoka
 
Bwana Wanga ni jembe sana, mipango iko njiani kukamilisha barabara hizi kwa kiwango cha lami, wala hakuna mwananchi anyekwamisha ujenzi kisa lami, wapo wapiga dili ofisini kwake ndio wanaombabaisha.

Tuungane nae tupige kelele hadi hao wapiga dili waondoke, sie atujengee barabara fidia atatupa badae na tutabomoa wenyewe, sisi shida yetu barabara sio fidia.
 
Wana ilemela tumeshajifunza hatuchagui tena upinzani hawana maono kabisa. Mama Mabula na kijana wetu Mr.Wanga pigeni kazi.
 
Wana ilemela tumeshajifunza hatuchagui tena upinzani hawana maono kabisa. Mama Mabula na kijana wetu Mr.Wanga pigeni kazi.
Harudi tena huyo,

Yeye na mwenzie wa nyamagana.

Mpaka sasa hakuna alichofanya zaidi ya kufungua akaunti za manispaa Facebook na instargram,

Tunamwangalia tu kama shilawadu.

Safari hii kuna makanisa na makasisi tutawaanika
 
Nasikia jamaa wa shirika la Nyumba la taifa wanalalamika kuchangishwa kila siku kufadhili mambo ya ilemela kana kwamba shirika hilo ni mali ya jimbo hilo.....hali hii ikiendelea shirika hilo linaweza kufilisika,kuna mtu ameliganda kama ruba

Pole sana Nehemiah mchechu
 
Habari za leo wanaJF

Ndugu yangu mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela Mwanza, kama mimi ningekuwa ndiyo weye (Mkurugenzi wa Manispaa Ilemela) basi ningemuagiza mhandisi wa manispaa kushughulikia barabara ya National hadi wilayani kwa kujenga mitaro imara ya kusafirisha maji.

Na ningemwagiza aweke makaRavati katika eneo la shule ya msingi Gedeli, Buswelu center na Bondeni ili kuifanya barabara isiharibike kwa maji ya mvua yanayopita juu ya barabara.

Lakini kikubwa kuliko vyote ningeifanya barabara hiyo kupitia fedha za makusanyo ya halmashauri ijengwe kwa kiwango cha lami kuanzia hapo National hadi eneo maarufu la "Mbogamboga" hapo Buswelu center.

Bahati mbaya tu ni kwamba mimi siyo mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela.
shagi upo kaka, salamu zao huko nawamisi.....
 
Kampeni za 2015 ziligharimu karibu bilioni moja,

Kata zilipata karibu milioni 15

Naandaa listi ya wafadhili ambao mpaka sasa wamefilisika .....serikalini hakuna madili tena
 
Hivi halmashauri ya manispaa ya Ilemela imewahi kujenga barabara ya lami hata moja toka imeanzishwa? Hii nchi ya kipumbavu Sana, mtu anakuwa mkurugenzi wa manispaa au jiji busy kujenga mabarabara ya vumbi na matope. Kifuku matope kiangazi vumbi halafu tunaita jiji au manispaa. Nani kasema duniani hapa majiji yanajenga barabara za matope? Only in Tanzania. Tuangalie watu wa kuwapa ukurugenzi wa majiji na manispaa sio kuokoteza tu
 
Bwana Wanga ni jembe sana, mipango iko njiani kukamilisha barabara hizi kwa kiwango cha lami, wala hakuna mwananchi anyekwamisha ujenzi kisa lami, wapo wapiga dili ofisini kwake ndio wanaombabaisha.

Tuungane nae tupige kelele hadi hao wapiga dili waondoke, sie atujengee barabara fidia atatupa badae na tutabomoa wenyewe, sisi shida yetu barabara sio fidia.
Hivi hapa Tanzania kwa wakurugenzi Kuna mpiga dili zaidi ya huyu jamaa? Aliuza Nyumba za Halmashauri pale Ghana next to Rock City Mall akina Kinana wamejenga ghorofa na petrol stations. Huyu weka mbali na fedha
 
Vijana wa mwakilishi wetu wanakula bata China,Mara ujerumani wakati ilemela imejifia kwenye kila idara.

Mwalo hovyo,barabara hovyo,Huduma za afya hovyo,kirumba inahudumiwa na kidispensari cha serikali wakati ina malaki ya watu.

Hakuna mipango ya maendeleo ya akina mama na vijana.

