Kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na ya kwake anayotenda, kutomshukuru ni kujichumia tu dhambi za bure!

Kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na ya kwake anayotenda, kutomshukuru ni kujichumia tu dhambi za bure!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,718
Wanabodi

Naomba kuanza na Angalizo:
Mada kama hizi ni mada za kiutu uzima, hakuna kutaja taja majina ya watu wowote humu!, na ukijiona una washwa washwa kutaka kutaja majina hapa, au kuuliza ni nani, ujijue huu uzi sii saizi yako!, nakuomba jipitie tuu kwenda kwenye nyuzi za kimo chako!, sio lazima kuchangia kila uzi!.

Ada ya Mja Hunena, Muungwana ni Kitendo, Kwa Makubwa Aliyoyatenda, haja ya kupiga tarumbeta kumnenea, tuyaache matokeo yatamnenea!, tena hakuna hata haja ya kumsukuma mlevi! anayesema hakujafanyika kitu!.

Mimi mwenzenu, sio tuu nimepiga kura toka uchaguzi wa mwaka 1990 ambao ndio uchaguzi wa mwisho wa chama kimoja!, kwenye urais, tulikuwa tunampigia kura mgombea mmoja anayeshindana na kivuli!

Nimeshiriki nikiwa mwandishi wa habari na kuna wakati nilikuwa mwangalizi, na niliendelea kushiriki chaguzi zote za vyama vingi, toka ule uchaguzi mdogo wa jimbo la Kwahani, 1994, uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, 2020, na sasa 2025, hivyo kuna vitu niliviona naweza kuvitolea ushauri wa busara, kwa kuviandika, vinaweza kusaidia jambo kuelekea uchaguzi wa 2025 huku nikiwafunza vijana wa leo, busara zilizomo ndani ya ngano za lugha yetu adhimu ya Kiswahili. Wakati wetu tulifundishwa hadithi, vitendawili, nahau, na tamathali za semi.

Mada ya leo ni ya tamathali za semi hii ya Kiswahili isemayo "Ada ya Mja Hunena, Muungwana ni Kitendo“, ni sawa na ile semi inayosema "Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno"

Ada ya mja hunena, ada ni matendo, mja ni mtu, kiumbe wa Mwenyeezi Mungu, Ada ya mja hunena, ni matendo ya mtu anayotenda yananena, yana sauti, yana msemea, badala ya mtu kusema kwa maneno, nimefanya hiki au nimefanya kile, wewe tenda, fanya kitu cha kuonekanikani, halafu matokeo ya matendo yako, au matokeo ya ulichokifanya ndio yakusemee!, ukifanya jambo jema zuri la kuonekanika, huna haja ya kusema, umefanya nini, acha watu waone kilichofanyika, halafu hicho kilichofanyika ndio kinakuenea. Neno muungwana ni kitendo sio kauli au maneno "mimi muungwana", tenda uungwana, halafu hayo matendo yako ya uungwana au kiungwana ndio yakunenea na kukusemea, fulani ni muungwana!.

Binadamu siku zote, huwa hawana mema, sio watu wote ni watu wema, kuna wengine ni mahasisidi, hasidi huwa hana sababu!, kuna watu sio wana wema, hata uwatendee mema makubwa kiasi gani, ipo siku, watakutenda tuu!, ndio maana. Waswahili wanamsemo wa "Tenda wema uende zako, usisubirie shukrani", na mahali penye wema, kuna msemo, “pema usijapo pema, ukipema, sii pema tena”, ukitenda jambo jema, usijisifu kwa jema hilo, ukijisifu, hilo jema litatafutiwa ubaya!.

Nimeleta mada hii baada ya kuangalia mubashara kupitia TBC, uzinduzi wa daraja la JPM, Kigongo - Busisi, nikakumbuka daraja la Tanzanite, nikakumbuka flyover ya Tazara, Interchange ya Ubungo, Mradi wa JNHPP, nikakumbuka reli ya SGR, serikali kuhamia Dodoma, Ikulu ya Chamwino, mashule, mahospitali, mabarabara kibao, midege ya ATCL tulioinunua kwa kupiga tanchi!, na maendeleo mengine mengi makubwa ya kuonekanika, nikajisemea kimoyo moyo, “kiukweli Yule Kaka yangu, alikuwa na uthubutu mkubwa!, kuna baadhi aliyatekeleza wala hayakuwemo kwenye ilani, ila pia kuna yaliyokuwemo kwenye ilani, akaachana nayo kwasababu sio kipaumbele chake.

Pamoja na wema wote huo, ulipofika muda wa kutwaliwa, Kaka alitwaliwa na Dada akaingia na kukamilisha yale mema makubwa mazuri ya kuonekanika anayoyatenda mja huyu aliyepo sasa, kwanza kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na ya kwake anayotenda, kiukweli kabisa, matendo yake yamekidhi haja maridhawa kuiko maneno!, hivyo Watanzania tuwe waungwana, anastahili kushukuriwa kwa kupewa shukrani ya asante stahiki!.

