Kwa Lowassa, mwenye macho haambiwi tazama

Kwa Lowassa, mwenye macho haambiwi tazama

kura yangu kwa lowasa....wewe endelea kusubr wanaosema mpaka waoteshwe ndotoooooooooooooo.....miaka mitano kutafsi ndotoooooo....mingne mitano kuhadthia ndotoooooooooooooooooo...........duh kweli siasa zmevamiwa
 
hapo watanzania wanateseka tu...achen kupotea njia machaguo yaliyobak nchi hii ni mawili tu....LOWASA AU SILAHA FULL STOP
 
weeeeeeeeeeeeeeee unayejiita kamundu at nannnnnnnnn vle membeeeeeeeee aongee na wawekezaji wa gesi...mikataba ipo bndng rais wa chna alishapaa nayo baba...kwa taarfa yako miaka 100 hadi 500 utakuwepo....jenga hoja who s Andrew Molel siasa maji taka.....ukipewa kula lakn tumain lililobak nchi hii ni lowasa na silaha tu.............lowasa hana dhiki,watoto wake hawana dhiki wala tamaa.. na ni mtendaji na ni jasri anaamini anachokiamua si kgeugeu...hatutak rais shati 2015 ambaye maamuz atakuwa anafanya RTZ...Upooooooooooooo....VOTE FOR LOWASA 2015
 
Kwa hakika lowassa anaweza, huyu membe kashachelewa kujiandaa na wasiwasi wengi tuliyonayo ni uwezo, wizara anayongoza kwa sasa haina jipya zaidi ya kodi zetu wanazotafuna kwenda nchi ambazo zingine, udhaifu jk aliyonao ndo huohuo membe anao kimsingi watz tusifanye makosa tumpe lowassa hoja ya kuwa tajir au maskin sioni sababu hii nchi tuko nyuma sana na viongozi wetu wamelala usingizi anahitajika lowassa kuwamsha membe atakuwa mzigo zaidi hata ya jk
 
Matatizo makubwa ya Lowassa ni (1) Rushwa- anapenda sana rushwa hivyo akiwa raisi sijui itakuwaje kila kitu kwake ni deal (2) Mbinafsi sana: Vitu vingi anafanya kwa kutafuta sifa na kwa faida za binafsi lakini ni mbinafsi sana. Anasaidia makanisa kwa sifa je kamsadia rafiki yake nani bila kufikiria faida binafsi!. Hata ndugu zake wa Kimasai wakina Mollel wako wapi leo. (3) Anatumia watu kwa faida binafsi- Miradi ya maua Arusha mfano alichukua mkopo na Adrew Mollel yule aliyekuwa na kampuni ya kutengeneza vyakula vya kuku wa Euro 2 million kwa jina na Adrew lakini biashara ilipokufa na kushidwa kulipa mkopo akamkimbia Adrew Mollel na madeni na hata urafiki ukaisha!. (4) Kuna viongozi wazuri zaidi yake kama Pinda, Membe na Migiro ambao wanaweza kuongea na wawekezaji wa mafuta na Gas na kuwaelewa. Lowassa bado hajafika wakati wa kuweza kuja na kujieleza jukwaani ni kwanini wawekezaji waende Tanzania. Pesa ya Tanzania inatatoka kwenye Gas, Tourism, Trade, Gold sasa kwenye haya ukali wa Lowassa utasaidia vipi kama rushwa iko palepele. Je mikataba ya Gas itasaidia vipi Tanzania kama raisi ni mla rushwa namba moja. Kuweka ukali kwa wakuu wa Wilaya haitasaidia hili. Hivyo Lowassa angefaa kuwa mkuu wa polisi lakini sio raisi

Mkuu kula tano. Tunachohitaji hapa siyo kufoka foka bali ni uadilifu na uwezo wa kuuweka uzalendo na maslahi ya umma mbele. Huyu bwana hajawahi kufanya lolote lenye maslahi kwa taifa au umma, zaidi ya kuhonga nyumba za ibada na kuwachinjia ng'ombe wamasai huku wakizidi kupotelea kwenye kazi za ulinzi na ususi.

hata huyo Kagame anayesifiwa kwa ukali wake ni mtu anayejali maslahi kwa umma ni mwadilifu. Lowassa ni wa kuogopa kama ukoma!
 