Ni mwendo wa ndege tu,dar mwanza

Ilemela inahitaji mwakilishi sahihi 2020
 
Hivi halmashauri ya manispaa ya Ilemela imewahi kujenga barabara ya lami hata moja toka imeanzishwa? Hii nchi ya kipumbavu Sana, mtu anakuwa mkurugenzi wa manispaa au jiji busy kujenga mabarabara ya vumbi na matope. Kifuku matope kiangazi vumbi halafu tunaita jiji au manispaa. Nani kasema duniani hapa majiji yanajenga barabara za matope? Only in Tanzania. Tuangalie watu wa kuwapa ukurugenzi wa majiji na manispaa sio kuokoteza tu
Mkuu,maeneo ya milimani kulianza kujengwa barabara za mawe chini ya uongozi wa wabunge wa chadema,zilijengwa nyingi na zilisaidia,chini ya hewa wabunge wa ccm wamefuta kabisa ujenzi wa barabara hizo,majimboni hawaonekani,jiji limejaa kero

Enzi ya chadema jiji lilikuwa likigawa Viwanja Mara kwa Mara,chini ya uongozi wa hawa watu,japo wamepewa wizara inayogusa hayo,hakuna wanalofanya zaidi ya kupitapita kwenye vikundi vya akina mama na makanisani(sijui kama wanaendaga kusali kwa maana ya kusali)
 
Barabara hii ni kero kubwa sana kwa wakazi wanaoishi kandokando ya barabara hiyo. Barabara hii iko chini ya TANROADS lakini Mkurugenzi wa Ilemela anatakiwa kuwa mfuatiliaji wa barabara hii ili itengenezwe kwa kiwango cha lami. Mimi nadhani sote tuungane uchaguzi wa 2020 tumpige chini Mbunge wa Ilemela. Tumemueleza sana juu ya kero ya barabara hii lakini hakuna kinachotendeka. Waingereza wanasema enough is enough. Mbunge hatufai hata kidgo.
 
Siku ile Magufuli ametua uwanja wa ndege hapa Mwanza akatoa amri hii barabara ya Airport - Igombe ifunguliwe haraka, naona kila kitu kilikufa, ila ile kauli ilikuwa ni ya kisiasa Zaidi siyo kitaalamu, na ni suala la muda tu hiyo barabara itafungwa, sasa ilikuwa ni jukumu la Manispaa na TANROADS kukutana haraka na kupanga mipango ya kuanza ujenzi wa Barabara hii ya NATIONAL-IGOMBE kwa kiwango cha LAMI ili nauli ishuke kutoka sh. 700 ile ya awali hadi 400 au 500, na hii ndio ilisababisha hadi Rais akatoa amri ya kufunguliwa hii barabara maana wakazi wa maeneo hayo kila siku walikuwa wanatumia sh. 1400 kama nauli kutoka IGOMBE kupitia National hadi mjini, sasa, sijui MKURUGENZI wa MANISPAA ndugu yetu WANGA ameridhika na hali hii au vipi?

Na kwa MANISPAA Ya Ilemela hiyo ndio barabara kero Zaidi inayotunyima usingizi wakazi wa Mwanza, maana watu tuna nyumba zetu huko lakini tumeshindwa kuhamia kutokana na kukosekana usafiri wa UMMA kuja kazini Mjini.

Tafadhari sana ndugu yetu Wanga, kama mipango ya lami bado sana, basi zungumza na SUMATRA ili Hiace zianzie maeneo ya NYAMWILOLELWA -SHIBULA-ILALILA-KAHAMA-BUSWERU-Hadi National-TO mjini, wakati mipango ya lami mkiikamilisha...


Hivi ina maana mapato ya ndani ya manispaa hayawezi kuijenga hii barabara kwa kushirikiana na TANROADS? mambo mengine ni kujiongeza tu si mpaka RAIS aseme, mkishaanza kuijenga ninyi basi serikali kuu itaweka mkono wake kuwasupport, na iwe kweli LAMI siyo kokoto tu Uchafu wa lami.
 
Tuuunganeni kwa pamoja wakazi wa Buswelu Majengo mapya, Nyamadoke, Ilalila, Buteja, Buyombe, Kigala, Bujingwa, Mbogamboga nk kwa kupiga kelele kila siku humu JF ili mkurugenzi asikie kelele zetu.

Namfahamu mkurugenzi ni member humu na hizi post anazisoma saaaana, hivo kwa pamoja tutamfanya achukue hatua.

Na ninaaamini tukipiga "kelele" kwa namna pia ya kutoa ushauri atatuelewa zaidi kwa kuwa yeye ni mtu muelewa.

Kigala ndio mtaa wangu, karibuni wote wana Buswelu tukae pale Lagos
 
Back
Top Bottom