Kitendo cha mtu kufanyiwa wema mkubwa hivi, halafu kuwa mtovu wa fadhila, kuwa mtovu wa shukrani, kutomshukuru mtu kama huyu ni kujichumia tuu bure ile dhambi! ya utovu wa fadhila na utovu wa shukrani!

Watanzania walio wengi ni waungwana sana, ni wastaarabu sana, na ni watu wa shukrani na kukumbuka fadhila, sio watovu wa shukrani kivile!, hivyo utakapo wadia ule muda wa kutoa shukrani, Watanzania watampatia shukrani zake stahiki!.

Wakati wote, mema haya, makubwa na mazuri haya yakiendelea, kuna walevi, wamelewa na wanaiga kelele sana kuwa hakuna chochote kilichofanyika!, kuna msemo mwingine wa Kiswahili, unaitwa "kumsukuma mlevi". Unamuona mlevi amelewa chakari, anatembea kwa kuyumba yumba, yaani ni amelewa tilalila!, ukimsukuma kidogo tuu, ni anakwenda chini, na jinsi pombe zilivyomzidia, akienda chini, anaweza hata kudondoka mtaroni, akashindwa kuinuka ikawa ndio mtolee!, mtu ameondoka jumla!.

Kufuatia shukrani za Watanzania kwa mja huyu, kwa kilichofanyika, hakuna kabisa sababu ya kumsukuma huyu mlevi, mja wetu, usimsukume kabisa, huyu mlevi, mwache aendelee kutembea kwa kupepesuka na pombe zake, atajiangukia mwenyewe, bora lawama za kutomsaidia mlevi kwa kumwacha akapepesuka hadi akaanguka mwenyewe, kuliko fedheha ya kumsukuma mlevi akaanguka, na ile anguka yake ikawa ni ile anguka ya mtolee!. Lawama utabebeshwa wewe kwa kumsukuma!.

Asante stahiki kwa huyu mja aliyepo ni ile asante ya ile siku ya siku, ni unachukua, unaweka, !, ..

Hivyo namshauri aliyepo, awape tuu kila wanachokitaka, hata kama hawastahili, ali mradi, wameomba, wanapiga makelele sana, yanatukosesha usingizi, wapewe tuu!

Wasipopewa, baada ya Watanzania kuonyesha shukrani zao kwa yaliyofanyika, mtakuwa mmewapa uhalali wa lile jambo letu lile, watasema yule aliyepita sio amepita kwasababu alistahili, watadai ni amepita kwasababu, amesimama na vivuli, mshindani wa ukweli, amefanyiwa figisu ya kubambikiwa kesi mbaya ili kuhalalisha kumhifadhi pahala salama kupisha jambo letu, hivyo aliyeshinda, ameshinda kwasababu ameshindanishwa na kivuli, au vivuli!.

Naendelea kushauri, kale ka simba ka Kizimkazi, kaondolewe tuu kwenye ile cage, katatusumbua sana kwa kupigiwa kelele kutoka karibu kila kona!.

Hebu tuwape tuu wanachotaka, tuingie uwanjani kwenye uwanja ulio sawa, ( a level playing field), tuboreshe kanuni za mchezo kwa fair play, tuweke refa mtenda haki, mwisho wa mchezo, mshindi apatikane kwa haki, tufurahie ushindi wa haki, tena kwa hisia zangu, hizi mambo za figisu, zinaweza kuwa ndio zimechagia kwenye ile karma iliyopelelekea lile tukio lile kutokea!, tusipojirekebisha hii 2025, tukio kama lile linaweza kuja kujirudia!.

Mwenye macho na aone,
Mwenye masikio asikie!

Mungu Ibariki Tanzania.

Mzee Pasco
 
Pasco tunakubali wao ni chama kubwa, wamefanya mengi, muda wote wako serikalini. Sawa.

Lakini mbona hawataki uchaguzi ulio huru na wa haki ?!. Mbona wanautaka uchaguzi wanaoudhibiti wao dhidi ya washindani wao !!

Unaweza kuwa umefanya mengi Lakini haturidhiki na utendaji wako. Tunadhani kuna wanaoweza kufanya vizuri zaidi. Tunachotaka ni Tume huru ya uchaguzi na mahakama zilizo huru dhidi ya serikali kuu.
 
Wanabodi

Mimi mwenzenu, sio tiu nimepiga kura toka uchaguzi wa mwaka 1990 ambao ndio uchaguzi wa mwisho wa chama kimoja!, kwenye urais, tulikuwa tunampigia kura mgombea mmoja anayeshindana na kivuli!

