Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Wana JF.
Ni wazi kwamba uozo uliopo kwenye mfumo wetu mzima ni mbovu, alichofanya rais si jambo geni kusukwa upya baraza la mawaziri ni kuongeza ulaji na ufisadi unakithiri, ndivyo itakavyokuwa mara hii.
Rais amesema ataendelea kuwawajibisha maofisa wa Serikali pia, maana yake ni kuwastaafisha kwa manufaa ya umma, kitu ambacho kimekuwa kikifanyika miaka yote, hebu watuambie mpaka sasa ni Mawaziri na Wakurugenzi wangapi wako gerezani wakitumikia vifungo? Wangapi wamefilisiwa mali walizotupora.
Mfumo mzima ni mbovu ndio maana Serikali inatoa misamaha ya kodi ya shilingi zaidi ya trilioni 1.02. Hii ni asilimia 18 ya kodi yote inayokusanywa.
Sio kila kitu rais mpaka kuambiwa na CAG au Kamati ya kudumu kujua uozo uliopo, haiwezekani Serikali itumie Sh544 bilioni bila kuidhinishwa na Bunge, Sh bilioni moja zimelipwa mishahara kwa watumishi hewa na Sh3 bilioni zimetumika katika balozi zetu nje ya nchi. Fedha hizo ziko nje ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge.
Huu ni ubovu wa mfumo mzima wa Serikali hautaondoka kwa kuunda baraza jipya la Mawaziri.
Ni wazi kwamba uozo uliopo kwenye mfumo wetu mzima ni mbovu, alichofanya rais si jambo geni kusukwa upya baraza la mawaziri ni kuongeza ulaji na ufisadi unakithiri, ndivyo itakavyokuwa mara hii.
Rais amesema ataendelea kuwawajibisha maofisa wa Serikali pia, maana yake ni kuwastaafisha kwa manufaa ya umma, kitu ambacho kimekuwa kikifanyika miaka yote, hebu watuambie mpaka sasa ni Mawaziri na Wakurugenzi wangapi wako gerezani wakitumikia vifungo? Wangapi wamefilisiwa mali walizotupora.
Mfumo mzima ni mbovu ndio maana Serikali inatoa misamaha ya kodi ya shilingi zaidi ya trilioni 1.02. Hii ni asilimia 18 ya kodi yote inayokusanywa.
Sio kila kitu rais mpaka kuambiwa na CAG au Kamati ya kudumu kujua uozo uliopo, haiwezekani Serikali itumie Sh544 bilioni bila kuidhinishwa na Bunge, Sh bilioni moja zimelipwa mishahara kwa watumishi hewa na Sh3 bilioni zimetumika katika balozi zetu nje ya nchi. Fedha hizo ziko nje ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge.
Huu ni ubovu wa mfumo mzima wa Serikali hautaondoka kwa kuunda baraza jipya la Mawaziri.