Mkuu Kaumza,

Me nimekubali sana hayo maandishi yako umeelezea vizuri sana kuhusu Lowassa, na kama hao Wapinzani wake wanasifa kama zake mbona hatuzioni, Jamaa Jembe, Nlikuwa namuuliza jamaa yangu Membe amefanya kipi katika nchi hii kinachomfanya aone anasifa ya kuwa rais ila jamaa alichoniambia ni kuwa eti ni kwa sababu ni waziri wa mambo ya nje na hivyo anasifa ya kuwa rais, tukumbuke kuwa alikuwa naibu waziri wa Migiro so ambaye tungetarajia kutajwa ni Migiro na si yeye kwani yeye hata unaibu aliupata kwa uswaiba na pengine undugu na mukulu ila leo kifua mbele naye urais anautaka.

My take, kama CCM wanaitaji kweli chama kiwe imara ni kwanza kuondoa ukasuku, wivu, fitina na unafiki baina ya viongozi wake. Nasema hivi kwa sababu kwa mtu makini anaweza kung'amua ya kwamba anayeharibu CCM ni wanaccm wenyewe tena viongozi waandamizi ambao wametanguliza maslahi yao mbele kuliko ya chama.

Kumza, ni kitu cha ajabu sana leo kuona kiongozi wa ccm akimwita mwenzake fisadi tena bila uthibitisho ila kumbe nyuma ya pazia ana agenda binafsi.. Yaliyompata Edward yalipangwa na wahusika wanafahamika na hii imekuwa laana hata kwa serikali ya Jakaya, wote tunakumbuka wakati Edu akiwa waziri mkuu spidi ya maisha bora ilionekana ila baada ya kuondoka mambo yakapwaya.

Kingine ni urafiki wa mashaka kati ya Mukulu na Edu kuna kila dalali hawa jamaa hawaelewani, na hii inaonyesha wazi kuwa yale maneno ya Edu aliyoyatoa NEC yanaukweli kuwa hausiki na Richmond na kwanda alishamwambia rais wavunje mkataba ila akasema wavute subira...inawezekana kabsa kwamba muhusika bado yu ndani ya serikali.

Lowassa ni Jembe, anayesema mla Rushwa toa ushahidi kila aliyewahi kufanya naye kazi anamsifia na kila ambaye ameuona utendaji wake unavuta, ni mvumilivu si mropokaji kama wapinzani wake...AKIGOMBEA NITAJITOA MIA KWA MIA KUMPIGIA KAMPANI BUREEEEE.....KWA MANA I AM SURE HE GONNA PROVE PEOPLE WRONG, VIVA EDWARD LOWASSA

Acha kupotosha habari kwa tawkimu zako za kibwege. Membe hajawahi kuwa naibu wa Migiro hata siku moja. Wakati Migiro akiwa waziri, naibu wake alikuwa Cyril Chami na baada ya Migoro kuondoka Membe akachukua nafasi yake.

hivi ushahidi wa rushwa unataka utolewe humu kwenye JF? Angalia mali zake halafu kaangalie alichojaza tume ya maadili uone ambavyo hayuko wazi. Halafu tuambie kwa utumishi wake wa umma na bila kuchukua mikopo benki ametoa wapi fedha zote hizo. Hata Mwalimu alimbaini na hata umuoshe kwa jiwe gani hafai
 
Hivi chanzo cha hii makala ni wapi,kama ni humu Jf,basi mleta uzi anatakiwa apigwe ban kwa kulipotosha bunge.mhe.mods, ninaomba mwongozo hapa tafadhari. Hivi kati ya dr slaa na lowasa ni nani anaeongoza kutajwa humu? Iwe kwa mema au mabaya? Kama si lowasa, futeni huu uzi. Mwandishi,hivi bado unaamini kuwa Jk alikuwa hazina ya taifa hili? Nadhani hata mwinyi leo hii anatamani kuifuta kauli yake hii coz katuletea matatizo. Kama unataka amini Lowasa ni mwizi, subiri CDM ichukue nchi 2015,atafia jela huyu ndg yako.sahivi si analindwa na mwizi mwenzie kesi ya ngedere ummpelekee nyani! Kweli?. Dr slaa is a best choice presdnt.
 