Nimeshiriki nikiwa mwandishi wa habari na kuna wakati nilikuwa mwangalizi, na niliendelea kushiriki chaguzi zote za vyama vingi, toka ule uchaguzi mdogo wa jimbo la Kwahani, 1994, uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, 2020, na sasa 2025, hivyo kuna vitu niliviona naweza kuvitolea ushauri wa busara, hivyo naanzisha mfululizo wa mada zangu za busara za Mzee Pasco.

Mada hizi ni za kiutu uzima, hakuna kutaja taja majina!, na ukijiona unataka kuuliza ni nani au kutaja jina, ujue huu uzi sii saizi yako!.

Mada ya kwanza usemi wa Kiswahili usemao "Haja ya Mja Hunena, Muungwana ni Kitendo" Kumaanisha binadamu wote sio wema, hata uwatendee mema makubwa kiasi gani, ipo siku, atakutenda tuu!, ndio maana. Waswahili wanamsemo wa "Tenda wema uende zako, usisibirie shukrani".

Leo nilikuwa naangalia mubashara kupitia TBC, uzinduzi wa Daraja la JPM, Kigongo- Busisi, nikakumbuka daraja la Tanzanite, nikakumbuka flyover ya Tazara, Interchange ya Ubungo, Mradi wa JNHPP, nikakumbuka reli ya SGR, serikali kuhamia Dodoma, Ikulu ya Chamwino, mashule, mahospitali, mabarabara kibao, nikajisemea kiukweli Jamaa alikuwa na uthubutu!. Pamoja na wema wote huo, ulipofika muda wa watu kufanya uamuzi, amini usiamini, kuna maeneo watu walimtenda!, ikabidi utumike ule utaratibu wetu ule wa ku nanilii, kama alivyosema Nape!.

Sasa kwa mema makubwa mazuri ya kuonekanika anayoyatenda huyu aliyepo, kwanza kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na yake anayotenda, kiukweli kabisa, anastahili kushukuriwa kwa kupewa asante stahiki!.

Kitendo cha mtu kufanyiwa wema mkubwa hivi, halafu kuwa mtovu wa fadhila, kuwa mtovu wa shukrani, kutomshukuru mtu kama huyu ni kujichumia tuu dhambi! ya utovu wa fadhila na utovu
wa shukrani.

Watanzania sio watovu wa shukrani kivile!.

Kuna msemo mwingine wa
Kiswahili, unaitwa "kumsukuma mlevi". Unamuona mlevi amelewa chakari, anatembea kwa kuyumba yumba, yaani ni amelewa tilalila!, ukimsukuma kidogo tuu, ni anakwenda chini, na jinsi pombe zilivyomzidia, akienda chini, inaweza kuwa jumla!.

Kufuatia shukrani za Watanzania kwa kilichofanyika, hakuna kabisa sababu ya kumsukuma huyu mlevi, usimsukume kabisaa, huyu mlevi, mwache aendelee kutembea kwa kupepesuka, atajiangukia mwenyewe, bora lawama za kutomsaidia mlevi akaanguka, kuliko fedheha ya kumsukuma mlevi akaanguka ile ya mtolee!.

Asante stahiki kwa huyu aliyepo ni ile asante ya ile siku ya unachukua, unaweka, !, hivyo namshauri aliyepo, awape tuu kila wanachokitaka, hata kama hawastahili, ali mradi, wameomba, wanapiga makelele, wapewe tuu!

Wasipopewa, baada ya Watanzania kuonyesha shukrani zao kwa yaliyofanyika, mtakuwa mmewapa uhalali wa lile jambo letu lile, watasama yule aliyepita sio amepita kwasababu alistahili, ni amepita kwasababu, mshindani wa ukweli, amefanyiwa figisu ya kubambikiwa kesi mbaya ili kuhalalisha kumhifadhi pahala salama kupisha jambo letu, hivyo aliyeshinda, ameshinda kwasababu ameshindanishwa na kivuli, au vivuli!.

Naendelea kushauri, kale ka simba ka Kizimkazi, kaondolewe kwenye ile cage, katatusumbua sana kwa kelele!.

Tuwape wanachotaka, tungie uwanjani kwenye a level playing field, tuweke refa mtenda haki, mwisho wa mchezo, mshindi apatikane kwa haki, tufurahie ushindi wa hakia, tena kwa hisia zangu, hizi mambo za figisu, zimechagia kwenye ile karma iliyopelelekea lile tukio!.

Mwenye macho na aone,
Mwenye masikio asikie!

Mzee Pasci
Zaidi ya trillion 40 zimekopwa ndani ya miaka 4. Zimekwenda wapi ikiwa Miradi yote kaikuta imeenza kujengwa? Toka uhuru mpaka mwaka 2021 nchi ilikuwa imekopa chini ya trillion 60. Je tukimuita tapeli na fisadi Kuna ubaya Gani?
 
