Kwa jambo hili sintomsahau Mh. John Mnyika!

Kwa jambo hili sintomsahau Mh. John Mnyika!

Amiliki

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2011
Posts
2,085
Reaction score
1,005
Leo ndio nimestuka na kuanza kujiuliza wapi yalipo yale magari ya akina Mringo na wenzake ambayo yalifikia mahali cha kutukosesha amani ya usalama wa watoto wetu kwa kila dakika kupita mitaani huku Kimara yakifanya biashara ya Maji? Tulizoea kuyaona magari mengi sana ya kuuza maji ambapo leo ni vigumu sana kuyaona yakifanya biashara hiyo.

Kila mwenye pesa yake wakati huo Kimara hakuwa ameona biashara nyingine ya kufanya zaidi ya kuuza maji maana ndiyo biashara iliyokuwa maarufu sana na inatoka sana huku Kimara.

Leo hii wengi wameshabadilisha matumizi ya magari yale kwa kukosa wateja kwani tatizo la Maji Kimara limepungua kwa kiwango kikubwa sana kama si kukaribia kwisha.

Je waliomtangulia akina Keenja, Ngula n.k walishindwa kabisa kuona kwamba hiki kitu kinawezekana kiasi cha kuwaruhusu akina Diwani(CCM) Mringo kupata utajiri kwa biashara hiyo huku wakifanya kila jitihada maji yasipatikane Kimara ili wao wauze?

Heko JJ. Mnyika, Mbunge wangu.


 
Hahaha! Mkuu ulivyoandika tu au simu yangu inaonesha vibaya! Japo nimekupata!
 
huyo ndo JJ, sikujali usingizi wangu kukesha kwa ajili ya kulinda kura zake...

ha ha ha kumbe tulikuwa pamoja ile cku, ngoja kuna watu wnakaa lumumba watakwambia ni uongo, mimi nipo hapa k/ngule ni kweli mnyika amefanikiwa hili
 
Pamoja na kupata maji ya uhakika, siku hizi hata tukiwa maofisini hatuna wasi wa watoto zetu kugongwa na magari chakavu ya maji ambayo yalikuwa hayakauki mtaani!
What more can one say about that!
 
kimara ipi mkuu mbona tembon.kwa msuguri.kibanda cha mkaa.suka.stop ove.bunyokwa.king'ongo.bwalon na nk bado watu wanafanya biashara sana tu.na maji hakuna
 
kimara ipi mkuu mbona tembon.kwa msuguri.kibanda cha mkaa.suka.stop ove.bunyokwa.king'ongo.bwalon na nk bado watu wanafanya biashara sana tu.na maji hakuna

Tuiulize serkar yako ya magamba kwann hakuna maji........??
 
My Web... Suka ipi unayoizungumzia ,.... Mimi na kaa Suka nyuma ya kanisa la Roma kabla ya kufika kwenye ukumbi wa Mbiro na tunauhakika wa maji siku tatu kwa week ... yaani Jmosi, jnne na Alhamisi wakati enzi zile maji ilikuwa mpaka msubirie mvua au mnunue kwenye malori ya X Diwani

My Web kuwa mkweli na sidhani kama unaishi SUKA kweli .... Mimi ni member wa Bufalo na Suca Bar washkaji wote kule upande wa Golani na Temboni watakubaliana nami hali imebadilika sana tena sana siku hizi hata pale wanapojazia maji karibu na Gerage hukuti maroli ya maji yamejazana

mimi siyo mwanasiasa but haki ya mtu mpeni... mnyika amejitahidi sana kwa hilo
 
Mkuu Kimbunga,

Wewe ni mkazi wa Kimara hebu tufahamishe maji yapo.
 
Last edited by a moderator:
Miongoni mwa wabunge majembe ya cdm hutashindwa kumtaja JJ Mnyika, ni mbunge makini sana mwenye kuwajibika kwa wananchi moja kwa moja. Jembe jingine ni la mbozi magharibi Mh. Silinde naye huyu jimboni kwake kafanya mambo makubwa sana.
Hongera sana majembe ya cdm
 
Chadema ni mkombozi wetu,hongera sana kamanda Mnyika,tunaomba mkatusemee bungeni na hivi vikamudhi vinavyotuzingua sasa tufanyeje?
 
Amiliki inawezekana kuna uafadhali katika upatikanaji wa maji baadhi ya sehemu tu, kuanzia stop over kwenda mpaka mbezi kwa yusufu vurumai ya magari ya maji bado iko vilevile kama zamani. kuna maeneo mengi sana ambayo hayajui maji ya bomba; makabe, mshikamano, msumi nk huku kote maji ni bidhaa adimu sana pamoja na kuwa karibu sana(2km) na linapopita bomba kubwa la maji ambalo amebinafsishiwa mtu binafsi anayewauzia wenye magari ili watuuzie. Mkuu shida ya maji bado kubwa sana.
 
Pamoja na kupata maji ya uhakika, siku hizi hata tukiwa maofisini hatuna wasi wa watoto zetu kugongwa na magari chakavu ya maji ambayo yalikuwa hayaka..
What more can one say about that!
Mh Mnyika amebakisha huku kwetu Changanyikeni. Bado tunachanganywa na kuchanganyikiwa na shida ya maji
 
Back
Top Bottom