Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Public Discourse 1 - Tuwaite Wahujumu Uchumi:
Na. M. M. Mwanakijiji
Ndio tumeamua kuwapachika majina ya uongo na hivyo kuficha uzito wa makosa yao na kwa kuwaita kitu ambacho sicho tumeshiriki kuficha ukali wa uovu wao. Tumeamua kuwabatiza jina la "mafisadi" tukiamini ya kwamba hilo ndilo jina sahihi linaloelezea kile wanachokifanya.
Tumewaita "mafisadi" tukiamini ya kuwa tunataja kosa lao na hivyo kuashiria katika jamii kuwa tumewagundua. Hata hivyo ukweli hauko mbali; kwa kuwaita "mafisadi" tumeshiriki katika kuighiribu jamii kuamini kwanza kabisa kuwa kuna kosa la "ufisadi" na pili tunawaaibisha watu hao kwa kuwaonesha kile wanachofanya.
Hakuna kosa la "ufisadi" nchini, halijawahi kuwepo. Ufisadi kimsingi unahusiana na mambo ya ngono zaidi kuliko kutafsiri neno "corruption" kama wengi tulivyolichukulia. Yawezekana kutokana na kukua kwa lugha neno hilo sasa linakubalika kuelezea mkusanyiko wa tabia zote ambapo mtu katika sekta ya umma na binafsi anatumia nafasi yake kujinufaisha, kuiibia serikali, au kutumia madaraka yake vibaya. Lakini hata ikiwa hivyo "ufisadi" hauelezei kile hasa ambacho kimefanywa na watu mbalimbali ambacho kinaathiri au kimeathiri uchumi wetu na nafasi ya Taifa zima kufanikiwa.
Huko nyuma kuna wimbo (nadhani ni Vijana Jazz wale) unaoitwa "Wanaitwa Matapeli". Wimbo huo ninapoufikiria unaelezea kile ambacho kilidaiwa kufanywa na watu kadhaa ambacho ni kuwauzia watu kanyaboya kwa minajili ya kujipatia fedha bila kutoa huduma au bidhaa halisi. Hivyo watu hawa walipoibuka waliitwa "Matapeli".
Naamini wakati umefika wa kuwaita watu hawa jina wanalostahili, linaloelezea kosa lao la kisheriia na pia kile wanachokifanya dhidi ya nchi yetu. Ndugu zangu watu hawa ni WAHUJUMU UCHUMI kwa mujibu wa sheria ya Kuhujumu Uchumi ya 1984 na mabadiliko yake ya 1987.
Kwa wengine jina hilo linawafanya vinyweleo visimame kwani vinawakumbusha kampeni dhidi ya wahujumu uchumi ya miaka ya themanini. Watu wanaoogopa kuwaita wauza magendo, mchoromchoro, na wanaopenda mwendo wa kuruka kuwa ni wahujumu uchumi. Tumekwepa kuwaita walioiibia Benki Kuu mabilioni ya shilingi kuwa ni Wahujumu Uchumi na badala yake tumewavika mafuta ya "Ufisadi". Tumeshindwa kumuita Chenge Mhujumu uchumi anapohamisha Shilingi Bilioni moja na kuzificha nje ya nchi, tumemuita fisadi tu. Tumeshindwa kuwaita kina Karamagi, Lowassa, Msabaha na kina Gire kuwa ni Wahujumu Uchumi licha ya maamuzi na matendo yao kuathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wetu.
Tumeogopa (sijui sababu nini) kuwaita waliogawiana mali za Taifa letu kama njugu na kumegeana kama viazi nyumba zetu kuwa ni wahujumu uchumi. Kwa kuwaita "mafisadi" tumeficha uovu wao na kuficha kiini cha matendo yao. Ndugu zangu hawa ni wahujumu uchumi na hilo ndilo lililivyo.
Kuwaita "mafisadi" ni kuwavisha cheo cha chini cha uovu na matendo yao. Ni sawa na kumuitwa mwizi "aliyesogeza kitu si chake" au mbakaji "aliyejiridhisha zinaa bilaa ridhaa ya mwingine". Tunapotumia neno "fisadi" kimsingi hatutaki kuita kile ambacho wote naamini tunakifahamu kuwa watu hawa waliokwapua fedha za umma, kufanya maamuzi mabaya kabisa kwenye Taifa letu si kingine isipokuwa ni WAHUJUMU UCHUMI.
Tukiweza kuwapa jina sahihi ndipo hapo tutajua tupambane nao vipi kwani tutakuwa tumedefine adui yetu sawasawa na hivyo kutafuta mbinu sahihi za kupambana naye. Kwa vile hakuna sheria dhidi ya ufisadi ni vigumu kupambana na mafisadi.
Ashukuriwe aliyejuu kuna sheria inayohusiana na "uhujumu uchumi" na ambayo inastahili kutumiwa kwa nguvu zote sasa kupambana na wahujumu uchumi hawa ambao wamejificha kwenye pazia lilioandikwa "Ufisadi". Tuwape jina sahihi, ili tuwashughulikie kwa usahihi. Vinginevyo, tukiendelea kuwaita "Mafisadi" tunaficha uzito wa matendo yao. Nimeamua kuwaita "wahujumu uchumi' kwani hivyo NDIVYO WALIVYO.
Ni mimi,
Mwenzenu,
Ndugu yenu,
Rafiki yenu na kwa wengine
ADUI YENU
M to the THIRD POWER!