Hakuna cha kupewa wala cha nini hapa. Kama wao CHADEMA wanataka kususa uchaguzi acha wasusie tu na hakuna cha kuwabembeleza wala wa kuwabembeleza . Pia ningependa kukwambia ya kuwa RAIS Samia hana Mpinzani wa kushindana naye wala wa kushindanishwa naye katika sanduku la kura . Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka Marekani bado CCM na Rais Samia atashinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.

Kitu kingine ningekushauri Ndugu yangu Paschal Mayallay Kuwa Embu Jaribu kunyooka kimsimamo na usiwe vuguvugu wala moto. Usipende kupuliza na kuuuma kama panya. pia unapoandika ujue unawaandikia watu wazima wenye akili Timamu na wenye kujielewa. Kwa hiyo usiwe unaandika kwa kuzunguka zunguka sana na kupaka paka rangi.

Pili ningekusihi uache kuandika habari za vitisho au kutisha au kuonyesha kwamba jambo fulani lisipofanyika basi ni lazima litatokea jambo fulani. Uache habari sijui za Karma na madubwasha ya aina hiyo kana kwamba wewe ni Mungu na una maagano na Mungu.

Lakini pia usipende kuhusianisha habari za Kifo cha Hayati Dkt Magufuli na habari sijui za kusema hakusikiliza jambo hili ndio maana akapatwa na jambo hili kama Karma.

Uhai wa mtu upo Mikononi Mwa Mungu Mwenyewe. Usipende kujiweka katika mzani wa Utimilifu kana kwamba usemacho wewe kimetoka kwa Mungu mwenyewe na kushushiwa wewe Kama Nabii Musa ili ukileta Duniani. Nafuatilia sana maandiko yako humu jukwaani lakini nilishagundua wewe ni mtu ambaye ulitamani Rais Samia asiendelee kuwa Rais baada ya 2025. Yapo maandishi humu jukwaani yenye kuonyesha hivyo. Kuna wakati ukawa unaandika hadi kuwa ikiwezekana mara sijui amuachie nani . Mara ukaja na habari zako sijui umeonyeshwa kuwa Dkt Philipo mpango ndio Mpango wenyewe mara ukaja na makala sijui Dkt Husseni Mwingi ndiye ajae. yaani ukawa ni vurugu vurugu ilimradi tu kutaka kuchora picha na taswira ya kutaka RAIS Samia akwame na asipewe nafasi ya kugombea Uraisi.

Lakini pia Paschal Mayallal kabla ya 2015 ukiandika makala nyingi sana humu jukwaani za kutushambulia,kutujeruhi na kutuboa CCM mpaka kufikia hatua kuonyesha kuwa wenye kuichagua CCM ni wale wasiojitambua. Lakini cha ajabu 2020 ukataka upewe nafasi ya kugombea ubunge kwa chama kilekile ambacho ulikijeruhi ,kukiumiza na kukibomoa kwa karamu yako.

Usiwe kama kinyonga . Kuwa na msimamo na usiwe kama panya wa kuuma na kupuliza. Nyooka na ueleweke msimamo wako ni upi. Siyo kuleta habari zako za sijui sheria hizi na hizi ni batili na hivyo uchaguzi utakuwa sijui haramu. Tena ikiwezekana chukua kadi ya CHADEMA ili uwe huru kabisa kugombea na kuongea mtizamo wako uwapo kwenye majukwaa ya kisiasa na siyo kufanya kuleta ukinyonga.
 
Asoshukuru hana fadhila. Mkuu kajitahidi japo dosari hazikosekanagi lakini miradi kaikamilisha,
Naamini ana wasaidizi je wanashindwa kushauri mambo mema ya haki na akili.
Umeeleweka loud and clear. Japo wahafidhina na machawa wanaolinda ugali wao ndani ya.chama hawapendi kusikia ushauri kama wako hasa kuhusu simba in the cage to be freeid.
 
Mzee unatafuta teuzi, ila ni muda sasa mfumo ukuone aisee
Kinondoni huu ni mwezi wa tatu hakuna maji, na hii haijawai kutokea kwa miaka hii karibuni
 
Mn
Hakuna cha kupewa wala cha nini hapa. Kama wao CHADEMA wanataka kususa uchaguzi acha wasusie tu na hakuna cha kuwabembeleza wala wa kuwabembeleza . Pia ningependa kukwambia ya kuwa RAIS Samia hana Mpinzani wa kushindana naye wala wa kushindanishwa naye katika sanduku la kura . Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka Marekani bado CCM na Rais Samia atashinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.

Kitu kingine ningekushauri Ndugu yangu Paschal Mayallay Kuwa Embu Jaribu kunyooka kimsimamo na usiwe vuguvugu wala moto. Usipende kupuliza na kuuuma kama panya. pia unapoandika ujue unawaandikia watu wazima wenye akili Timamu na wenye kujielewa. Kwa hiyo usiwe unaandika kwa kuzunguka zunguka sana na kupaka paka rangi.

