Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:
Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki
Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:
Sijui inawezekana kuwa sasahivi:
JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?
Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.