Labda kwa kukusahihisha tu siyo waziri mkuu mstaafu bali ni waziri mkuu aliyejiuzu, pia sidhani kama uliyoeleza yana ukweli saana juu ya el
 
Na kama kwa lowasa mwenye macho haambiwi tazama, mgazeti wote huu wa nini? Si muache wenye macho watazame? Hadanganyiki mtu hapa. Hatuitaki ccm!
 
Lowassa ni fisadi na hana ujasiri wowote ule. Angekuwa na ujasiri angezungumzia rushwa na ufisadi uliokithiri ndani ya CCM na Serikali lakini hata siku moja hawezi kufanya hivyo kwa kuwa yeye mwenyewe ni fisadi hafai kabisa kupewa nafasi ya kugombea Urais 2015.

Huyu ndiye Lowassa au mwingine?
John Daniel
RAIA MWEMA


Toleo la 287
27 Mar 2013

HILI limenisikitisha! Kwa hakika siwezi kukaa kimya bila kushika kalamu yangu kuwasiliana na maelfu ya wasomaji wa gazeti hili la Raia Mwema.
Leo nataka nijikite katika hoja ya Komredi Edward Lowassa, ya wiki iliyopita ya kuwa na wasiwasi kuhusu sekta ya gesi asilia nchini katika wakati ambao nchi haina sera wala sheria inayosimamia sekta hiyo.
Kimsingi kama kauli yake hiyo ya wasiwasi ingetolewa na Mtanzania mwingine wa kawaida asiye na sifa za Lowassa nisingeshangaa kuwa mfumo wa nchi yetu bado hautoi nafasi pana kwa mwananchi wa kijijini kujua kila kinachofanywa na serikali, hata kama kinamuhusu moja kwa moja.

Sifa za Lowassa
Lowassa ni Mbunge wa Monduli, amewahi kuwa Waziri na kufanya vizuri katika sehemu ya utendaji wake serikalini na japo maeneo mengine alivuruga.
Lowassa amewahi kuwa Waziri Mkuu na kipindi chake baadhi ya wakurugenzi wa halmashauri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa na watendaji wengine wa serikali walikuwa wakikesha ofisini kila wanaposikia Lowassa atafanya ziara katika maeneo yao ya kazi.
Pia Lowassa sasa bado ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge wa Mambo ya Nje, nafasi aliyopewa hivi karibuni tu. Kutokana na sifa hizo anaweza kupata taarifa kutoka wizara yoyote kwa urahisi zaidi kuliko hata mimi mwandishi wa habari, ambaye naweza kuzunguka na kisha kuamua kutumia mbinu za uchunguzi ili kupata taarifa sahihi.
Wiki iliyopita Komredi Lowassa aliweka wazi wasiwasi wake kuhusu suala la gesi asilia na kunukuliwa na gazeti moja la kila siku, akitamka hadharani kuwa anapata wasiwasi na uwezekezaji wa sasa katika gesi asilia huku nchi ikiwa haina sera wala sheria.
Kwanza niweke wazi kuwa Komredi Lowassa ni kiongozi aliyepata kushika nyadhifa mbalimbali kama nilivyoanisha hapo awali.
Komredi Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu ambaye ni mtendaji Mkuu wa shughuli za kila siku za serikali bungeni na msaidizi namba mbili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya Makamu wa Rais. Hii ni nafasi kubwa ndiyo ataendelea kuhudumiwa na serikali karibu kila kitu kutokana na wadhifa aliopata kushika na kwa hiyo, kila anapozungumza jambo kauli yake ni muhimu ikapewa uzito Fulani.
Naamini Lowassa anajua mfumo mzima wa serikali, anajua na anaweza kufuatilia kila kitu ndani ya serikali kwa kuwa ana uzoefu, uwezo na sababu ya kufanya hivyo akiamua.