Pili ningekusihi uache kuandika habari za vitisho au kutisha au kuonyesha kwamba jambo fulani lisipofanyika basi ni lazima litatokea jambo fulani. Uache habari sijui za Karma na madubwasha ya aina hiyo kana kwamba wewe ni Mungu na una maagano na Mungu.

Lakini pia usipende kuhusianisha habari za Kifo cha Hayati Dkt Magufuli na habari sijui za kusema hakusikiliza jambo hili ndio maana akapatwa na jambo hili kama Karma.

Uhai wa mtu upo Mikononi Mwa Mungu Mwenyewe. Usipende kujiweka katika mzani wa Utimilifu kana kwamba usemacho wewe kimetoka kwa Mungu mwenyewe na kushushiwa wewe Kama Nabii Musa ili ukileta Duniani. Nafuatilia sana maandiko yako humu jukwaani lakini nilishagundua wewe ni mtu ambaye ulitamani Rais Samia asiendelee kuwa Rais baada ya 2025. Yapo maandishi humu jukwaani yenye kuonyesha hivyo. Kuna wakati ukawa unaandika hadi kuwa ikiwezekana mara sijui amuachie nani . Mara ukaja na habari zako sijui umeonyeshwa kuwa Dkt Philipo mpango ndio Mpango wenyewe mara ukaja na makala sijui Dkt Husseni Mwingi ndiye ajae. yaani ukawa ni vurugu vurugu ilimradi tu kutaka kuchora picha na taswira ya kutaka RAIS Samia akwame na asipewe nafasi ya kugombea Uraisi.

Lakini pia Paschal Mayallal kabla ya 2015 ukiandika makala nyingi sana humu jukwaani za kutushambulia,kutujeruhi na kutuboa CCM mpaka kufikia hatua kuonyesha kuwa wenye kuichagua CCM ni wale wasiojitambua. Lakini cha ajabu 2020 ukataka upewe nafasi ya kugombea ubunge kwa chama kilekile ambacho ulikijeruhi ,kukiumiza na kukibomoa kwa karamu yako.

Usiwe kama kinyonga . Kuwa na msimamo na usiwe kama panya wa kuuma na kupuliza. Nyooka na ueleweke msimamo wako ni upi. Siyo kuleta habari zako za sijui sheria hizi na hizi ni batili na hivyo uchaguzi utakuwa sijui haramu. Tena ikiwezekana chukua kadi ya CHADEMA ili uwe huru kabisa kugombea na kuongea mtizamo wako uwapo kwenye majukwaa ya kisiasa na siyo kufanya kuleta ukinyonga.
Mnapenda sana kusifiwa na kuabudiwa, so ikitokea mtu kaongea kisichowafurahisha hata kama ni kweli mnafura kweli. Inawezekana ameamua kuacha uchawa, kwa nini unataka umpangie cha kusema. We si ufanye mambo yako na yeye umwache afanye mambo yake? Wanaoichagua CCM ni kweli hawana akili, ndo maana wanarubuniwa na buku ten ten wanabebwa kwenye malori, mpaka wengine walikufa. Sheria zinakataza kubeba watu kwenye malori kama abiria, nyie mnawabeba tu kama mikungu ya ndizi halafu mnataka watu wakae kimya? Mpina angemsifia Rais angemjibu kama alivyomjibu, Simiyu na Wilaya zake na Majimbo yake ndo vinaongoza kwa umasikini Tanzania? Ulitaka aseme kwamba mama ametufikia? Watu wa hovyo kabisa nyie
 
Hakuna cha kupewa wala cha nini hapa. Kama wao CHADEMA wanataka kususa uchaguzi acha wasusie tu na hakuna cha kuwabembeleza wala wa kuwabembeleza . Pia ningependa kukwambia ya kuwa RAIS Samia hana Mpinzani wa kushindana naye wala wa kushindanishwa naye katika sanduku la kura . Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka Marekani bado CCM na Rais Samia atashinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.

Kitu kingine ningekushauri Ndugu yangu Paschal Mayallay Kuwa Embu Jaribu kunyooka kimsimamo na usiwe vuguvugu wala moto. Usipende kupuliza na kuuuma kama panya. pia unapoandika ujue unawaandikia watu wazima wenye akili Timamu na wenye kujielewa. Kwa hiyo usiwe unaandika kwa kuzunguka zunguka sana na kupaka paka rangi.

Pili ningekusihi uache kuandika habari za vitisho au kutisha au kuonyesha kwamba jambo fulani lisipofanyika basi ni lazima litatokea jambo fulani. Uache habari sijui za Karma na madubwasha ya aina hiyo kana kwamba wewe ni Mungu na una maagano na Mungu.