Na. M. M. Mwanakijiji
Ndio tumeamua kuwapachika majina ya uongo na hivyo kuficha uzito wa makosa yao na kwa kuwaita kitu ambacho sicho tumeshiriki kuficha ukali wa uovu wao. Tumeamua kuwabatiza jina la "mafisadi" tukiamini ya kwamba hilo ndilo jina sahihi linaloelezea kile wanachokifanya.
Tumewaita "mafisadi" tukiamini ya kuwa tunataja kosa lao na hivyo kuashiria katika jamii kuwa tumewagundua. Hata hivyo ukweli hauko mbali; kwa kuwaita "mafisadi" tumeshiriki katika kuighiribu jamii kuamini kwanza kabisa kuwa kuna kosa la "ufisadi" na pili tunawaaibisha watu hao kwa kuwaonesha kile wanachofanya.
Hakuna kosa la "ufisadi" nchini, halijawahi kuwepo. Ufisadi kimsingi unahusiana na mambo ya ngono zaidi kuliko kutafsiri neno "corruption" kama wengi tulivyolichukulia. Yawezekana kutokana na kukua kwa lugha neno hilo sasa linakubalika kuelezea mkusanyiko wa tabia zote ambapo mtu katika sekta ya umma na binafsi anatumia nafasi yake kujinufaisha, kuiibia serikali, au kutumia madaraka yake vibaya. Lakini hata ikiwa hivyo "ufisadi" hauelezei kile hasa ambacho kimefanywa na watu mbalimbali ambacho kinaathiri au kimeathiri uchumi wetu na nafasi ya Taifa zima kufanikiwa.
Huko nyuma kuna wimbo (nadhani ni Vijana Jazz wale) unaoitwa "Wanaitwa Matapeli". Wimbo huo ninapoufikiria unaelezea kile ambacho kilidaiwa kufanywa na watu kadhaa ambacho ni kuwauzia watu kanyaboya kwa minajili ya kujipatia fedha bila kutoa huduma au bidhaa halisi. Hivyo watu hawa walipoibuka waliitwa "Matapeli".
Naamini wakati umefika wa kuwaita watu hawa jina wanalostahili, linaloelezea kosa lao la kisheriia na pia kile wanachokifanya dhidi ya nchi yetu. Ndugu zangu watu hawa ni WAHUJUMU UCHUMI kwa mujibu wa sheria ya Kuhujumu Uchumi ya 1984 na mabadiliko yake ya 1987.
Kwa wengine jina hilo linawafanya vinyweleo visimame kwani vinawakumbusha kampeni dhidi ya wahujumu uchumi ya miaka ya themanini. Watu wanaoogopa kuwaita wauza magendo, mchoromchoro, na wanaopenda mwendo wa kuruka kuwa ni wahujumu uchumi. Tumekwepa kuwaita walioiibia Benki Kuu mabilioni ya shilingi kuwa ni Wahujumu Uchumi na badala yake tumewavika mafuta ya "Ufisadi". Tumeshindwa kumuita Chenge Mhujumu uchumi anapohamisha Shilingi Bilioni moja na kuzificha nje ya nchi, tumemuita fisadi tu. Tumeshindwa kuwaita kina Karamagi, Lowassa, Msabaha na kina Gire kuwa ni Wahujumu Uchumi licha ya maamuzi na matendo yao kuathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wetu.
Tumeogopa (sijui sababu nini) kuwaita waliogawiana mali za Taifa letu kama njugu na kumegeana kama viazi nyumba zetu kuwa ni wahujumu uchumi. Kwa kuwaita "mafisadi" tumeficha uovu wao na kuficha kiini cha matendo yao. Ndugu zangu hawa ni wahujumu uchumi na hilo ndilo lililivyo.
Kuwaita "mafisadi" ni kuwavisha cheo cha chini cha uovu na matendo yao. Ni sawa na kumuitwa mwizi "aliyesogeza kitu si chake" au mbakaji "aliyejiridhisha zinaa bilaa ridhaa ya mwingine". Tunapotumia neno "fisadi" kimsingi hatutaki kuita kile ambacho wote naamini tunakifahamu kuwa watu hawa waliokwapua fedha za umma, kufanya maamuzi mabaya kabisa kwenye Taifa letu si kingine isipokuwa ni WAHUJUMU UCHUMI.
Tukiweza kuwapa jina sahihi ndipo hapo tutajua tupambane nao vipi kwani tutakuwa tumedefine adui yetu sawasawa na hivyo kutafuta mbinu sahihi za kupambana naye. Kwa vile hakuna sheria dhidi ya ufisadi ni vigumu kupambana na mafisadi.
Ashukuriwe aliyejuu kuna sheria inayohusiana na "uhujumu uchumi" na ambayo inastahili kutumiwa kwa nguvu zote sasa kupambana na wahujumu uchumi hawa ambao wamejificha kwenye pazia lilioandikwa "Ufisadi". Tuwape jina sahihi, ili tuwashughulikie kwa usahihi. Vinginevyo, tukiendelea kuwaita "Mafisadi" tunaficha uzito wa matendo yao. Nimeamua kuwaita "wahujumu uchumi' kwani hivyo NDIVYO WALIVYO.
Ni mimi,
Mwenzenu,
Ndugu yenu,
Rafiki yenu na kwa wengine
ADUI YENU
M to the THIRD POWER!