Lowassa na hoja dhaifu
Komredi Lowassa anaposema ana wasiwasi wakati yeye ndiye anayepaswa kuwaondoa wasiwasi Watanzania kuhusu uwekezaji katika sekta hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ambaye wawekezaji wa sekta hiyo anapaswa kuwajua, maana yake ni nini? Kuna ajenda gani?
Hivi kweli Komredi Lowassa hajui kuwa baada ya Waziri wa sasa wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, na Katibu wake Mkuu, Eliakim Maswi kuingia wizarani hapo walikumbana na changamoto kubwa tatu kubwa na hilo la Sera na Sheria ya Gesi ndilo la pili, baada ya umeme wa uhakika kwa taifa?
Nimkumbushe Komredi Lowassa kuwa Sera ya Gesi ilitangazwa katika vyombo karibu vyote vya habari nchini na kilichokwamisha kukosekana kwa kamati husika ya Bunge ili kupitia rasimu hiyo na kisha hatua nyingine ziendelee.
Kiongozi huyo anajua wazi kuwa rasimu hiyo inatakiwa kupitia hatua kuu muhimu nne, kwa mujibu wa taratibu ambazo yeye Komredi Lowassa alishiriki kuziweka akiwa katika nyadhifa zake mbalimbali, ikiwamo nafasi ya Waziri Mkuu.
Hatua hizo ni pamoja na sera kutangazwa katika vyombo vya habari, Kamati ya Bunge kupitia na kuridhia sera hiyo hatua ya tatu ni kuwasilishwa katika kikao cha makatibu wakuu na hatua ya mwisho ni kuwasilishwa katika kikao cha Baraza la Mawaziri.
Komredi Lowassa kwa nafasi yake alipaswa kujua kuwa hatua ya kwanza ya kutangazwa kwa sera ilikwishafanyika, tena kwa kipindi kirefu na baada ya hapo Wizara ikakwama kusubiri uundaji wa Kamati ya Bunge ili iwasilishwe kazi ambayo naamini sasa itakamilika wiki hii, kwa kuwa kamati ipo na inaendelea na kazi.
Nasema haya kwa kuwa ninaamini uchunguzi wangu na taarifa zangu siku zote ni za kweli, sitaki niwe mzungumzaji wa Wizara ya Nishati na Madini na wala sina sababu ya kufanya hivyo, lakini penye ukweli ni lazima nishike kalamu yangu kuelimisha Watanzania wenzangu kujua hali halisi ili twende pamoja kama taifa.
Naamini Komredi Lowassa anatambua wazi kuwa Aprili, mwaka jana (2012) kuna mkataba wa gesi ulitakiwa kusainiwa lakini wizara husika ilisitisha hadi hapo sera na sheria itakapokamilka au hili nalo hajui?
Nilitarajia Komredi Lowassa asimame na kuwaambia Watanzania kamati imepitia mkataba wa kampuni fulani uliyosainiwa tarehe, mwezi na mwaka fulani na kuitaka serikali kusitisha mara moja kwa kuwa sera na sheria zipo katika mchakato wa maandalizi lakini si kusema ana wasiwasi na uwekezaji huo, bila kutoa suluhisho au jibu la mwisho.
Binafsi nimebaini kwamba rasimu ya sheria ya kusimamia sekta ya gesi nchini ipo tayari lakini haiwezi kutolewa kabla ya sera ambayo ilikwama kutokana na sababu za kibunge ambazo Komredi Lowassa ni moja kati ya wajumbe wa Kamati ya Uongozi hivyo ndiye anayestahili kututoa wasiwasi Watanzania badala ya kuonesha wasiwasi.
Nataka nimkumbushe Komredi Lowassa kuwa yeye mwenyewe aliwahi kusimama bungeni na kutamka wazi kuwa ‘tuache kulalamika, tuchukue hatua' leo anarudia yale yale aliyokemea bungeni.
Naamini katika hili Komredi Lowassa alijisahau na anapaswa kujirekebisha kwa kuwa anatukatisha tamaa na kuwafanya Watanzania kuanza kuchambua kauli zake kama kweli zinalenga kujenga au kuna walakini.