Lakini pia usipende kuhusianisha habari za Kifo cha Hayati Dkt Magufuli na habari sijui za kusema hakusikiliza jambo hili ndio maana akapatwa na jambo hili kama Karma.

Uhai wa mtu upo Mikononi Mwa Mungu Mwenyewe. Usipende kujiweka katika mzani wa Utimilifu kana kwamba usemacho wewe kimetoka kwa Mungu mwenyewe na kushushiwa wewe Kama Nabii Musa ili ukileta Duniani. Nafuatilia sana maandiko yako humu jukwaani lakini nilishagundua wewe ni mtu ambaye ulitamani Rais Samia asiendelee kuwa Rais baada ya 2025. Yapo maandishi humu jukwaani yenye kuonyesha hivyo. Kuna wakati ukawa unaandika hadi kuwa ikiwezekana mara sijui amuachie nani . Mara ukaja na habari zako sijui umeonyeshwa kuwa Dkt Philipo mpango ndio Mpango wenyewe mara ukaja na makala sijui Dkt Husseni Mwingi ndiye ajae. yaani ukawa ni vurugu vurugu ilimradi tu kutaka kuchora picha na taswira ya kutaka RAIS Samia akwame na asipewe nafasi ya kugombea Uraisi.

Lakini pia Paschal Mayallal kabla ya 2015 ukiandika makala nyingi sana humu jukwaani za kutushambulia,kutujeruhi na kutuboa CCM mpaka kufikia hatua kuonyesha kuwa wenye kuichagua CCM ni wale wasiojitambua. Lakini cha ajabu 2020 ukataka upewe nafasi ya kugombea ubunge kwa chama kilekile ambacho ulikijeruhi ,kukiumiza na kukibomoa kwa karamu yako.

Usiwe kama kinyonga . Kuwa na msimamo na usiwe kama panya wa kuuma na kupuliza. Nyooka na ueleweke msimamo wako ni upi. Siyo kuleta habari zako za sijui sheria hizi na hizi ni batili na hivyo uchaguzi utakuwa sijui haramu. Tena ikiwezekana chukua kadi ya CHADEMA ili uwe huru kabisa kugombea na kuongea mtizamo wako uwapo kwenye majukwaa ya kisiasa na siyo kufanya kuleta ukinyonga.
Chawa acha kupanick, huyo mkongwe anajua kwa sasa ccm hamna uwezo wa kushinda tena kwa uchaguzi halali. Anauma na kupuuliza maana ukweli anaujua, na anajua akiusema ni hatari kwa maisha yake. Naona unaogopa ccm ikitoka madarakani shughuli zako haramu zitakwamwa.
 
Wanabodi

Mimi mwenzenu, sio tiu nimepiga kura toka uchaguzi wa mwaka 1990 ambao ndio uchaguzi wa mwisho wa chama kimoja!, kwenye urais, tulikuwa tunampigia kura mgombea mmoja anayeshindana na kivuli!

Nimeshiriki nikiwa mwandishi wa habari na kuna wakati nilikuwa mwangalizi, na niliendelea kushiriki chaguzi zote za vyama vingi, toka ule uchaguzi mdogo wa jimbo la Kwahani, 1994, uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, 2020, na sasa 2025, hivyo kuna vitu niliviona naweza kuvitolea ushauri wa busara, hivyo naanzisha mfululizo wa mada zangu za busara za Mzee Pasco.

Mada hizi ni za kiutu uzima, hakuna kutaja taja majina!, na ukijiona unataka kuuliza ni nani au kutaja jina, ujue huu uzi sii saizi yako!.

Mada ya kwanza usemi wa Kiswahili usemao "Haja ya Mja Hunena, Muungwana ni Kitendo" Kumaanisha binadamu wote sio wema, hata uwatendee mema makubwa kiasi gani, ipo siku, atakutenda tuu!, ndio maana. Waswahili wanamsemo wa "Tenda wema uende zako, usisibirie shukrani".

Leo nilikuwa naangalia mubashara kupitia TBC, uzinduzi wa Daraja la JPM, Kigongo- Busisi, nikakumbuka daraja la Tanzanite, nikakumbuka flyover ya Tazara, Interchange ya Ubungo, Mradi wa JNHPP, nikakumbuka reli ya SGR, serikali kuhamia Dodoma, Ikulu ya Chamwino, mashule, mahospitali, mabarabara kibao, nikajisemea kiukweli Jamaa alikuwa na uthubutu!. Pamoja na wema wote huo, ulipofika muda wa watu kufanya uamuzi, amini usiamini, kuna maeneo watu walimtenda!, ikabidi utumike ule utaratibu wetu ule wa ku nanilii, kama alivyosema Nape!.