Angalizo muhimu kwa wanasiasa
Mara kadhaa tumesikia wanasiasa hususan wabunge wakijaribu kutaka kupaka matope vyombo vya habari kwamba ndivyo vinavyochochea wananchi kuwa na uelewa hasi dhidi ya taifa lao, lakini nadhani wanasiasa ndiyo wanaofanya hivyo tena kwa makusudi.
Vijana wa kizazi hiki wengi hawataki usumbufu, hawapendi kutumia nguvu nyingi kutafuta vitu vya maana ndiyo maana kwenye daladala, pikipiki, migahawa kuna redio lakini ni nadra sana kuwaona wakisikiliza taarifa za habari, zaidi ya muziki asubuhi hadi usiku hivyo ni rahisi kudaka na kuyumbishwa na kauli za viongozi, akiwamo Komredi Lowassa.
Hali hiyo inawafanya vijana wengi kupokea na kuamini chochote watakachosikia bila kufanya utafiti wa kina hivyo kauli kama ya Komredi Lowassa ya kuwa na wasiwasi ni sawa na kuwataka Watanzania kuwa na wasiwasi na hata kukosa imani na Wizara ya Nishati na Madini.
Nashawishika kumshauri Komredi Lowassa kuhakikisha anakuwa na utamaduni wa kufanya utafiti wa kutosha kama kiongozi kabla ya kuzungumza.

Mungu ibariki Tanzania
 
Matatizo makubwa ya Lowassa ni (1) Rushwa- anapenda sana rushwa hivyo akiwa raisi sijui itakuwaje kila kitu kwake ni deal (2) Mbinafsi sana: Vitu vingi anafanya kwa kutafuta sifa na kwa faida za binafsi lakini ni mbinafsi sana. Anasaidia makanisa kwa sifa je kamsadia rafiki yake nani bila kufikiria faida binafsi!. Hata ndugu zake wa Kimasai wakina Mollel wako wapi leo. (3) Anatumia watu kwa faida binafsi- Miradi ya maua Arusha mfano alichukua mkopo na Adrew Mollel yule aliyekuwa na kampuni ya kutengeneza vyakula vya kuku wa Euro 2 million kwa jina na Adrew lakini biashara ilipokufa na kushidwa kulipa mkopo akamkimbia Adrew Mollel na madeni na hata urafiki ukaisha!. (4) Kuna viongozi wazuri zaidi yake kama Pinda, Membe na Migiro ambao wanaweza kuongea na wawekezaji wa mafuta na Gas na kuwaelewa. Lowassa bado hajafika wakati wa kuweza kuja na kujieleza jukwaani ni kwanini wawekezaji waende Tanzania. Pesa ya Tanzania inatatoka kwenye Gas, Tourism, Trade, Gold sasa kwenye haya ukali wa Lowassa utasaidia vipi kama rushwa iko palepele. Je mikataba ya Gas itasaidia vipi Tanzania kama raisi ni mla rushwa namba moja. Kuweka ukali kwa wakuu wa Wilaya haitasaidia hili. Hivyo Lowassa angefaa kuwa mkuu wa polisi lakini sio raisi

Nilikuwa nimeanza kukusoma seriously mpaka pale ulipotaja viongozi wazuri kama Migiro. Huyo mama hayumo kabisa katika kundi hilo. Simpendi Lowassa kama kiongozi lakini kati yake na Migiro Lowassa ni ten times better.
 
Bado mapema Sana kuzungumzia Urais tujenge nchi siasa iwe ya vipindi si kila siku kampeni halafu wenzetu wana piga bao tunalalamika eac hiyoooo Kenya wana take place si mada za kisiasa daily m sorry see my signature below
 
Endeleeni kumpa moyo huku mkichuma pesa zake alizotuibia!! Ikulu ataisoma!! FISADI MKUBWA!!
 
You do not know what you are talking about! Hi dhana ya kumsafisha kiongozi kwa madudu aliyofanya ni ya ajabu kabisa. Ceasar's wife should be beyond suspicion.
 
Back
Top Bottom