Sasa kwa mema makubwa mazuri ya kuonekanika anayoyatenda huyu aliyepo, kwanza kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na yake anayotenda, kiukweli kabisa, anastahili kushukuriwa kwa kupewa asante stahiki!.

Kitendo cha mtu kufanyiwa wema mkubwa hivi, halafu kuwa mtovu wa fadhila, kuwa mtovu wa shukrani, kutomshukuru mtu kama huyu ni kujichumia tuu dhambi! ya utovu wa fadhila na utovu
wa shukrani.

Watanzania sio watovu wa shukrani kivile!.

Kuna msemo mwingine wa
Kiswahili, unaitwa "kumsukuma mlevi". Unamuona mlevi amelewa chakari, anatembea kwa kuyumba yumba, yaani ni amelewa tilalila!, ukimsukuma kidogo tuu, ni anakwenda chini, na jinsi pombe zilivyomzidia, akienda chini, inaweza kuwa jumla!.

Kufuatia shukrani za Watanzania kwa kilichofanyika, hakuna kabisa sababu ya kumsukuma huyu mlevi, usimsukume kabisaa, huyu mlevi, mwache aendelee kutembea kwa kupepesuka, atajiangukia mwenyewe, bora lawama za kutomsaidia mlevi akaanguka, kuliko fedheha ya kumsukuma mlevi akaanguka ile ya mtolee!.

Asante stahiki kwa huyu aliyepo ni ile asante ya ile siku ya unachukua, unaweka, !, hivyo namshauri aliyepo, awape tuu kila wanachokitaka, hata kama hawastahili, ali mradi, wameomba, wanapiga makelele, wapewe tuu!

Wasipopewa, baada ya Watanzania kuonyesha shukrani zao kwa yaliyofanyika, mtakuwa mmewapa uhalali wa lile jambo letu lile, watasama yule aliyepita sio amepita kwasababu alistahili, ni amepita kwasababu, mshindani wa ukweli, amefanyiwa figisu ya kubambikiwa kesi mbaya ili kuhalalisha kumhifadhi pahala salama kupisha jambo letu, hivyo aliyeshinda, ameshinda kwasababu ameshindanishwa na kivuli, au vivuli!.

Naendelea kushauri, kale ka simba ka Kizimkazi, kaondolewe kwenye ile cage, katatusumbua sana kwa kelele!.

Tuwape wanachotaka, tungie uwanjani kwenye a level playing field, tuweke refa mtenda haki, mwisho wa mchezo, mshindi apatikane kwa haki, tufurahie ushindi wa hakia, tena kwa hisia zangu, hizi mambo za figisu, zimechagia kwenye ile karma iliyopelelekea lile tukio!.

Mwenye macho na aone,
Mwenye masikio asikie!

Mzee Pasci
Subiri wale walikuzwa na maziwa ya lactogen waanze kukutakana.
Ila uwasamehe maana hawajijui Wala hawajui watendalo.
 
Kwa hii mikopo aliyokopa kwa hiki.kipindi cha miaka yake 4 madarakani ambayo inakaribia kufikia mara 2 ya matangulizi wake aliyekaa miaka 5 unasemaje
 
Leo nilikuwa naangalia mubashara kupitia TBC, uzinduzi wa Daraja la JPM, Kigongo- Busisi, nikakumbuka daraja la Tanzanite, nikakumbuka flyover ya Tazara, Interchange ya Ubungo, Mradi wa JNHPP, nikakumbuka reli ya SGR, serikali kuhamia Dodoma, Ikulu ya Chamwino, mashule, mahospitali, mabarabara kibao, nikajisemea kiukweli Jamaa alikuwa na uthubutu!. Pamoja na wema wote huo, ulipofika muda wa watu kufanya uamuzi, amini usiamini, kuna maeneo watu walimtenda!, ikabidi utumike ule utaratibu wetu ule wa ku nanilii, kama alivyosema Nape!.
Mleta mada (umesema tusitaje majina), nini kinaendelea? Umenistua sana (red bold)
 
Believe me hana guts za mechi yenye level playing field ni muoga mno na uoga wake unakuwa coumpanded na woga wa Msoga yasitokee ya Lowassa.
 
Wanabodi

Mimi mwenzenu, sio tiu nimepiga kura toka uchaguzi wa mwaka 1990 ambao ndio uchaguzi wa mwisho wa chama kimoja!, kwenye urais, tulikuwa tunampigia kura mgombea mmoja anayeshindana na kivuli!

Nimeshiriki nikiwa mwandishi wa habari na kuna wakati nilikuwa mwangalizi, na niliendelea kushiriki chaguzi zote za vyama vingi, toka ule uchaguzi mdogo wa jimbo la Kwahani, 1994, uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, 2020, na sasa 2025, hivyo kuna vitu niliviona naweza kuvitolea ushauri wa busara, hivyo naanzisha mfululizo wa mada zangu za busara za Mzee Pasco.

Mada hizi ni za kiutu uzima, hakuna kutaja taja majina!, na ukijiona unataka kuuliza ni nani au kutaja jina, ujue huu uzi sii saizi yako!.

Mada ya kwanza usemi wa Kiswahili usemao "Haja ya Mja Hunena, Muungwana ni Kitendo" Kumaanisha binadamu wote sio wema, hata uwatendee mema makubwa kiasi gani, ipo siku, atakutenda tuu!, ndio maana. Waswahili wanamsemo wa "Tenda wema uende zako, usisibirie shukrani".

Leo nilikuwa naangalia mubashara kupitia TBC, uzinduzi wa Daraja la JPM, Kigongo- Busisi, nikakumbuka daraja la Tanzanite, nikakumbuka flyover ya Tazara, Interchange ya Ubungo, Mradi wa JNHPP, nikakumbuka reli ya SGR, serikali kuhamia Dodoma, Ikulu ya Chamwino, mashule, mahospitali, mabarabara kibao, nikajisemea kiukweli Jamaa alikuwa na uthubutu!. Pamoja na wema wote huo, ulipofika muda wa watu kufanya uamuzi, amini usiamini, kuna maeneo watu walimtenda!, ikabidi utumike ule utaratibu wetu ule wa ku nanilii, kama alivyosema Nape!.

Sasa kwa mema makubwa mazuri ya kuonekanika anayoyatenda huyu aliyepo, kwanza kwa kukamilisha yale ya mtangulizi wake, kisha kujumlisha na yake anayotenda, kiukweli kabisa, anastahili kushukuriwa kwa kupewa asante stahiki!.

Kitendo cha mtu kufanyiwa wema mkubwa hivi, halafu kuwa mtovu wa fadhila, kuwa mtovu wa shukrani, kutomshukuru mtu kama huyu ni kujichumia tuu dhambi! ya utovu wa fadhila na utovu
wa shukrani.

Watanzania sio watovu wa shukrani kivile!.

Kuna msemo mwingine wa
Kiswahili, unaitwa "kumsukuma mlevi". Unamuona mlevi amelewa chakari, anatembea kwa kuyumba yumba, yaani ni amelewa tilalila!, ukimsukuma kidogo tuu, ni anakwenda chini, na jinsi pombe zilivyomzidia, akienda chini, inaweza kuwa jumla!.

Kufuatia shukrani za Watanzania kwa kilichofanyika, hakuna kabisa sababu ya kumsukuma huyu mlevi, usimsukume kabisaa, huyu mlevi, mwache aendelee kutembea kwa kupepesuka, atajiangukia mwenyewe, bora lawama za kutomsaidia mlevi akaanguka, kuliko fedheha ya kumsukuma mlevi akaanguka ile ya mtolee!.

Asante stahiki kwa huyu aliyepo ni ile asante ya ile siku ya unachukua, unaweka, !, hivyo namshauri aliyepo, awape tuu kila wanachokitaka, hata kama hawastahili, ali mradi, wameomba, wanapiga makelele, wapewe tuu!

Wasipopewa, baada ya Watanzania kuonyesha shukrani zao kwa yaliyofanyika, mtakuwa mmewapa uhalali wa lile jambo letu lile, watasama yule aliyepita sio amepita kwasababu alistahili, ni amepita kwasababu, mshindani wa ukweli, amefanyiwa figisu ya kubambikiwa kesi mbaya ili kuhalalisha kumhifadhi pahala salama kupisha jambo letu, hivyo aliyeshinda, ameshinda kwasababu ameshindanishwa na kivuli, au vivuli!.

Naendelea kushauri, kale ka simba ka Kizimkazi, kaondolewe kwenye ile cage, katatusumbua sana kwa kelele!.

Tuwape wanachotaka, tungie uwanjani kwenye a level playing field, tuweke refa mtenda haki, mwisho wa mchezo, mshindi apatikane kwa haki, tufurahie ushindi wa hakia, tena kwa hisia zangu, hizi mambo za figisu, zimechagia kwenye ile karma iliyopelelekea lile tukio!.

Mwenye macho na aone,
Mwenye masikio asikie!

Mzee Pasci
Binafsi nilikuwamshabiki wa hoja zako ktk jukwaa hili kaka, Ila baads ya kuanza tabia za chawa nikaanza kukupuuza, Ila niovyo kwa Sasa umevuka renki ya kuwa chawa Sasa umefikia viwango vya kunguni, endelea Ila elewa kadri siku zinavyo songa ndiyo unavyopoteza hadhi yako na reputation uloijenga kwa Muda mrefu, nakushauri Bora ukakaa kimya Kama Ndugai kuliko kujipaka kinyesi ilihali hunufaiki nacho.Gd byee.
 
Back
Top Bottom